Nilifurahi sana Chuo Kikuu Huria kilipoanzishwa hapa nchini. Nafurahi sana pia kuona kuwa Watanzania wengi wamejiunga na chuo hiki kiasi kwamba kama kisingekuwapo basi watu wengi wangekosa nafasi ya kujiendeleza hasa kwa kiwango cha elimu ya chuo kikuu. Kuna wanafunzi wa rika zote: vijana sana, vijana wa kati, middle age na wazee. Hii ni nzuri!
Kinachonisikitisha ni huduma duni na ukosefu wa ufanisi mzuri katika kutunza data na kuhakiki kazi za wanafunzi. Hii inakatisha tamaa sana! Halafu pia naona wanaotoa huduma ni kama watu wamechoka vile. Yaani, baadhi wanaonekana kama wamelazimishwa - hawana motisha! Sijui malipo ndiyo madogo au ni tabia tu ya utendaji kazi.
Ukiuluza kitu unajibiwa kimkato sana na kama hujaelewa unaambiwa unapoteza muda kwa vile wengine ambao wako nyuma yako nao wanangojea huduma kama wewe. Na mara nyingi hao wanaosema hivyo huwa wana kauli ambayo ni 'arrogant'. Na hata hao wanaowasema 'wengine' kama watauliza wafafanuliwe kitu, utasikia kama ugomvi tena.
Kwa hiyo, utakuta kwamba kuliko kwenda kuuliza kitu unaamua kufanya jinsi unavyoona wewe na wakati mwingine unaweza kupatia au kukosea. Hivi hatuna njia ya kuboresha huduma katika Regional Centres zetu na hata pale Makao Makuu ya Chuo Kikuu Huria, Kinondoni?
Tuchangie namna ya kuboresha huduma Chuo Kikuu Huria ili kiweze kutoa huduma nzuri zaidi. Mimi naona huduma zake ni kama level ya sekondari - yaani, ukiwa maeneo yale hupati challenge ya kukufanya uone kama ni level ya chuo kikuu hasa kwenye Regional Centres na hata pale Makao Makuu. Je, niko 'prejudiced' au na nyinyi mnaona hivyo?
Kinachonisikitisha ni huduma duni na ukosefu wa ufanisi mzuri katika kutunza data na kuhakiki kazi za wanafunzi. Hii inakatisha tamaa sana! Halafu pia naona wanaotoa huduma ni kama watu wamechoka vile. Yaani, baadhi wanaonekana kama wamelazimishwa - hawana motisha! Sijui malipo ndiyo madogo au ni tabia tu ya utendaji kazi.
Ukiuluza kitu unajibiwa kimkato sana na kama hujaelewa unaambiwa unapoteza muda kwa vile wengine ambao wako nyuma yako nao wanangojea huduma kama wewe. Na mara nyingi hao wanaosema hivyo huwa wana kauli ambayo ni 'arrogant'. Na hata hao wanaowasema 'wengine' kama watauliza wafafanuliwe kitu, utasikia kama ugomvi tena.
Kwa hiyo, utakuta kwamba kuliko kwenda kuuliza kitu unaamua kufanya jinsi unavyoona wewe na wakati mwingine unaweza kupatia au kukosea. Hivi hatuna njia ya kuboresha huduma katika Regional Centres zetu na hata pale Makao Makuu ya Chuo Kikuu Huria, Kinondoni?
Tuchangie namna ya kuboresha huduma Chuo Kikuu Huria ili kiweze kutoa huduma nzuri zaidi. Mimi naona huduma zake ni kama level ya sekondari - yaani, ukiwa maeneo yale hupati challenge ya kukufanya uone kama ni level ya chuo kikuu hasa kwenye Regional Centres na hata pale Makao Makuu. Je, niko 'prejudiced' au na nyinyi mnaona hivyo?