Clouds Media bado wana mapenzi na Diamond!!!

Chinga One

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2013
Posts
11,469
Reaction score
12,391
Sasa ndo naamini kwamba wafanyakazi wa clouds wana Mapenzi Diamond na bado wanafurahia kazi zake,na Wana Mmiss pia isipokuwa tu wanaogopa kibarua kuota nyasi kwa vile bosi wao ana chuki binafsi na WCB,tunawatukana na kuwalaumu bure pasipo kujua kuwa ndani ya CMG wapo team WCB damu damu ila tu ndo hivyo tena mambo ya kuajiriwa lazma ukubali kulala uchi......angalia hizi picha utamuona kibonde akiwa na kitenge na kwa nyuma mzee mzima Chibu D akiperform kwangwaru...sijui ilikuwa ni party ya nini...lakini kwenye video clip inaonyesha Kibonde akiserebuka na baadae akakimbia kukwepa camera...nadhani alijishtukia...Ingia kwenye instagram ya Kitenge Maulid kuona hizo clip.

My take: Hakuna jambo zuri kama uhuru wa nafsi,mwili na akili...vijana wenzangu tujitahidi kufanya kazi sana ili na sisi tuwe mabosi wa kazi zetu kuliko kuwa watumwa.....
 
Nakaa siti ya mbele mwenyewe....
 
Hiyo Ni nje ya kazi!
Kwani ulisikia wameambiwa wasiwasiliane na diamond hata nje ya ofisi?

Unajua chanzo cha mgogoro wao?

Ninachomkubali Ruge huwa haongei sana Ni vitendo tu!
Yaani kama vile umemkuta mwizi nyumbani kwako unaanza kumfukuza kimya kimya mpaka uhakikishe anaanza kupiga yowe yeye mwenyewe!

Na anawawezea kweli!
 
Lakini mpaka sasa hivi ameshafeli vijana wanapiga kazi kwa kwenda mbele...zama zimebadilika hizi.
 
Na sijui waligombania nini hawa si wayamalize tu. Ruge naye bwana bifu zake anaihusisha kampuni.
 
Kwa wcb kafeli,hadi top 20 yao imekuwa ya ajabu ajabu tu
 
Hapo kibonde alikuwa ni mc kwenye inshu hiyo ya cocacola
 
Lakini mpaka sasa hivi ameshafeli vijana wanapiga kazi kwa kwenda mbele...zama zimebadilika hizi.
Umeangalia kitu gani kikakuthibitisha amefeli?
Huku kuweweseka tu ni mafanikio tosha kwamba ruge amefanikiwa kwa kiasi chake!( angalia sio nyie mashabiki tu Hata wao kwenye Instagram page zao)

Juzi kati kwenye birthday yake alisema ishu iliyowahi kumsumbua akili Ni ile ya Vinega tu nayo anadhani kwasababu alikuwa mdogo"

[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Kwa wcb kafeli,hadi top 20 yao imekuwa ya ajabu ajabu tu
Hivi ni aspect zipi hizo mnazoziangalia mpaka mseme kafeli?
Yaani Kumbe top 20 inapendezeshwa na nyimbo za WCB tu?
Mbona east Africa huwezi zisikia hizo nyimbo zao Na mambo yanaenda kama kawaida?
 
Ruge ndiye aliyeufanya mziki wa bongo flavor ukae kibiashara, namaanisha yeye ndiye aliyetengeneza soko lake ndani na nje, na yeye ndiye alishika soko lao, East Afrika walichemka, kina majizzo walijikita kwenye burudani lakini Ruge peke yake ndo alijikita kwenye biashara, kabla ya Ruge kuupeleka mziki huo level za kimataifa aliurasimisha ukawa na haadhi hapa nchini, nani mkulu angekaa enzi hizo kusikiliza Julietha na nyambizi? Ulichukuliwa kihuni tu, alifanya juhudi kuua hipo hop kabisa ili wasanii wote waimbe wakiwa civilized! Na kupitia makundi yote ya ki hip hop gangsters yalikufa, hapo kabla ungesikia EastCost wana bifu na TMK wanaume japo wote walionekana machoko mbele ya Nako2Nako na Kikosi cha mizinga, huku unamkuta fid q na pale dudubaya, mabifu ya kuhuni kabisa, Ruge alipofanikiwa kuua hipo hipo akamgeuza na fid q kuwa muimba taarabu siku hizi, pima uwezo wa Ruge alipomwambia Mrisho Mpoto Mjomba, acha ufala tafuta hela, muziki wako uingize hela, tangu hapo mjomba anaimba nini? Zaidi ya kualikwa Ikulu ka mwanasiasa, kazi ya Ruge katika hiyo industry ni kubwa japo yapo ya hovyo pia alifanya, amewanyonya wasanini lakini ni yeye aliyewasaidia leo kila msanii analilia ngoma yake ichezwe clouds

Hata asipocheza ngoma yako ila anajua fitina zote za hiyo industry coz he blooded to build it, jiulize tangu diamond ametoswa na clouds kuna show gani ya maana amewahi kuifanya ya kumuingizia mkwanja? Kama alivyompandosha atamshusha tu, yaani diamond asahau kukanyaga Ikulu tena mark my words, hao wasanii wote ambao Ruge kawalea na kuwakuza anaouweza kuwa destroy kama alivyofanya kwa wengine kina Saida tena dada yake, na wengine kibao, THT wakati inaanza alikuwepo kina Vumilia na tangu alipotoka kujiunga na band hadi leo hasikiki!

Kwakifupi dogo diamond anakosea sana na management yake inamdanganya, alimzingua Bob junior na Kiba waliomsaidia hadi ruge na kina babu tale kumjua, anamzingua na Ruge aliyemsaidia kufika hapo alipo leo, clouds ilikuwa haipiti siku bila kusikia nyimbo ya diamonds sasa hivi ameota mapembe subiri tu promo atakayopewa kiba utashangaa.....!
 
Ila hawa mashabiki wa diamond kwa kweli naona kama wanaweweseka tangu juzi naona wanatoa nyuzi kuhusu clouds na ruge. Sasa kama clouds wameshindwa kwa diamond sioni haja had kupiga kelele.kupiga kelele huku maana yake CMG wana power na influence kubwa na maana yake dawa inaingia.
 
mbona maelezo marefu sana halafu hakuna hit point?
 
Onyesha sehemu ambayo amefanikiwa kuwapoteza WCB?
 
Kila utawala una zama zake brother, sasa kwa kuwa unawainua watu ndio uwapangie level za mafanikio yao, mtu akitaka step flani kwakuwa haikupendezi ndio awe adui!? I think WCB watafanya mapinduzi makubwa ya kuwafumbua wasanii na huu utumwa wa Ruge. Na hakuna mafanikio ya kweli chini ya utumwa ni lazma ujikomboe upambane ili kupata mafanikio. Diamond is a natural talented artist...na yupo level flani...naamini akiwa focused atakata hii minyororo...hata Puff Daddy alikata minyororo akafanikiwa......kisa mtu kuanzisha TV unamchukia wanataka auze tuu Karanga...and to the dismay ya watangazaji wa clouds media hawajijui nao wamo kifungoni....Millardayo.com anatakiwa ajitambue si kuendeshwaa ameshakua ila hajitambui....ruge he thinks same tactics alizotumia 90s on jidee will work in 2018...so stupid sana, sasa hv YouTube tuu ni zaidi ya Radio...acha Instagram....
 

Hahaha nimeangalia hii video nimecheka sana, Ruge amewageuza wafanyakazi wake misukule aisee hawana amani.
 
Yes, ni kweli mkuu! Ninachojaribu kusema sio kwamba Ruge anafanya poa, hapana ninachojaribu kusema ni kwamba ametengeneza soko ambalo ili msanii utoke lazima umlambe miguu, Ruge hapendi kudharauliwa kwa kazi aliyoifanya, na Ruge anapiga pesa kupitia wasanii aliowasaidia, tatizo ni hizo za dharau anazomuoneshea kwamba mimi pia ni mkubwa, Ruge katika industry ni Godfather wa diamond, so kama diamond ameingia kwenye industry aliyopo Ruge hapo kinachofata ni ushindani tu kibiashara na sio bifu, Sebastian Ndege mzee wa njia panda anamiliki band na radio, lakini hana bifu na Ruge,

Ugomvi wa Ruge na Diamond haupo pia, ugongomvi uliopo ni kati ya Ruge na Kusaga tu, Kusaga ndo mmiliki wa Wasafi tv na Radio, diamond karanga while Ruge yuko na chibu perfume na wasafi.com
Diamond ni mdogo hawezi na hatokaa aweze bifu na Ruge ningemshauri asijiingize huko kabisa, kama amejiona na yeye ni mkubwa anaweza tengeneza soko lake mwenyewe kama alivyofanya Majizzo na maisha yakaendelea
 
Pamoja na kwamba mimi ni shabiki wa Alikiba ila ukoloni wa clouds media siukubali hata kidogo. Siwalaumu sana wanayoyafanya ya kujaribu kuwabania baadhi ya wasanii la hasha ni uamuzi wao, kinachowafanya clouds media kubehave that way ni kwa sababu wameaminishwa kuwa hakuna media yenye nguvu kuliko clouds media na wameaminishwa kwamba kila msanii watakayembania atapotea kimuziki. Mpaka pale watakapothibitishiwa vinginevyo naamini watabadilika. Wakithibitishiwa kuwa wao si kitu na kwamba msanii anaweza kufanya vizuri bila mkono wao watabadilika sana na kubehave accordingly!
 
Sina ninachokijua hapa, nimejaribu kusoma michango ya wadau nielewe chochote, ila naona nyota tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…