Coastal Union imevunja mkataba na Ley Matamp aliyekuwa golikipa bora wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/24

Coastal Union imevunja mkataba na Ley Matamp aliyekuwa golikipa bora wa Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2023/24

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Klabu ya Coastal Union imethibitisha kuvunja mkataba na aliyekuwa mlinda mlango wao, Ley Ngumbi Matamp ambaye alikuwa golikipa bora wa msimu wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania bara msimu uliopita kwa makubaliano ya pande zote mbili.
GT7BEpcXQAAx4NB.jpg
Taarifa ya leo Desemba 10, 2024 ya leo kupitia ukurasa rasmi wa klabu hiyo iliyoambatana na picha ya nyanda huyo raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imesema:- "Tunakutakia kheri nyingi na mafanikio zaidi katika maisha yako."

"Tumefikia makubaliano baina ya klabu yetu na golikipa wetu Ley Ngumbi Matamp ya kumaliza huduma za pande zote mbili. Uzoefu wako umechangia kwa asilimia kubwa mafanikio yetu ya msimu uliopita" imesema taarifa hiyo.
Screenshot 2024-12-10 112332.png
Matampi alijiunga na Coastal Union msimu uliopita 2023/2024 akiwa mchezaji huru baada ya kumalizana na FC Lupopo ya Congo, na msimu huo aliibuka kuwa kipa bora wa msimu.
 
Huyu itakuwa anakwenda Yanga
Sidhani kama anaenda Yanga mkuu, kuna tetesi za Ley kuwa alikuwa na shida ya kinidhamu kama unakumbuka hata wakati timu inaripoti kambini kwa ajili ya kujiandaa na pre season hakuwa na timu
 
Alikuwepo Dunia adonis,moshi ally,salimu waziri,Hamisi makena,Mohamedi mwameja,Duncan Mwamba na Riffat said wote waliondoka coastal ilibaki imara!
 
Alikuwepo Dunia adonis,moshi ally,salimu waziri,Hamisi makena,Mohamedi mwameja,Duncan Mwamba na Riffat said wote waliondoka coastal ilibaki imara!
DUNCAN MWAMBA alihamia kwetu Moro akakiwasha sana na RELI Morogoro pamoja na akina Magosso, Mbuyi Yondani, Butinini, Prof. Madundo Mtambo, Njohole Bonny, Mwanamtwa .... daaaah
 
DUNCAN MWAMBA alihamia kwetu Moro akakiwasha sana na RELI Morogoro pamoja na akina Magosso, Mbuyi Yondani, Butinini, Prof. Madundo Mtambo, Njohole Bonny, Mwanamtwa .... daaaah
Hakika kabisa!
 
  • Thanks
Reactions: K11
Umeona mechi yoyote kubwa wanadiriki kuweka kipa mwingine zaidi ya Diarra ambaye na mwenyewe siku hizi mashuti anayaangalia tu kwa macho?
Angekuwa anaangalia tu asingekuwa kipa namba moja wa Timu ya Taifa ya Mali.

Kama umewahi kucheza mpira huwezi kumlaumu kwa aina ile ya magoli.
 
Back
Top Bottom