Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ni cha Serikali?

Chuo Kikuu Huria cha Tanzania ni cha Serikali?

Sumba-Wanga

JF-Expert Member
Joined
Feb 2, 2011
Posts
5,353
Reaction score
1,234
Nimekuwa najiuliza kama Chuo Kikuu Huria au OUT ni chuo cha serikali. Inakuwaje chuo cha serikali kikawa na mambo ya ajabu namna hii?

Sisi Walimu kutoka nje tuliofanya kazi kama external examiners kwenye kazi za wanafunzi tuna zaidi ya miezi 6 hatujalipwa. Tukiuliza tunaambiwa utaratibu mpya wa Muse unachelewesha malipo. Jambo la ajabu, vyuo vingine vya serikali, kama UDSM na SUA vinavyotumia mfumo huo wa Muse, external examiners wanalipwa.

Haijaishia hapo. Hata wafanyakazi wa OUT hawajapata stahiki zao mbali mbali,.kisingizio kikubwa ni mfumo wa Muse. Hii Muse ya OUT ni tofauti na nyingine?

Swali la kujiuliza, viongozi wa OUT hawalioni hili? Jibu ni rahisi tu, wao wanapata pesa za kusafiri kila wanapotaka, tena ni misululu ya wapambe. Kwa jinsi, hawana haka ya kuhangaikia mfumo ufanye kazi. Everybody for himself, God for us all.

Mwenye macho haambiwi Tazama!

Mungu ibariki Muse,
Mungu bariki viongozi wa OUT
Mungu ibariki Tanzania.
 
Double standards inakatisha sana tamaa ya kufanya kazi kwa bidii
 
Uzalendo kwa wengine tu huku wao wakijilipa 3M - 30M per month.

Uzalendo kwa wengine huku wao wakiwa ndani ya Ma V8.

Uzalendo kwa wengine huku wao wakivaa suti.

Uzalendo kwa wengine tu huku wao wakiishi kwenye majumba ya kifahari.

Nk.

NENO UZALENDO NI PANA SANA.
 
Uzalendo kwa wengine tu huku wao wakijilipa 3M - 30M per month.

Uzalendo kwa wengine huku wao wakiwa ndani ya Ma V8.

Uzalendo kwa wengine huku wao wakivaa suti.

Uzalendo kwa wengine tu huku wao wakiishi kwenye majumba ya kifahari.

Nk.

NENO UZALENDO NI PANA SANA.

Kwa hakika:

Wao = ma CCM

Ni sahihi zaidi.

Hawa wanaweza kuwa na vinasaba nao.
 
OUT ni wababaishaji balaa. Kuna mdogo wangu anasoma ualimu, alifanya TP mwezi w tatu hadi leo hawajamuwekea matokeo.
 
Uzalendo kwa wengine tu huku wao wakijilipa 3M - 30M per month.

Uzalendo kwa wengine huku wao wakiwa ndani ya Ma V8.

Uzalendo kwa wengine huku wao wakivaa suti.

Uzalendo kwa wengine tu huku wao wakiishi kwenye majumba ya kifahari.

Nk.

NENO UZALENDO NI PANA SANA.
Katika kitu nisicho taka kukisikia ni neno uzalendo,ivi uzalendo ni kitu gan? Ikiwa wew unalipwa m10 per month wakati mimi nalipwa laki 4 pumbavu kabisa
 
Katika kitu nisicho taka kukisikia ni neno uzalendo,ivi uzalendo ni kitu gan? Ikiwa wew unalipwa m10 per month wakati mimi nalipwa laki 4 pumbavu kabisa
Uzalendo ni kuwaminya wanaonyonywa ili watawala waendelee kunufaika na kula vizuri na familia zao.

Mtu analipwa 25M wakati huku kijijini wamekosa kisima cha 8M tu ili waache kunywa maji kwenye madimbwi NI UKATILI NA UNYAMA WA HALI YA JUU SANA.
 
OUT ni wababaishaji balaa. Kuna mdogo wangu anasoma ualimu, alifanya TP mwezi w tatu hadi leo hawajamuwekea matokeo.
Hawawezi kuwa makini. Kama malipo halali ya external examiners na staff yanashindikana.

Chief Executive Officer, amechukua hatua gani?

Au kwa sababu mambo yake yanakwenda vizuri, hana habari na staff wala wengine?
 
Hii ni taasisi ya serikali. Nina imani swala hili litafanyiwa kazi.

Kama kuna ukweli kwenye hili, pumba na chenga zitaonekana.

Poleni external examiners.

Poleni Staff wa OUT, ambao mnatumia pesa zenu kutoka mikoani kwenye makao makuu kusahihisha mitihani, na MNAKOPWA kisa MUSE haifanyi kazi.

Mheshimiwa Mwigulu Nchemba yumo humu
 
Hii ni taasisi ya serikali. Nina imani swala hili litafanyiwa kazi.

Kama kuna ukweli kwenye hili, pumba na chenga zitaonekana.

Poleni external examiners.

Poleni Staff wa OUT, ambao mnatumia pesa zenu kutoka mikoani kwenye makao makuu kusahihisha mitihani, na MNAKOPWA kisa MUSE haifanyi kazi.

Mheshimiwa Mwigulu Nchemba yumo humu
Duh pole

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom