Clatous Chama awa target ya kuchezewa rafu nyingi huko AFCON

Clatous Chama awa target ya kuchezewa rafu nyingi huko AFCON

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Sikupata wasaa wa kuangalia game ya marudiano ya Zambia vs Lesotho katika mashindano ya kutafuta kufuzu AFCON. Katika mechi hiyo Zambia walishinda 2-0.

Katika mechi hiyo, kiungo wa Simba, Clatous Chama aliingia kipindi cha pili dakika ya 80 na kucheza kwa takribani dakika 10+. Takwimu nilizopata zinaonyesha aligusa mpira karibia mara 20 akitoa pasi mbalimbali za maana kwa wenzake.

Leo nilipoangalia highlights za mechi hiyo, ilionyesha wakati Chama akiingia. Huwa si kawaida highlights za mchezo kuonyesha pale mabadiliko ya timu yanafanyika unless mchezaji anayeingia ni mchezaji mkubwa. Hilo ni jambo la kwanza nililochukua.

Baada ya hapo highlights hizo kwa bahati mbaya hazikuonyesha sana movements za Chama ila baada ya mchezaji mmoja wa Zambia kuchezewa rafu, mtangazaji alitoa comment moja akisema "toka Chama ameingia katika mechi hii amechezewa rafu nyingi" akiongezea kuwa "kila mchezaji anayekuja kucheza katika mechi hizi anaombea arudi salama katika club yake bila majeruhi".

Kwa hiyo nililochukua kutoka highlights ile ni kuwa uwezo wa Chama unajulikana vizuri Africa hii na Lesotho walijipanga kumzuia kwa njia zote asiweze kufurukuta.
 
Watu wanaotoka nbc si chochote kwenye timu zao za taifa,bado tuna safar,au makocha wamekariri wachezaj kutoka ulaya
Nadhani kuna kazi inabidi kufanyika kukuza branding ya ligi yetu kiujumla. Mafanikio ya timu binafsi za Simba na Yanga inaonyesha hayatoshi kuwapa namba. Inabidi wenzetu wakiwaita wachezaji wao wanaocheza huku, heshma fulani inabidi iambatane na ligi hii wanayochezea.
 
Huyu Mzee Chama wamchezee rafu za nini?

Ana nini cha kutisha wakati ni mchezaji wa kawaida sana.
 
Huyu Mzee Chama wamchezee rafu za nini?

Ana nini cha kutisha wakati ni mchezaji wa kawaida sana.
Hayo si maneno yangu, ni maneno ya mtangazaji wa mechi hiyo na nadhani hakuwa mtanzania.
 
Sikupata wasaa wa kuangalia game ya marudiano ya Zambia vs Lesotho katika mashindano ya kutafuta kufuzu AFCON. Katika mechi hiyo Zambia walishinda 2-0...
Chama kwa Zambia ni sawa na Kibu Taifa Stars. Watu waache kuwakamia wachezaji wa EPL waje kudili wa flop wa Berkene !

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Bro Zambia na Congo wana watu hawa unaowaona kwenye ligi yetu si chochote acha unafiki..
Ndiyo ujue bado tuna safari ndefu nilitegemea usikitishwe na hili sisi kwetu ni bora inamaana wachezaji wetu wa ndani viwango vyao ni vibovu.
 
Ilikuwaje mwamba wa lusaka kuanzia benchi?? Huyu kocha wa Zambia atakuwa shabiki wa timu ya "wananchi" lia lia!!
 
Ilikuwaje mwamba wa lusaka kuanzia benchi?? Huyu kocha wa Zambia atakuwa shabiki wa timu ya "wananchi" lia lia!!
Afadhali Chama kacheza dakika 10.Mayele na Musonda waliingia dakika za mwisho kabisa za 88 na 89 ambazo huwa zinatumika kimkakati kupoteza muda.
 
Lakini jana Mayele kaingia dk ya 59

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
Halafu akafanya nini?
Tulikuwa tunaongelea mechi za kwanza.Jana Bukambu alipigwa umeme. Congo ndio wanaburuza mkia kwenye kundi lao.Mnawakuza tu hawana wachezaji wa standard ya juu.Wamepitwa kwenye kundi lao hata na Mauritania.
 
Huyu Mzee Chama wamchezee rafu za nini?

Ana nini cha kutisha wakati ni mchezaji wa kawaida sana.
Kwa kasi waliyonayo Zambia na kwa spidi yake ya konokono ni halali aingie kipindi cha pili baada ya timu kuwa imeshashinda
 
Halafu akafanya nini?
Tulikuwa tunaongelea mechi za kwanza.Jana Bukambu alipigwa umeme. Congo ndio wanaburuza mkia kwenye kundi lao.Mnawakuza tu hawana wachezaji wa standard ya juu.Wamepitwa kwenye kundi lao hata na Mauritania.
Kufanya nini ni story nyingine afu hata huyo chama mechi ya kwanza hakucheza kabisa

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom