Chuki Simba na Yanga

Hata mimi nashangaa siyo utani wa jadi Tena Bali chuki ya jadi
 
Hajui kwamba Derby namba moja duniani River Plate ns Boca Junior sometimes hadi wanahamisha mechi na kupelekwa nchi nyingine kisa vurugu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndo utani wenyewe hamna chuki hapo,ushindani ni mkali ndo maana kila mtu anamwombea mwenzake mabaya maana moja akifaulu mwingine anaanza kumcheka mwenzake, mbona sisi mashabiki ndo tunaona starehe kubishana hivo.

Na kwenye familia zetu baba kama siyo Simba basi Yanga,na watoto hivo hivo pia na hakuna kugombana,sasa kutakuwa na raha gani watu wote kushabikia upande mmoja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa utafiti mdogo tu wenye tabia hizo ni mashabiki waliozaliwa kuanzia mwaka 1990 kuja mbele

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Sidhani kama nchi za ulimwengu wa kwanza zina tabia kama hizi
Kule ndiyo hatari zaidi nafuu huku Tanzania kuna Amani hizi kelele unazoona ni maneno ya mtandaoni tu .
Ukiangalia boca junior na river plate au flamingo na vasco da gama utaelewa nini namaanisha.
Uje Liverpool na man United au inter Milan na ac Milan au juventus na ac Milan au Barcelona na Real Madrid utaelewa nini namaanisha .
 
Halafu wameingia hawa watu wapuuzi na hovyo wenye kuitwa maafisa habari ndio wanazidi kuipanda mbegu ya chuki!
 
Wabongo ndivyo mlivyo, hasa simba na yanga ni chuki juu ya chuki
 
Soka limeingiliwa n wachumia Tumbo...polepole wanabadioisha utani wa jadi kuwa chuki! Unapoona waandishi ,wachakbuzi nao wanaingi humo hiyo ni Hatari!
Na hao wachumia tumbo.ni mahodari wa propaganda na wanatumia gharama kubwa kulevya watu!
Leo hii shabiki wa Simba analishwa ujinga kihangaika na ya Yañga!
Upande wapili ni yaleyale!
Leo hii mashabiki wa Yañga wanaiita Simba .eti Mwakarobo! Na watu wanaimba ..Halafu huo anaye Cheka ,alikuwa hajjaingia Hatua ya Makundi ( sio robo) Kwa miaka 25! Hali anayechekwa amechrza mara Nne ndani ya miaka 6 !
Inahitaji upumbavu wa Daraja la juu kubebwa na upepo huo!
 
Huu unaoendelea sasa sio utani mkuu, ni kitu kingine kabisa ila kimejificha kwa jina la utani. Chunguza vizuri
Boss Hujui Mpira, Na siku wakiacha tu kuchukiana basi na hamasa ya watu kujaa uwanjani imeishia hapo....

Si unaona nchi nyengine wakienda huko viwanja ni vyeupe kabisa?? Unajua wanakosa nini?? Wanakosa Mafahari wanaochukiana.
 
Mkuu huu ndo UTANI WA JADI, wala hatuchukiani.

Tungechukiana ungeona tumeingia vitani kama Gaza.

Ujifungwa mrani atakucheka tu.
Tofautusha chuki na UTANI WA JADI
 
Ni ushamba na ulimbukeni tu. Mchezo wa mpira umeingiliwa na watu wasioujua mpira bali ni washabiki tu timu.
 
Tanzania tunaamini sekta ya burudani hainogi bila mashabiki wa upande fulani kutukanana na wa upande mwingine, refer hata kwenye muziki mashabiki wa Diamond vs Alikiba au kwenye filamu enzi za Kanumba vs Ray nk, yani kila mahali tunalazimisha kuweka utimu ambao baadaye hukomaa na kuwa uadui sasa
 
Usichukulie serious sana, hao ni watani...
 
Chuki ndiyo inafanya tupate furaha sana pale mtani yanapomkuta mabaya akiwa uwanjani..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…