Commissioner General TRA na watu wako mnatutia aibu, mmekosa kazi hadi mnakagua risiti barabarani?

Watu

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2008
Posts
3,231
Reaction score
1,471
Siku ya leo hapa Dar es salaam kuna vitu vya ajabu sana vinafanyika kuna watu wa TRA/WAKALA wao wanakamata kila mzigo unapoita barabarani na kudai Risit ya mauzo!!! hadi imekuwa kero.....

Mzigo wa dukani nendani mkasimame dukani mone mwenye duka anatoa risiti?

Biashara zingine mauzo ni kwa PURCHASE ORDER??? invoicing is done after delivery and acceptance...waelewesheni watu wenu.......
 
Hawa siku hizi hawana tofauti na Mgambo wa City.
Wanafanya maisha kuwa magum.
Huku Zanzibar hawathubutu Ujinga huo.Watatusubiria hukohuko Maofisini.
Maana hata hivyo bado kuna duty conflict kati yao na ZRB(Zanzibar Revenue board)
 

mimi nadhani ni ubunifu mzuri ila ni wa kizamani. they cant think! kuna watu wengi hawana ajira mjini wanafanya misheni town watangazieni hilo dili

kuwa ukiwezesha kukamatwa kwa mfanyabiashara yeyote anayetakiwa kutoa risiti ya TRA akakuuzia bila kutoa risiti au akafanya mauzo bila kutoa risiti zawadi shilingi kadhaa. ambayo italipwa na mfanyabiashara huyohuyo aliyekamatwa.

tatizo ndani ya tra kuna watu hawataki mifumo hii mipya ya TRA kwa maana inawazibia mianya hata wao lakini kama kitaifa kutakuwa na mkakati nadhani mambo yataenda vizuri
 
Hiyo nayo kali... Kwa nini wasivizie madukani wadai hiyo EFD receipt kama mtu hana awapeleke dukani wakadeal na mwenye duka? Kwani dhamana ya kukusanya na kureport kodi tra kapewa muuzaji, mnunuzi au wote?


 
Nadhani wanakusanya kodi kwa walala hoi kwa sababu misaada hakuna tena
 
hizo kazi wanafanya wakala wao MAJEMBE ACTION MART
 
Jambo ambalo wanalifanya ni zuri pengine kuwe na maboresho kadha wa kadha. Si mfanyabiashara tu anawajibika kutoa
risiti lakini pia ni wajibu wa mnunuzi kuhakikisha anapewa hiyo risiti.Tuisaidie nchi yetu jamani.Hawa wafanyabiashara
wanatuuzia bidhaa ikiwa na VAT, inauma pale wasipopeleka hayo marejesho TRA.Wanajinufaisha kupitia hela zetu.Nchi inaibiwa sana na hawa wafanyabishara na wanasiasa, tusimame jamani.
 
Nadhani wanakusanya kodi kwa walala hoi kwa sababu misaada hakuna tena

Hapana mkuu, hao wafanyabishara wanaotuuzia bidhaa Kariakoo si walala hoi hata kidogo. Kumbuka wengi wao ni wahindi na Waswahili wachache, wana mitaji mikubwa, kwa nini wanakwepa kodi? Usipowadai kodi wanadanganya takwimu za mauzo yao.Tushirikiane kuwabana jamani, tunaibiwa s
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…