Chuo cha Uhasibu Arusha kutoa mafunzo ya Uhasibu, Tehama na Uongozi Comoro

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797
Chuo cha Uhasibu Arusha kutoa mafunzo ya Uhasibu, Tehama na Uongozi Comoro

Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Profesa Eliamani Sedoyeka anaongoza ujumbe wa chuo hicho katika mazungumzo na Chuo Kikuu cha Comoro ili kuanzisha ushirikiano utakaowezesha wanafunzi wa Comoro kupata mafunzo toka IAA.

Katika mazungumzo hayo yanayoendelea nchini Comoro, Profesa Sedoyeka alimjulisha mwenyeji wake, Mkuu wa Chuo cha Comoro Prof Ali Tabibu Iburoi maeneo ambayo IAA ingependa kujikita nchini Comoro kuwa ni Uhasibu, Fedha, Utawala Bora, Tehama na pia kuwa washauri katika maeneo mkakati kulingana na vipaumbele vya Serikali ya Comoro.

Hivi karibuni Rais Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alielekeza Taasisi na Mashirika ya Umma kuangazia fursa nje ya mipaka ya Tanzania na juhudi hizo za IAA ni sehemu ya utekelezaji wa agizo hilo.


Ziara hiyo imeratibiwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Comoro ambapo Balozi wake, Mhe. Saidi Yakubu alieleza ujumbe huo utakutana pia na Gavana wa Benki Kuu na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Maendeleo ya Dijitali nchini Comoro na kutembelea vitivo kadhaa vya Chuo Kikuu cha Comoro.
 

Attachments

  • mini_magick20241104-32263-c6enh8.jpg
    157.6 KB · Views: 5
  • mini_magick20241104-32263-q7w17f.jpg
    164.5 KB · Views: 7
  • mini_magick20241104-32263-2y83hz.jpg
    142 KB · Views: 5
  • mini_magick20241104-32263-1pt2vy.jpg
    136.3 KB · Views: 6
  • mini_magick20241104-32263-h9299t.jpg
    103.6 KB · Views: 5
  • mini_magick20241104-32263-8q8f46.jpg
    235.9 KB · Views: 9
  • mini_magick20241104-32263-f9t1j6.jpg
    119.4 KB · Views: 7
Kwetu tu elimu hii imeonekana haina tija tena maana haiendani na uhalisia wa kuyabadili maisha ya vijana bongo,labda kwa huko itakuwa na tija
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…