Clouds wagoma kuleta msanii wa nje kwa hofu ya Bashite Dar.

Clouds wagoma kuleta msanii wa nje kwa hofu ya Bashite Dar.

instagram

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
2,118
Reaction score
4,863
Kuna za kunyapia kuwa clouds wali cancel booking ya msanii mkubwa wa kimataifa toka Marekani na wengine wakubwa kutoka Nigeria, Ghana, zimbabwe na South Africa, katika moja ya show ambayo ingeweka historia ya fiesta kufuatia show ya Castle lite, ila walihofia hali ya sintofahamu baada ya mkutano wa bashite na baraza la wahariri ambapo bashite alikataa kuomba radhi kwa clouds.

Clouds wanahofia bifu la kimya kimya kuweza kuwafilisi endapo watagharimia uwepo wa wasanii hao kwenye finali ya fiesta Dar alafu bashite akapiga marufuku tamasha hilo hatua za mwisho.

Tetesi ni kuwa clouds ingewagharimu pesa nyingi kumleta mkali wa nyimbo ya "i'm the one" toka marekani ambaye ni raia wa Canada endapo show ingeharibika ingepelekea kufilisika na kupelekea mgogoro mkubwa kati ya clouds na mfadhili wao mkubwa.
 
Acha hizo mkuu..TANGU MWAKA JANA RUGE alisema kwamba mwaka huu HAWANA PLAN ya kuleta msanii wa nje..ilikuwa ni baada ya ile bifu ya kiba na mondi kuibuka upya soon baada ya fiest iliyopita..na ilikuwa kwny kipindi cha XXL alihojiwa ndo akasema hivyo..ss ww naona unataka kuleta vitu visivyokuwepo.
 
ina make sense... huyu jamaa bashite yupo kwa maslahi yake. kwa sasa yeye ni mungu mtu. sema uzuri time ni kitu ambacho hakiongpii. kama zama za kina hitler zilipita hata zama za huyu kiazi zitapita pia
 
huyu bashite kila kitu yy,vijana fanyeni kazi achaneni na huu uzushi wa mitandaoni ,yaani kufeli kwao wenyewe clouds wamsingizie bashite.
 
Sijawahi waza kama BASHITE ana nguvu kiasi hiki.Bashite ana uwezo mkubwa mnooo aseeee.Akisema leo wanaume wote wa dar hakuna kupanda gari kwenda makazini tutembee tufanye mazoezi....nina imani kwa nguvu mnayosema anayo basi watu watatiii
 
Bashite,shokaga Kolomije...,tolihomkaya wamayo,wankiima,wababa na wasengi zogo lolo Bashite!
 
Yani nyie sasa mmeshakuwa kama matahira...kila jambo kafanya bashite...duuu..
Itafika kipindi mtashindwa kuwapa mimba wake zenu mtasema sababu ni Bashite..
Kumbe umekubali anaitwa hivo
 
Hawana ela ,wasilete Bla blaa
Fiesta ilikua serengeti sio Tigo
Toka mwaka jana ruge akihojiwa alisema fiesta ya mwaka huu hawataleta msanii wa nje maana mziki wetu umekuwa hauhutaji msanii toka nje ili tamasha kunoga.
Huyu kaamua tu andika hizi habari sidhani hata kama kazisikia kokote ila tu watu wanapenda kujifanya wana taarifa exclusive
 
Natamani sana ningekuwa Makonda, ningepiga Marufuku wanaume wa dar kulala na wake zao siku za weekend jumamosi na jumapili......
 
Back
Top Bottom