Clouds wanavyosota kumwangusha Hanstone

Unajua sababu yao ya kumtema mkuu
Nidhamu ya kazi hana, plus alivujisha nyimbo bila kufuata utaratibu. Alipoambiwa kuhusu hio ishu akapiga bunda!!

Na nirekebishe sehemu; Hawakumfukuza ni yeye aliesepa Hanscana Brand. Na kipindi anakula kona audio ya Chibonge ilikwisha toka ila video haikuwa tayari.. Abbah (mmiliki wa nyimbo) akamwomba Hans japo ampe ushirikiano washuti video akawa anapiga chenga na kwa ukubwa wa nyimbo kuitoa video bila msanii kuonekana na sauti zinapita haikuwa option ya Abbah ndio maana G nako sasa.
 
That's very true
 
Kumbe Ruge mlikuwa mnamsingizia tu hiyo ni POLICY yaan "Terms and conditions apply" ya CMG.
Kumbukeni ile ni mali binafsi sio redio au tv ya umma kwamba kila msanii ana haki ya kupigiwa wimbo wake. So vigezo na masharti kuzingatiwa, wabongo wagumu sana kuelewa.

Wale wapo kibiashara wanaangalia faida so mkishindwa kuelewana na mteja hakuna biashara

Ni sawa na hapa jf unaweza hata kupigwa life ban

Hili suala Ruge aliwahi kulifafanua vizuri sana
 
Tuache Kulialia sasa,Wasafi TV ipo tunalialia nini tena?
Tamasha Lipo Wasafi Festival hao clouds ni wakuwaacha tu wakutazama TV hiyo watazame Na kusikiliza Redio Na wasikilize halazimishwi MTU .Tupo kidijitali zaidi.Siyo Analogy.
 
Ila support za msanii mmoja mmoja ndizo zinazochangia wasanii kufa na stress, Madawa ya kulevya kuwa sehemu ya maisha yao, kudanga kwa wasanii wa kike pamoja na ushoga kwa baadhi ya wasanii wa kiume!! Naona bado hatujajifunza tunaendelea kulilia mtu mmoja abebwe!! Wacha niendelee kusikiliza mashairi yenye PHD kutoka kwa Disasta Vina!!
 
Kumbe Ruge mlikuwa mnamsingizia tu hiyo ni POLICY yaan "Terms and conditions apply" ya CMG.
kutokujielewa now CMG wanapoteza mvuto bado wanaule mtizamo wao Kuwa wanaweza kumpandisha&kumshusha msanii kimziki nakumbuka walijaribu... Kiba mara aslay... Nafikiri mbeleko zilitoboka now nyimbo zinazoongoza chat CLOUDS hazina views wakutosha pia hazi trend YouTube and very local songs
 
We jamaa Muongo sana na utachomwa moto mbaya sama..Nakushauri mtafute Abba process akupe stor kamili kuusu uyu dogo..clouds wana matatizo yao lakini kwa hili si ukwel unawaonea bure
 

sasa wamesotaje kumwangusha? mbona kajiangusha na hata wewe umeweka nyimbo 2'tu

Pili clouds ni private radio we mbululax waache na radio yao, sio TBC ile

huyu akomae na radio zingine nyingi zaidi ya 100

the fact unaiongelea Clouds unathibitisha ni redio pendwa, bora, na ina nguvu
 
Kama anajua why uje/ulalamike kuwa unafanyiwa fitna?? Hivi redio ni. Moja tu???

Mbona tuliwajua wasanii wa chiriku na mdundiko kilupitia efm??

Kama anajua tutamjua..kama hajui atakuwa kama yule kayumba was bss
 
Kwa wale ambao hatujui kusoma nyakati je, tuende tuition?
 
We jamaa Muongo sana na utachomwa moto mbaya sama..Nakushauri mtafute Abba process akupe stor kamili kuusu uyu dogo..clouds wana matatizo yao lakini kwa hili si ukwel unawaonea bure
Embu weka hapa ..huyo Abba process alisema nini kuhusu huyo dogo??
 
We Jamaa acha uongo ,mtafute ABBA akupe mkanda mzima Wa huyo dogo
 
We Jamaa acha uongo ,mtafute ABBA akupe mkanda mzima Wa huyo dogo
Huyo Abba kasemaje kwani??mnaposema tutamfute tumtafutaje kwa mfano?? Na je atakuwa willing kueleza huo mkanda kwa kila mtu?
 
Kwani lazima nyimbo zako zipigwe clouds
 
Kinachonishangaza ni mtu anasema Clouds hawana tena nguvu,ila at the same time anasema wanambania msanii fulani kutoboa..how is this possible??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…