DOKEZO Chuo cha IFM hakijatoa vyeti vya Wahitimu wa 2023/2024 na hakuna maelezo ya kueleweka

DOKEZO Chuo cha IFM hakijatoa vyeti vya Wahitimu wa 2023/2024 na hakuna maelezo ya kueleweka

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

KwetuKwanza

Member
Joined
Mar 13, 2023
Posts
82
Reaction score
150
Sisi Wahitimu wa ngazi ya Shahada wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) kutoka kampasi zote wa Mwaka wa Masomo 2023/2024 tunakabiliwa na changamoto kubwa ya ucheleweshaji wa vyeti licha ya kufuzu masomo.

1. Kukosa Fursa za Kazi: Ucheleweshaji wa vyeti unatuzuia wahitimu kuomba nafasi za ajira zinazohitaji cheti kama kigezo muhimu, hali inayowaweka katika changamoto za kifedha na kijamii.

2. Kucheleweshwa Maendeleo ya Kitaaluma kwa wanaohitaji kuendelea na masomo: Wahitimu wanakosa nafasi za kujiendeleza kielimu katika shahada za juu ndani na nje ya nchi, jambo linalozorotesha mipango yao ya maisha.

Natoa wito kwa IFM na mamlaka husika kuchukua hatua za haraka kutatua changamoto hii ili kulinda maslahi ya wahitimu hawa.

Vyeti vilitakiwa kutoka tangu Desemba 2024 lakini sasa ni Februari 2025 hakuna majibu yaliyonyooka, kila tukienda kuuliza tunaambiwa wanashughulikia.

Tetesi zilizopo ni kuwa Chuo kinadaiwa na Mzabuni wa Serikali, kuna malimbikizo ya malipo hayajafanyika, hivyo Mzabuni amegoma kuwapatia vyeti, kama hivyo ni kweli basi tunaumia sisi ambao hatuhusiki na hayo makosa ya Uongozi wa Chuo.

RAIS WA WANAFUNZI IFM
JamiiForums
imewasiliana na Rais wa Wanafunzi wa IFM, Fabian Cornelius Mkondo kuhusu hoja hiyo, amesema:

“Ni kweli nilipata malalamiko hayo, siyo jambo gani, nimelifikisha kwa viongozi wa chuo wanaohusika wanalishughuliki, mimi pia nalifanyia kazi kwa upande wa levo yangu.

“Chuo kipo kwenye kipindi cha mitihani, ndio maana ‘focus’ ipo huko sana lakini naamini Chuo kitashughulikia na suala hilo litamalizika.”

Jitihada za JamiiForums kuutafuta Uongozi wa Chuo cha IFM zinaendelea.
 
Naomba niku karibishe rasmi katika chama pendwa Cha ma jobless pro max.

Upendo, umoja na utu ndio vipaumbele vyetu.

Mimi Intelligent businessman ni raisi wa chama cha ma jobless pro max, makamu ni Bolotoba,
katibu ni min -me, wakili wa ma jobless ni Selikavu, waziri wa mambo ya ndani Thecoder, msajili wa chama Cha ma jobless ni dosho12, mratibu wa mipango ni Edo kissy

Msemaji wa chama Cha ma jobless pro max ni makutupora

Kidumu chama Cha ma jobless pro max
OIG3.jpeg
 
Naomba niku karibishe rasmi katika chama pendwa Cha ma jobless pro max.

Upendo, umoja na utu ndio vipaumbele vyetu.

Mimi Intelligent businessman ni raisi wa chama cha ma jobless pro max, makamu ni Bolotoba,
katibu ni min -me, wakili wa ma jobless ni Selikavu, waziri wa mambo ya ndani Thecoder, msajili wa chama Cha ma jobless ni dosho12, mratibu wa mipango ni Edo kissy

Msemaji wa chama Cha ma jobless pro max ni makutupora

Kidumu chama Cha ma jobless pro max
View attachment 3233118
Karibu sanaaa

Hukuna michango
Hakuna nongwa.
Hakuna fedheha
 
Naomba niku karibishe rasmi katika chama pendwa Cha ma jobless pro max.

Upendo, umoja na utu ndio vipaumbele vyetu.

Mimi Intelligent businessman ni raisi wa chama cha ma jobless pro max, makamu ni Bolotoba,
katibu ni min -me, wakili wa ma jobless ni Selikavu, waziri wa mambo ya ndani Thecoder, msajili wa chama Cha ma jobless ni dosho12, mratibu wa mipango ni Edo kissy

Msemaji wa chama Cha ma jobless pro max ni makutupora

Kidumu chama Cha ma jobless pro max
View attachment 3233118
Kaona kazi TRA analialia oya kuna wenzio wana miaka 10 mtaani huku hawana ajira na vyeti wanavyo tena vimenyooka vipo tu vinapigwa na mavumbi wengine wameomba interview hawaitwi mpaka wamesahau kabisa
 
Inatakiwa ukimaliza chuo matokeo yakatoka huna shida upate cheti chako lakini ajabu watu hukaa hata miaka 2 hawajapata vyeti. Mambo ya hovyo sana.
 
Next week labda kama kutembeza majagi 😁 ila ajira ya kulipwa hela nzuri haipatikani kirahisi. Kutembeza majagi hakuhitaji hata cheti
Sikuhizi vijana wamehamia kwenye kucheza dili chafu tu win win situation sitozitaja hapa ila kifo nje nje
 
Hii ingependeza pia ikapandishwa kwenye kurasa rasmi za Jamii Forum zenye wafatiliaji wengi kama vile Instagram ili kuweza kuwasaidia wahitimu kwa haraka na kuwafikia wenye mamlaka mapema
 
Kuna kitu hakiko sawa kwa IFM nzima na ujumla wake , kile chuo pale watoto wanalipa ada zaidi ya 1.7M kwa mwaka , utadhani private kuna mahali chuo kimekwama serikali ingilie kati watoto wapewa
Vyeti vyao
 
Back
Top Bottom