nyundo2017
JF-Expert Member
- Sep 7, 2017
- 1,439
- 861
Hongera CJ
Napenda kukushauri huu utaratibu wa "session" uufutilie mbali kwani unachelewesha haki za raia.
Unakuta majaji wapo na wanalipwa mishahara yao kila mwezi lakini kesi haziendi wakisubiri session na session zenyewe hazifanyiki hadi kuwe na pesa za posho za vikao vya majaji,mbona mahakimu wanaendesha kesi kila siku hawasubiri vikao?
Kero kubwa iko divisheni ya kazi mahakama kuu ambako majaji wengi wanaishi dar es salaam hadi vikao vifike na hela zipatikane ndiyo wanaomekana vituoni,je hii ni sawa?
Wafanyakazi wengi wanaachishwa kazi zao kwa hila hasa serikalini pasipo sababu za msingi au kufuata taratibu,anaenda CMA ambako ucheleweshaji wa kesi ni mkubwa sana pasipo sababu za msingi akitoka hapo ni rufaa kama kuna upande haujaridhika sasa huko ndiyo miaka kibao nenda rudi,nenda rudi kisa vikao havijaanza hamna hela za vikao vya majaji.
Je waliajiriwa kwa kutegemea posho zaidi?
Nawasilisha kwako.
Napenda kukushauri huu utaratibu wa "session" uufutilie mbali kwani unachelewesha haki za raia.
Unakuta majaji wapo na wanalipwa mishahara yao kila mwezi lakini kesi haziendi wakisubiri session na session zenyewe hazifanyiki hadi kuwe na pesa za posho za vikao vya majaji,mbona mahakimu wanaendesha kesi kila siku hawasubiri vikao?
Kero kubwa iko divisheni ya kazi mahakama kuu ambako majaji wengi wanaishi dar es salaam hadi vikao vifike na hela zipatikane ndiyo wanaomekana vituoni,je hii ni sawa?
Wafanyakazi wengi wanaachishwa kazi zao kwa hila hasa serikalini pasipo sababu za msingi au kufuata taratibu,anaenda CMA ambako ucheleweshaji wa kesi ni mkubwa sana pasipo sababu za msingi akitoka hapo ni rufaa kama kuna upande haujaridhika sasa huko ndiyo miaka kibao nenda rudi,nenda rudi kisa vikao havijaanza hamna hela za vikao vya majaji.
Je waliajiriwa kwa kutegemea posho zaidi?
Nawasilisha kwako.