Col MAKANIKA auwawa na jeshi la FARDC

Col MAKANIKA auwawa na jeshi la FARDC

MBOKA NA NGAI

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2025
Posts
350
Reaction score
576
1740068975331.png


Pichani, ni aliekuwa kiongozi wa kundi la wapiganaji TWIRWANEHO(TUJIRINDE), la wanyamulenge huko Kivu kusini.

Ameuwawa akiwa na wenzie wa 5,wanaosemekana kuwa walinzi wake, katika shambulio la drone, lililoandaliwa na jeshi la serikali ya Congo, FARDC.

M23, kwa sasa inaelekea katika maeneo ya TWIRWANEHO, na Kiongozi huyo, alikuwa ametangaza kuwa punde tu M23 itakapowasili maeneo yake, watajiunga na kuongeza nguvu.



Makanika alitoroka jeshi akiwa na cheo cha kanali, na kurudi huko alikozaliwa katika jimbo la FIZI, kuhakikisha anakusanya vijana wa Kinyamulenge waliokuwa wakiuliwa na kupolwa mali zao na jeshi la FARDC na washilika wake, ambao ni FDLR,wazalendo, na mwishoe jeshi la serikali ya Burundi, lililokuja kwa lengo la kukabiliana na waasi wa serikali hiyo, wajulikanao kama RED-TABARA.
 
Kazi kwelikweli,na huko DRC nasikia kuna kundi pia lipo miaka kibao linajifua kuja kuangusha serikali ya TZ ngoja tuone
Mi nakubali kabisa sisi CCM ni wazinguzi ila likija suala la ujinga wa kuivamia hii nchi. CCM haina Kona Kona huwa inakua straight like Putin
 
Sijui,maana ni story nilizozisikiaga zamani kidgo
Basi vyema kama stori za kusikia. Ili livamie, lazima lipite Rwanda, Burundi au Uganda. Hapo ujue, nchi yoyote inayoruhusu waasi wa jirani watumie ardhi yake, otomatikali inakuwa adui wa mlengwa. Jambo hilo si rahisi kwa sasa, sidhani kama kuna nchi iliyo tayari kupigana na Tanzania kwa sababu za kipuuzi. Kaama hata yenyewe haijawahi kumkwaza jirani yeyote
 
Basi vyema kama stori za kusikia. Ili livamie, lazima lipite Rwanda, Burundi au Uganda. Hapo ujue, nchi yoyote inayoruhusu waasi wa jirani watumie ardhi yake, otomatikali inakuwa adui wa mlengwa. Jambo hilo si rahisi kwa sasa, sidhani kama kuna nchi iliyo tayari kupigana na Tanzania kwa sababu za kipuuzi. Kaama hata yenyewe haijawahi kumkwaza jirani yeyote
Idd amini
 
Basi vyema kama stori za kusikia. Ili livamie, lazima lipite Rwanda, Burundi au Uganda. Hapo ujue, nchi yoyote inayoruhusu waasi wa jirani watumie ardhi yake, otomatikali inakuwa adui wa mlengwa. Jambo hilo si rahisi kwa sasa, sidhani kama kuna nchi iliyo tayari kupigana na Tanzania kwa sababu za kipuuzi. Kaama hata yenyewe haijawahi kumkwaza jirani yeyote
hv hujui Bokoharama anapiga nchi 4 kwawakati mmoja , akipiga huku anaingia huku , huez mvamia mtu kisa waharifu wamekimbilia kwake
 
Katika ukands huu WA Afrika Mashariki na Kati nchi pekee inayoweza kuisumbua TZ kijeshi haipo..Kwa kusini ni Zimbabwe, SA na Angola pekee ndizo zinazowezs kuisumbua TZ..
PK na Museveni pamoja na mbwembwe zote hawathubutu Kwa TZ..
 
Mtu pekee aliyewahi tikisa jeshi la TZ kutokea Tanzania ni Nyamhanga tu, na possibly kamwe haitokuja tokea tena.

Huyu mjeshi alipigana vita ya Kagera, akiwa huko akawa anatuma majeneza yaliyofungwa bunduki na ammunitions. Baada ya vita ya Kagera, alivyorudi Tarime, aka-recruit jeshi lake, akalipa mafunzo, then akatangaza uhuru wa nchi ya Chui, akashusha bendera ya Tanzania, akapandisha ngozi ya chui.

Walianza JWTZ wakapambana kwa siku 7, inasemekana Nyamhanga akajiua baada ya kubaini kushindwa. Then Nyerere akaleta jeshi toka Zanzibar, halikuwa na huruma na watu wa Tarime, wananchi wakachapika haswa kwenye msako wa bunduki za jeshi la chui, watu wakafanyiwa maovu yote ikiwemo kubakwa, kulazimishwa fanya mapenzi, etc....

Mwisho wa siku ikalazimu vijana wengi wa Tarime mkoa wa Mara waingizwe kwenye majeshi ya Tanzania miaka ya 80 na 90 ili uhaini usijirudie tena. Maana walijitoa sana vita ya Kagera. Then vita kuisha wakarudi Mara hawana hili wala lile.

Kwasasa sahau kuhusu mtanzania yoyote kupindua nchi. Mizizi ya hii nchi imeenda chini sana.
 
Back
Top Bottom