KERO Chuo Kikuu Huria Tanzania lipeni Waajiriwa wenu pesa zao za kujikimu, mtawaua njaa na kuwafedhehesha mtaani

KERO Chuo Kikuu Huria Tanzania lipeni Waajiriwa wenu pesa zao za kujikimu, mtawaua njaa na kuwafedhehesha mtaani

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) ni moja kati ya Taasisi za Serikali ambayo hawajali kabisa suala la kulipa pesa za kujikimu kwa Wafanyakazi wao wanaposafiri.

Utakuta mtu anapangiwa kituo cha kazi Simiyu au Katavi na anapaswa kuripoti na ana familia, sio rahisi kuhama na kila kitu let say unatoka Arusha umepangiwa Katavi, hivyo mtu inabidi akaanze upya kwa sehemu kubwa.

Sasa mtu anatazamia hela za kujikimu ili angalau ajipange upya, sadly hizo pesa zinaweza kuchukua hadi mwaka ama zaidi.

Wakati huohuo, haturuhusiwi kukopa kwenye mfumo angalau kuweka mazingira sawa, mfumo unatuhitaji mpaka confirmation. Sasa hii inafanya wafanyakazi wenu wanakuwa watu wa kutembeza bakuli tu na madeni mengi, mnatufedhehesha, tulipeni pesa zetu.

HR Department kwakweli mnatuumiza sana, tuwekeeni pesa na sisi tujione Wafanyakazi kama nyie jamani, au mnataka kutuzima kama batch zingine mlivyowazima.

Pia soma:
~ Madai ya Chuo Kikuu Huria (OUT) kutolipa Watumishi stahiki zao, Chuo chatoa ufafanuzi
~
Uongozi wa Chuo Kikuu Huria wasema utaboresha mazingira ya Kampasi ya Singida
~ Chuo Kikuu Huria - Singida kiboreshe mazingira yake, ni kama vile kimetelekezwa
 
Umesema vizuri sana Ndugu yangu, nami nina mambo kadhaa ua kuongeza hapo:

nakuongezea mambo mengine, kwanza hakuna posho kwa staff wa kawaida, zaidi wanaopewa au niseme kupeana ni wachache wenye nafasi za juu.

Kuna wakubwa wachache wanapiga mpunga matokeo yake wafanyakazi wengine wakiwemo Wahadhiri wanaishia kulia njaa.

Mazingira kama hayo yanachangia Rushwa kuongezeka yanaathiri ubora wa elimu unaotolewa.

Mfano mpango wa OUT ni kufanya matangazo ili kupata Wanafunzi wengi, hilo limefanyika na Chuo chetu kimefanikiwa kuwa na Wanafunzi wengi lakini hata pesa inayoingia hatuioni, walao tupate hata incentive.

Mbaya zaidi imepelekea huduma mbovu na Wanafunzi wanaacha au kuhamia vyuo vingine.

Mara nyingi Wafanyakazi tunalazimika kuikopesha taasisi kwenye kazi mbalimbali.

Kuna mazoezi muhimu kama ya kurejelea mitaala ambayo yalipata fedha kutokana na mkopo wa Benki ya Dunia lakini bado Wafanyakazi wanaambiwa hakuna pesa.

Kuna baadhi ya kozi ambazo zinahitaji mafunzo kwa vitendo au wakati mwingine Wanafunzi wasome ana kwa ana pesa haipo lakini wanakuwa wamelipa ada.

Part Time Lecturers nao hawalipwi mpaka wengine wamesusa kufundisha, malipo ya watahini pia ni shida wakati Wanafunzi wanalipa ada.

Shida kubwa inakuja kwenye Uongozi wa Chuo, Viongozi wa juu wanateuliwa na wengi ni ambao wamestaafu, hawana malengo ya kuendeleza taasisi zaidi kujitengenezea safari ili watengeneze pesa.

Kama haya hayatasemwa hadharani na kufanyiwa kazi Chuo hiki kinaendelea kufa.
 
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) ni moja kati ya Taasisi za Serikali ambayo hawajali kabisa suala la kulipa pesa za kujikimu kwa Wafanyakazi wao wanaposafiri.

Utakuta mtu anapangiwa kituo cha kazi Simiyu au Katavi na anapaswa kuripoti na ana familia, sio rahisi kuhama na kila kitu let say unatoka Arusha umepangiwa Katavi, hivyo mtu inabidi akaanze upya kwa sehemu kubwa.

Sasa mtu anatazamia hela za kujikimu ili angalau ajipange upya, sadly hizo pesa zinaweza kuchukua hadi mwaka ama zaidi.

Wakati huohuo, haturuhusiwi kukopa kwenye mfumo angalau kuweka mazingira sawa, mfumo unatuhitaji mpaka confirmation. Sasa hii inafanya wafanyakazi wenu wanakuwa watu wa kutembeza bakuli tu na madeni mengi, mnatufedhehesha, tulipeni pesa zetu.

HR Department kwakweli mnatuumiza sana, tuwekeeni pesa na sisi tujione Wafanyakazi kama nyie jamani, au mnataka kutuzima kama batch zingine mlivyowazima.
Sekta ya elimu Tanzania haithaminiwi wala kuheshimiwa. Elimu Tanzania ni kitu cha Tia maji tia maji kianzia elimu ya awali hadi ya juu ndio maana watengeneza sera na mitaala ya elimu yetu, watoto wao hawasomeshwi nchini bali hupelekwa ughaibuni
 
Back
Top Bottom