'Competence' ya Bunge letu inanitia mashaka kwa kweli

'Competence' ya Bunge letu inanitia mashaka kwa kweli

Agrey998

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2019
Posts
417
Reaction score
550
Imekua kawaida kwa Bunge kupitisha miswada mbalimbali inayohusu maslahi ya walio wengi haswa wa kipato cha chini lakini miswaada hio imekua michungu mithilii ya siki katika Maisha ya wananchi wa Hali ya chini na umekua Kama utamaduni baada ya miswaada hio kupitishwa Raid anakuja kutengua miswaada hio Kwa kuifuta au kupunguza makali.

mwaka 2019 tuliona swala juu ya kikokotoo cha Pensheni za wastaafu, Jambo lililalamikiwa na wengi maana liligusa wastaafu wengi ambao Pensheni zao ndo zilikua mkombozi wao uzeeni lakini baada ya muda Rais akaja akaondoa kikokotoo.

Mwaka 2021 Bunge letu lilipitisha Sheria ya tozo za simu , wahanga wakuu katika swala hili lilikua wafanyabiashara wadogo wa huduma za kifedha na watu wa kipato cha chini ambao hutegemea miamala ya fedha kuendesha Maisha Yao , kilio kilikua kikubwa mpaka ikaundwa tume juu ya swala hili , wanasema tozo zimepunguzwa lakini bado makali ya Sheria hii yanatafuna biashara za wengi hasa masikini na hata CEO aliepita wa Vodacom alitamka wazi athari za Sheria hii kwenye MPesa.

Tozo za mafuta kupunguzwa

Bunge lilipitisha kupandisha tozo ya mafuta na kusababisha bei kupanda maradufu ilikua inashangaza kwamba Zambia wanategemea Bandari zetu kuleta mafuta katika nchi Yao lakini bei ya mafuta kwao ilikua ndogo kuliko apa , ilikua inashangaza Mtu kutoka Tunduma kwenda Zambia kununua mafuta Nadhan hata Zambia walikua wanatushangaa.

Kwa matajiri wala hutasikia wakilalamikia Sheria hizi maana wao wanapata economies of scale katika biashara zao Kwa kuwa wanafanya kwa wingi kwaio hata wakija wakicalculate Amount of Tax/levy per unit gharama unakuja ndogo tofauti na maskini anaezalisha unit chache na hata akipiga amount of levy per unit unakuja kubwa na kufanya gharama iwe kubwa zaidi na kumfanya auze Kwa gharama kubwa na alifanya Ivo ndo mwanzo wa wateja kukimbia na kwenda Kwa Tajiri anaezalisha Kwa gharama ndogo na kupelekea kuua biashara ya mtu masikini

Je, nini kifanyike

Nadhan Bunge letu lingejitahidi kuunda Sheria ambazo zinawezesha zaidi wafanyabiashara wadogo na watu wa Hali ya chini ili kupunguza income inequality Kwa Taifa maana Sheria zetu kwa kiasi kikubwa zina athari ndogo Sana Kwa matajiri.

Kufanya upembuzi yakinifu juu ya Sheria wanazoweka na madhara yake na manufaa yake. Hapa Nadhan kuna kamati za Bunge ambazo zina wataalamu ambao wangeweza kufanya utafiti mdogo juu ya Sheria hizo na kutoa majibu sahihi maana kazi zinazoenda kufanya na tume zinazoundwa baada ya tatzo kutokea zingefanywa na kamati za Bunge na kutoa majibu sahihi ambayo yangepunguza hata taharuki Kwa wananchi na pia hata wananchi wangekua na Imani juu ya watu waliowateua kuwawakilisha .

Nawasilisha Hoja . Kuwa mzalendo, ipende Nchi yako
 
Pamoja na ushabiki wa kupitisha vitu bila kuwaza, lawama zinaenda kwa Rais na baraza la mawaziri.

Miswada yote kabla ya kuja bungeni hupitiwa na baraza la mawaziri na kamati za kisekta kabla ya bunge. Kama kote huko hawaoni hayo mapungufu, itakuwaje bunge la wanao jua kusoma na kuandika waone? Nani kwa mfano huko bungeni ataoma?
 
Nashangaa hata dada yetu halima mdee na ubunge wake wa uhaini hata hafungui mdomo,Na wale wabunge wawili wa CUF na Chadema plus ACT wa ZNZ wote kimyaaaaaa.

Ila haya yote aliyataka Nape kuzuia bunge live wakati akiwa waziri wa habari
 
Inasikitisha.

Bunge la "ndiyooooo..." na kugonga meza kwa kila jambo hawawezi kufanya unavyosema. Wale ni 'rubber stamp'.

Mi5 tena!
 
WaTanzania hadi sasa yaano tokea uchaguzi uibiwe au tuseme utekwe nyara na matokeo ya kura kupangwa, nchi inaenda bila ya bunge, wale waliopo wote wanalipa fadhila za bwana na hawawezi kusema kwinn'yooo, hawana uthubutu huo maana wamewekwa au wamechomekwa kama plug, anytime wakileta ujuba wanachomolewa na kuwekwa mwingine, saa watu dizaini hizo unategemea niini?
 
Nashangaa hata dada yetu halima mdee na ubunge wake wa uhaini hata hafungui mdomo,Na wale wabunge wawili wa CUF na Chadema plus ACT wa ZNZ wote kimyaaaaaa.

Ila haya yote aliyataka Nape kuzuia bunge live wakati akiwa waziri wa habari
Nape aliagizwa na mwendazake, na asingeweza fanya lolote, lijamaa lilikuwa linaagizi wachini wanatekeleza hata kama wenyewe hawakupenda!
 
Hilo najua lakini kwenye kamati za wabunge Nadhan zingewekwa wataalamu mbali mbali bila kujali ni wabunge au si wabunge
Kwa hili panahitajika mabadiliko katika katiba na wala siyo mabadiliko katika sheria peke yake!

Katiba mpya ni muhimu!
 
Unategemea Nini kwa uongozi wa Spika ambae hata kwenye Jimbo lake watoto wanasomea shule za mbavu za mbwa licha ya kuwa mbunge na spika kwa zaidi ya miaka 20, Barabara yenye lami Ni chini ya kilometers 10 Jimbo zima.

Unategemea Nini kwa bunge ambalo wabunge wake wote Ni iyena iyena?
 
Wabunge wote ni wa CCM, na wote wanamuheshimu mwenyekiti wao ambaye ndiye Rais wa nchi kuzidi Mungu. Haiwezekani na haitatokea wabunge wapinge muswada wa sheria yo yote ambayo itapelekwa na serikali kwa kuamini kuwa mwenyekiti wao ameridhia. Kwa wao wabunge huo utakuwa utovu wa nidhamu na usaliti!
 
Unategemea Nini kwa uongozi wa Spika ambae hata kwenye Jimbo lake watoto wanasomea shule za mbavu za mbwa licha ya kuwa mbunge na spika kwa zaidi ya miaka 20, Barabara yenye lami Ni chini ya kilometers 10 Jimbo zima.

Unategemea Nini kwa bunge ambalo wabunge wake wote Ni iyena iyena?
Anawapa pombe za kienyeji
 
Wabunge wote ni wa CCM, na na wote wanamuheshimu mwenyekiti wao ambaye ndiye Rais wa nchi kuzidi Mungu. Haiwezekani na haitatokea wabunge wapinge muswada wa sheria yo yote ambayo itapelekwa na serikali kwa kuamini kuwa mwenyekiti wao ameridhia. Kwa wao wabunge huo utakuwa utovu wa nidhamu na usaliti!
Hatari sn na aibu
 
Ukiwangalia wanavyokaa na kuzunguka zunguka na viti mle ndani ya Bunge unaweza fikiri ni watu wa maana, kumbe ni negative sifuri kabisa. Uwezo wa kufikiri umeathiriwa na uchama, kazi yao kubwa waliotumwa ni kuitetea serikali na kupongezana kama mateja wa dawa za kulevya, na Kusema ndioooo(hata kama umeshtuka kutoka kwenye kusinzia na hujui nini kilikuwa kinajadiliwa) na kugonga meza kama ngoma za wachawi waliofeli/kuzidiwa nguvu za kichawi.
 
Unapoteza muda na nguvu nyingi kusubiria embe chini ya mnazi! Hao wabunge wengi wao walikataliwa na wajumbe wa chama chao cha CCM ila M/kiti akasema nipeni hao. Wakakataliwa kwenye sanduku la kura ila Mfalme akaiagiza Tume ya uchaguzi - nipeni hao. What do you expect?
 
Nape aliagizwa na mwendazake, na asingeweza fanya lolote, lijamaa lilikuwa linaagizi wachini wanatekeleza hata kama wenyewe hawakupenda!
Acheni kusingizia,KWA hyo bao la mkono ni yeye alimtuma pia?

Hapo ndo mnaonekana mna matatzo kichwani,Mtu aliyekua katibu mwenezi na kushambulia wapinzani ndo unayesema katumwa?


Nape anafunga bunge ni mikakati ya ccm Kabla baada ya wabunge wao kutaka hata JF ifungiwe.

J.makamba alivyokua naibu waziri wa mawasiliano alileta na alipitisha cyber crime act Kabla ya huyo mwendazake,Vp effect zake?


Rudisheni akili zenu sawa
 
Back
Top Bottom