Chuo cha Ukamanda (CSC) chatoa tuzo kwa Mati Super, chapongeza Maafisa wa Kijeshi kupewa mafunzo

Chuo cha Ukamanda (CSC) chatoa tuzo kwa Mati Super, chapongeza Maafisa wa Kijeshi kupewa mafunzo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
a1e98cef-1999-4e2c-a662-ceea292cf6f0.jpg
Kampuni ya Mati Super Brands Limited inayozalisha vinywaji changamshi yenye makao yake Makuu Mjini Babati Mkoani Manyara imepewa tuzo ya maalumu kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (CSC) kwa kutambua mchango wa kampuni hiyo katika kusaidia jamii inayowazunguka Pamoja na kushirikiana na taasisi mbali mbali za kiserikali.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo na Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (CSC) chenye makao yake Mkoani Arusha, Colonel Verus Chrysostom Mbuzi katika ziara maalumu ya kimafunzo iliyofanywa na Maafisa hao wa ngazi za juu wa Kijeshi kutoka mataifa mbalimbali katika Kampuni ya Mati Super Brands Ltd.
587041f5-2e8e-4308-a509-22f0c2132448.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mati Super Brands Limited, David Mulokozi ametoa shukrani zake kwa Chuo hicho cha kijeshi kwa kutambua mchango wa kampuni hiyo katika masuala mbalimbali ikiwemo kurudisha sehemu ya faida wanayoipata kwa jamii inayowazunguka.

Mulokozi amesema kuwa Tuzo hiyo inawapa chachu ya kuendelea kufanya vizuri kuendelea kushirikiana na taasisi za umma Pamoja na kuzalisha bidhaa bora zinazozingatia ubora na usalama wa mtumiaji.

Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (CSC), Colonel Verus Chrysostom Mbuzi amepongeza Kiwanda kwa kuwa karibu na jamii na taasisi za Serikali pamoja na kutoa fursa wa mafunzo kwa vitendo vya Maafisa wa Kijeshi juu ya masuala mbalimbali ikiwemo usalama wa chakula.
 
Kampuni ya Mati Super Brands Limited inayozalisha vinywaji changamshi yenye makao yake Makuu Mjini Babati Mkoani Manyara imepewa tuzo ya maalumu kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (CSC) kwa kutambua mchango wa kampuni hiyo katika kusaidia jamii inayowazunguka Pamoja na kushirikiana na taasisi mbali mbali za kiserikali.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo na Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (CSC) chenye makao yake Mkoani Arusha, Colonel Verus Chrysostom Mbuzi katika ziara maalumu ya kimafunzo iliyofanywa na Maafisa hao wa ngazi za juu wa Kijeshi kutoka mataifa mbalimbali katika Kampuni ya Mati Super Brands Ltd.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mati Super Brands Limited, David Mulokozi ametoa shukrani zake kwa Chuo hicho cha kijeshi kwa kutambua mchango wa kampuni hiyo katika masuala mbalimbali ikiwemo kurudisha sehemu ya faida wanayoipata kwa jamii inayowazunguka.

Mulokozi amesema kuwa Tuzo hiyo inawapa chachu ya kuendelea kufanya vizuri kuendelea kushirikiana na taasisi za umma Pamoja na kuzalisha bidhaa bora zinazozingatia ubora na usalama wa mtumiaji.

Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (CSC), Colonel Verus Chrysostom Mbuzi amepongeza Kiwanda kwa kuwa karibu na jamii na taasisi za Serikali pamoja na kutoa fursa wa mafunzo kwa vitendo vya Maafisa wa Kijeshi juu ya masuala mbalimbali ikiwemo usalama wa chakula.
Command and staff college.......wameonja visunguraaaa khaaa basi sawaaa
 
Back
Top Bottom