Chukua hatua dhidi ya maradhi ya ulaji mbovu

Chukua hatua dhidi ya maradhi ya ulaji mbovu

bryan2

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2016
Posts
3,323
Reaction score
4,679
Wapendwa afya ni mtaji kwa kila kitu ukitaka kufahamu hilo umwa hata mafua tu ndio utajua afya ikipata shida kidogo tu hakika mwili ndio unaumia na hatimaye kudhoofu na kuchoka kabisa na mhusika kukosa furaha/amani.

Ukitaka kujua afya ni mtaji angalia ule msafara kwa kwenda kwa Babu Loliondo-Samunge hakika kila mtu alitaka kupiga kikombe either kupata nafuu au kupona kabisa maradhi yaliyokua yanamsumbua.

Kichwa cha mada kinahusika, sasa ulaji mbovu pamoja na madhara yake pasipo na shaka linaenda kuwa tatizo la kitaifa soon.

Siku hizi watu haumwi sana malaria au kifua kikuu magonjwa yatokanayo na ulaji mbovu yanakuja kwa kasi. Na baadhi ya magonjwa hayo ni kama vile;

- Sukari ya Juu/diabetes Mellitus

- Shinikizo la juu la damu/hypertension

- Uzito mkubwa/overweight

- Gout

- Magonjwa ya mifupa/rheumatoid athritis nk.

Magonjwa hayo na mengineyo hakika yamekua changamoto kuna asilimia kubwa sana kuongezeka kwa magonjwa hayo sio vijana wala wazee. Ukiangalia kliniki ya maradhi hayo watu wanavyojaa ndio utajua kuna shida zaidi.

Ubaya watu wanakula hovyo halafu hakuna mazoezi mtu anakula chapati na supu asubuhi then anakaa ofisini mchana anakula chips then ofisini akirudi nyumbani ugali mkubwa then kulala hakuna mazoezi zaidi maradhi hayo bado kuna kuvimbiwa tena maudhi madogo madogo.

Bila kusahau vidonda vya tumbo/pud, mafuta kuwa juu/cholestrol/hyperlipidaemia, bado ni matokeo ya ulaji mbovu.

Hili ni suala mtambuka kuanzia kwenye jamii hadi taifa, watu waelekezwe ulaji bora, kuna wataalamu wa lishe kila wilaya wafundishe watu.

Kuwe na siku ya kitaifa ya kufanya mazoezi, litiliwe mkazo hasa watumishi wa ofisi za umma na binafsi, pia kwa mtu binafsi jipangie ratiba ya kupiga matizi.

Tuepuke vyakula hatarishi kwa afya zetu na pia tuwe na tabia za kupima afya zetu tusingoje tuwe hoi ndio tukimbilie hospitali.

Chagua afya bora kwa maendeleo yako na taifa.
 
Vijana wengi siku hizi full kula junk food ndio maana biashara ya dawa za nguvu za kiume inalipa Sana
 
Wako busy na kutoa ufafanuzi wa tozo badala na mambo Kama haya ya kitaifa wayasemehe katika ngazi ya taifa...ishu nyingi Kuna ndoa kuvunjika walipaswa Kama viongozi wahoji watu wawe na awareness
 
Hapo umetugusa wengi.

Tupe basi ata schedule kidogo.

Mfano: usile ABC kula xyz au kwa siku tembea ata 5,km kunywa maji lita ,2 lala masaa 6 etc
 
Hapo umetugusa wengi.

Tupe basi ata schedule kidogo.

Mfano: usile ABC kula xyz au kwa siku tembea ata 5,km kunywa maji lita ,2 lala masaa 6 etc

Cha msingi ni kula a well balance diet i mean mlo kamili safi kama huna maradhi kama Sukari, kama upo na sukari punguza Wanga kabisa igawe robo mboga za majani ya kutosha, kunywa maji ya kutosha.

Piga mazoezi yasaidie kuchoma hizo fatts angalua walking for 30-45mnts ni zoezi tosha per day.

Chakula cha usiku wahi kula then kaa masaa mawili ndio ukalale at least 6-8hrs per day
 
Hapo umetugusa wengi.

Tupe basi ata schedule kidogo.

Mfano: usile ABC kula xyz au kwa siku tembea ata 5,km kunywa maji lita ,2 lala masaa 6 etc
Ngoja me nikusaidie accordingly to my mentor dokta mmoja Yuko tabata liwiti ana ka Clinic pale ni mpakistani anatibu kwa kutumia Tiba unani ya ugiriki he was once my best friend tulikuwa very close Hadi akanipa formula anazotumia yeye





1.hali chochote kile isipokuwa chapati kavu,choroko, mamung'unya,tembere kabichi tikitimaji na tango na maziwamtindi sio Yale machachu kabisa.
2.maji litanne kwa siku

3.asubuhi anakimbia tabata mpka kariakoo na tukifanya wote hii jogging jion tunacheza tennis isiyotumia racket...he is very tough guy..ana group lipo fb Kama ukilihitaji kusoma physiological ideas...NI hayo TU.
 
Ahsante kwa ushauri

Ndio maana ulimsikia Waziri wa Afya akisema Non Communicable diseases zimeongezeka kwa kasi zinatishia uhai wa Bima its true kutibu non communicable ni expensive assume mtu kapata Hypertension then kapata Stroke kipimo cha Stroke either Ct Scan or Mri ni ghali.

Wanatakiwa wafanye primary Prevention na Sio Secondary prevention or Tertiary
 
Cha msingi ni kula a well balance diet i mean mlo kamili safi kama huna maradhi kama Sukari, kama upo na sukari punguza Wanga kabisa igawe robo mboga za majani ya kutosha, kunywa maji ya kutosha.

Piga mazoezi yasaidie kuchoma hizo fatts angalua walking for 30-45mnts ni zoezi tosha per day.

Chakula cha usiku wahi kula then kaa masaa mawili ndio ukalale at least 6-8hrs per day
Unapendekeza idadi ya milo mingapi kwa siku?
 
Ngoja me nikusaidie accordingly to my mentor dokta mmoja Yuko tabata liwiti ana ka Clinic pale ni mpakistani anatibu kwa kutumia Tiba unani ya ugiriki he was once my best friend tulikuwa very close Hadi akanipa formula anazotumia yeye





1.hali chochote kile isipokuwa chapati kavu,choroko, mamung'unya,tembere kabichi tikitimaji na tango na maziwamtindi sio Yale machachu kabisa.
2.maji litanne kwa siku

3.asubuhi anakimbia tabata mpka kariakoo na tukifanya wote hii jogging jion tunacheza tennis isiyotumia racket...he is very tough guy..ana group lipo fb Kama ukilihitaji kusoma physiological ideas...NI hayo TU.

Ntapita kwenye grupu nikapate Nondo shida kubwa Watanzania kupuuza mambo ya msingi na kudili na mambo ya ajabu mtu mpaka apate tatizo ndio anaanza kuhangaika
 
Unapendekeza idadi ya milo mingapi kwa siku?

Kama huna tatizo 3 meals ni sawa ila je unakula nini na kama unaweza pia 2 meals its ok kama huna shida ya vidonda vya tumbo na matatizo mengine ya kiafya manake kushinda njaa sio suluhisho shida unakula nini

Kuna mwana anashinda njaa ila jioni anakula plate 3 tena mawanga
 
Wapendwa afya ni mtaji kwa kila kitu ukitaka kufahamu hilo umwa hata mafua tu ndio utajua afya ikipata shida kidogo tu hakika mwili ndio unaumia na hatimaye kudhoofu na kuchoka kabisa na mhusika kukosa furaha/amani.

Ukitaka kujua afya ni mtaji angalia ule msafara kwa kwenda kwa Babu Loliondo-Samunge hakika kila mtu alitaka kupiga kikombe either kupata nafuu au kupona kabisa maradhi yaliyokua yanamsumbua.

Kichwa cha mada kinahusika, sasa ulaji mbovu pamoja na madhara yake pasipo na shaka linaenda kuwa tatizo la kitaifa soon.

Siku hizi watu haumwi sana malaria au kifua kikuu magonjwa yatokanayo na ulaji mbovu yanakuja kwa kasi. Na baadhi ya magonjwa hayo ni kama vile;

- Sukari ya Juu/diabetes Mellitus

- Shinikizo la juu la damu/hypertension

- Uzito mkubwa/overweight

- Gout

- Magonjwa ya mifupa/rheumatoid athritis nk.

Magonjwa hayo na mengineyo hakika yamekua changamoto kuna asilimia kubwa sana kuongezeka kwa magonjwa hayo sio vijana wala wazee. Ukiangalia kliniki ya maradhi hayo watu wanavyojaa ndio utajua kuna shida zaidi.

Ubaya watu wanakula hovyo halafu hakuna mazoezi mtu anakula chapati na supu asubuhi then anakaa ofisini mchana anakula chips then ofisini akirudi nyumbani ugali mkubwa then kulala hakuna mazoezi zaidi maradhi hayo bado kuna kuvimbiwa tena maudhi madogo madogo.

Bila kusahau vidonda vya tumbo/pud, mafuta kuwa juu/cholestrol/hyperlipidaemia, bado ni matokeo ya ulaji mbovu.

Hili ni suala mtambuka kuanzia kwenye jamii hadi taifa, watu waelekezwe ulaji bora, kuna wataalamu wa lishe kila wilaya wafundishe watu.

Kuwe na siku ya kitaifa ya kufanya mazoezi, litiliwe mkazo hasa watumishi wa ofisi za umma na binafsi, pia kwa mtu binafsi jipangie ratiba ya kupiga matizi.

Tuepuke vyakula hatarishi kwa afya zetu na pia tuwe na tabia za kupima afya zetu tusingoje tuwe hoi ndio tukimbilie hospitali.

Chagua afya bora kwa maendeleo yako na taifa.
Upime afya ya nini wewe...utapima siku ngoma imekohoa. Sasa mtu mzima unaendesha shughuli zako vizuri tuu unaenda kupima afya ili iweje?
 
Upime afya ya nini wewe...utapima siku ngoma imekohoa. Sasa mtu mzima unaendesha shughuli zako vizuri tuu unaenda kupima afya ili iweje?

Kiongozi regular check up ni kitu poa sana ugonjwa kama Hypertension tunasema ni Silent killer siku unajulikana upo nusu ya kufa sio ajabu ukakuchapa na stroke/kiharusi

Assume unachapwa na Kiharusi/stroke unakaa kwa bed 10yrz hakuna kukufa wewe unageuzwa kila siku mwisho wa siku ndugu wanaanza kukuchoka, hakuna kufanya kazi umaskini mkubwa unakuja kwa nyumba

Kwa kitu ambayo ungeweza kuzuia
 
Hoja yako nzuri ila subiri kushambuliwa. Utasikia kama kufa kupo tu. Una weza kugongwa na gari ukafa. Juzi mwingine humu jamvini anasema hata wembamba wanapata kisukari hivyo acheni watu wale watakavyo. Huwa naona prof janabi anavyoshambuliwa na watu kwa mada zake za ulaji wa hovyo mpaka nasema suala la afya mtu aachwe mwenyewe yakimkuta ndio akili itamkaa sawa
 
Hoja yako nzuri ila subiri kushambuliwa. Utasikia kama kufa kupo tu. Una weza kugongwa na gari ukafa. Juzi mwingine humu jamvini anasema hata wembamba wanapata kisukari hivyo acheni watu wale watakavyo. Huwa naona prof janabi anavyoshambuliwa na watu kwa mada zake za ulaji wa hovyo mpaka nasema suala la afya mtu aachwe mwenyewe yakimkuta ndio akili itamkaa sawa

Sawa kiongozi, mtu anaweza kubisha sababu hajakutana nayo either yeye or kwenye familia ni vema mtu asisubiri mpaka afike mahari akatazwe kula nyama na daktari au chumvi.

Tujifunze kubalance kila kitu
 
Kiongozi regular check up ni kitu poa sana ugonjwa kama Hypertension tunasema ni Silent killer siku unajulikana upo nusu ya kufa sio ajabu ukakuchapa na stroke/kiharusi

Assume unachapwa na Kiharusi/stroke unakaa kwa bed 10yrz hakuna kukufa wewe unageuzwa kila siku mwisho wa siku ndugu wanaanza kukuchoka, hakuna kufanya kazi umaskini mkubwa unakuja kwa nyumba

Kwa kitu ambayo ungeweza kuzuia
Wewe bwana haya mambo ya afya haya magonjwa yasio ya kuambukizwa hayana ujanja ni kuomba mungu tuu.
Unaweza kuwa mtu wakuangalia chakula na kufanya zoezi u apigwa na cancer. Acha tuu
 
Back
Top Bottom