mzaramo
JF-Expert Member
- Sep 4, 2006
- 6,371
- 5,186
Ni msanii gani amewahi kupata Connection kupitia Coke studio ?
Jaydee, Shaa, wote wamekuwemo mbona hatuoni hizo connection ?
N a kama lengo lingekuwa ni connection kwanini wasingekuwa wanakutanisha mameneja wao badala ya wasanii ?
Na kama huwa ni connection maprodyuza kama kina Nahreeh huwa wanaenda kufanya nini ?
Joh Makini alikutana Chidinma kule ikazaliwa perfect combo.
Flavour alikutana na Juliana ikazaliwa Nakupenda.
Sallam alipata ya kukutana na Neyo ikazaliwa I will marry u.
Diamond alikutana na Yemi Alade na ngoma ipo jikoni.
Yemi Alade alikutana na sauti Sol kenya na tumeiona.
na ukiambiwa connection aimaanishi mtoe nyimbo hiyo ni mifano tu kuna fursa nyingi nyuma yake na kujuana kwa wasanii kuna faida kubwa kibiashara na kama hujui managers huwa wanakwenda pia..Kama tulivyoona Sallam na Neyo walivyokutana.
Nahreal alisema baada ya kurudi toka Coke Studio kuwa kuwa pale kulimpa connection kibao na wasanii wakubwa na producers wengine walikuwepo pale.
Nasisitiza wanalipwa lakini sio kwa kiasi kikubwa kama tunavyotaka kuamini lengo hasa ni wasanii wajuaje na kupeana connection huku Coca Cola wakifanya matangazo yao ya kibiashara.
Asante.