Chura karudi majini, tutegemee mabadiliko au mkoromo usiomtisha tembo kunywa maji?

Chura karudi majini, tutegemee mabadiliko au mkoromo usiomtisha tembo kunywa maji?

shingta

Senior Member
Joined
Jan 27, 2014
Posts
101
Reaction score
17
Wanajamvi Mh. Samweli Sita karudi kwenye nyadhifa kama aliyokuwa nayo msimu wa kwanza wa serikali ya awamu ya nne, akiwa kama Spika wa bunge. Tofauti ipo kwani sasa ni Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba. Je, yeye kama chura (mzoeufu kwenye kiti cha kuongoza bunge aliyepewa tena nafasi hiyo) je ataweza kuzuia mapendekezo ya chama chake CCM yanayopingana na rasimu ya katiba, yani mkoromo wake kama chura utamzuia tembo kunywa maji (CCM)? au ni business as usual! Usanii ule ule tulionao kwa wanasiasa wa chama tawala? Napata wasi wasi kama mapendekezo ya wananchi yatazingatiwa au mapendekezo ya chama tawala ndo yatapewa kipaupendele. Manake rasimu haikubaliki na chama tawala, yaani mawazo ya wananchi sio ishu kwa chama tawala CCM. Kazi ipo.
 
Huyu Sita ni muumini wa serikali mbili. Hivyo kwa unafiki wake atatupilia mbali hoja ya serikali tatu na kuendeleza aina hii ya muungano wa kinyonyaji. Watanganyika maoni yetu ya kupata serikali yetu yameyeyuka chini ya huyu mnafiki! Natafuta nchi ya kwenda kujisajiri, bongo imeshindikana.
 
Back
Top Bottom