SI KWELI Clyton Chipando (Babalevo) alisema wenye akili timamu CHADEMA hawafiki 10

SI KWELI Clyton Chipando (Babalevo) alisema wenye akili timamu CHADEMA hawafiki 10

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
JAMII CHECK_SIKWELI (2).jpg
 
Tunachokijua
Babalevo ni mwanamuziki wa Bongo Fleva, Mtangazaji wa Wasafi FM, Mchekeshaji na Balozi wa makampuni mbalimbali. Zaidi ya kuwa kwenye tasnia ya burudani Babalevo amewahi kuwa kiongozi wa kisiasa (Diwani) wa Kata ya Mwanga, Manispaa ya Kigoma Ujiji kupitia Chama Cha ACT Wazalendo

Babalevo kama mfanyakazi wa Redio ya Wasafi FM husikika akizungumza mambo mbalimbali ya kijamii, kiasa na kimichezo katika kipindi cha jioni kinachoitwa Jana na Leo kinachoanza saa 11:00 jioni mpaka saa 2:00 usiku.

Leo Desemba 4, 2024 katika Mtandao wa X (Zamani Twitter) imeibuka chapisho lenye nembo ya Wasafi Media (litazame hapa) likiwa limemnukuu Babalevo akisema kuwa "Watu wenye akili ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hawazidi kumi".

Upi uhalisia wa Post hiyo?
JamiiCheck imefuatilia chapisho hilo kupitia Google Reverse Image Search na kubaini chapisho hilo lililoibuka leo lilichapishwa mara ya kwanza kwenye Mtandao wa X (hapa) Septemba 24, 2024 na kusambaa zaidi Septemba 25 na 26, 2024 (tazama hapa na hapa). Sehemu zote Post hii inasambaa ikiwa picha tu na nukuu hiyo lakini hakuna Video ikimuonesha Babalevo akitamka maneno hayo kuhusu CHADEMA

Zaidi ya hayo, Ufuatiliaji wa Kimtandao uliofanywa na JamiiCheck umebaini kuwa post yenye maneno hayo na nembo ya Wasafi Media haikuwahi kuchapishwa katika kurasa zao rasmi za Mitandao ya kijamii na wala haikuwahi kuwekwa kwenye Akaunti rasmi za Babalevo.

Uchambuzi wa Posti husika
Uchambuzi wa JamiiCheck umebaini aina ya Mwandiko (font type) iliyotumika katika post hiyo iliyomnukuu Babalevo haifanani na font wanayoitimia Wasafi Media katika kuchapisha Taarifa zao nyingine.

Aidha, Uchunguzi wetu kupitia Akauni ya Babalevo umebaini kuwa Siku ya Septemba 21, 2024 msanii huyo alionekana akisafiri kuelekea Dubai (Tazama hapa) ambapo mpaka siku ya September 24 ambayo post hiyo inatoka Babalevo alikuwa bado Dubai na hakuwa Redioni (Tazama hapa).

Hivyo, kutokana na ufuatiliaji huu tumejiridhisha kuwa Taarifa hii imetengenezwa na haina uhusiano wowote na Babalevo na Wasafi Media.
Kwani Baba levo anajua maana ya akili iwapo yeye mwenyewe hana akili?
 
Back
Top Bottom