Brother James
JF-Expert Member
- Feb 21, 2012
- 233
- 172
Nilikuwa napita pita katika TCU website hususani katika kitabu cha sifa za kudahiliwa katika fani fulani na kuangalia sifa za vyuo mbali mbali za kuingilia katika fani mbali mbali. Nimekutana na sifa za kuingilia fani za za BSc. Computer Science na BSc. Computer Engineering lakini nilichokiona nikaona nisinyamaze kwa sababu nilishindwa kuelewa nikaona niilete hii mada hapa labda wana JF mnaweza kunisaidia kwani yawezekana kuna vitu vya msingi vinavyoangaliwa hadi kufikia kila chuo kuwa na sifa mbali mbali za kuingilia katika fani zinazofanana.
1. Nilipita karibia kila chuo kinachodahili fani tajwa na kuona tofauti kubwa tu kwenye sifa za kuingilia katika hizo fani japo cut-points zao zinafanana zinaanzia 2.0 hadi 3.5. Mfano UDSM wanataka waliofaulu katika PGM, PCM na equivalents za Diploma in Computer Science/IT, UDOM wanataka watu waliofaulu katika EGM, PGM, PCM na equivalent za Dip. in IT/Comp. Science, ST Joseph wanataka waliofaulu (BSc. Comp. Science) katika EGM, PGM, ECA, HGE na Equivalents, St. Joseph (BSc. Comp. Engineering) wanataka waliofaulu ktk PCM na Equivalent tu, Ruaha University wanahitaji waliofaulu katika PCM, EGM, PCB, CBG na equivalents za Comp. science/IT, n.k; Swali langu je nini tafsiri ya hizi tofauti za kuingilia ktk the same programme kwa wanafunzi wanaosoma mtaala wa aina moja??
2. Wengi wa wanachuo wanaodahiliwa katika katika fani hizi kupitia equivalents za Diploma in IT/Comp. Science ni wale waliosoma katika fani za sanaa (Arts Combinations)baada ya kusoma courses za diploma katika vyuo kama UCC, DIT,IFM etc. ndio wanao onekana wapo vizuri zaidi wakidahiliwa ktk fani za computer ukilinganisha na wale direct from schools tena waliosoma PCM ,EGM, PGM, PCB na CBG's, Je Vyuo vyetu havioni kwamba ni wakati muafaka wa kutoa fursa sawa za kudahiliwa kwa wanafunzi waliosoma hata fani za Arts ili mradi tu wawatengee mwaka mmoja wa pre-University katika fani husika?? nimeshuhudia kupitia vyuo vingi tu, hawa (PCM, PGM, PCB, EGM n.k) wetu wakipata shida za kufaulu kwenye hizi fani sambamba kabisa na wale waliosoma arts (Tembelea UCC, St. Joseph, UDOM, IAA, DIT, IFM n.k utawakuta). Hata hivyo pamoja na ugeni wa fani hizi ktk mitaala ya kitanzania (no foundation at all) hususani ktk shule za msingi na masekondari lakini compter courses si ngumu.
3. Ndugu wadau, Je unadhani kuna haja ya kutenganisha sifa za kuingilia katika BSc. Computer Science na BSc. Computer Engineering?? FUNGUKA KAMA UNA MAWAZO MAZURI KWA AJILI YA KUNISAIDIA NA PIA KUVISAIDIA VYUO VYETU NA JAMII NZIMA YA KITANZANIA
####KATIKA KUJENGA POINTS ZAKO UNAWEZA KULINGANISHA FANI NYINGINEZO UNAZOZIFAHAMU ILI KUONA KAMA KUNA HAJA YA KUFANYA MABADILIKO PIA KTK HIZO FANI&SIFA ZA KUINGILIA####
NAOMBA KUWASILISHA
1. Nilipita karibia kila chuo kinachodahili fani tajwa na kuona tofauti kubwa tu kwenye sifa za kuingilia katika hizo fani japo cut-points zao zinafanana zinaanzia 2.0 hadi 3.5. Mfano UDSM wanataka waliofaulu katika PGM, PCM na equivalents za Diploma in Computer Science/IT, UDOM wanataka watu waliofaulu katika EGM, PGM, PCM na equivalent za Dip. in IT/Comp. Science, ST Joseph wanataka waliofaulu (BSc. Comp. Science) katika EGM, PGM, ECA, HGE na Equivalents, St. Joseph (BSc. Comp. Engineering) wanataka waliofaulu ktk PCM na Equivalent tu, Ruaha University wanahitaji waliofaulu katika PCM, EGM, PCB, CBG na equivalents za Comp. science/IT, n.k; Swali langu je nini tafsiri ya hizi tofauti za kuingilia ktk the same programme kwa wanafunzi wanaosoma mtaala wa aina moja??
2. Wengi wa wanachuo wanaodahiliwa katika katika fani hizi kupitia equivalents za Diploma in IT/Comp. Science ni wale waliosoma katika fani za sanaa (Arts Combinations)baada ya kusoma courses za diploma katika vyuo kama UCC, DIT,IFM etc. ndio wanao onekana wapo vizuri zaidi wakidahiliwa ktk fani za computer ukilinganisha na wale direct from schools tena waliosoma PCM ,EGM, PGM, PCB na CBG's, Je Vyuo vyetu havioni kwamba ni wakati muafaka wa kutoa fursa sawa za kudahiliwa kwa wanafunzi waliosoma hata fani za Arts ili mradi tu wawatengee mwaka mmoja wa pre-University katika fani husika?? nimeshuhudia kupitia vyuo vingi tu, hawa (PCM, PGM, PCB, EGM n.k) wetu wakipata shida za kufaulu kwenye hizi fani sambamba kabisa na wale waliosoma arts (Tembelea UCC, St. Joseph, UDOM, IAA, DIT, IFM n.k utawakuta). Hata hivyo pamoja na ugeni wa fani hizi ktk mitaala ya kitanzania (no foundation at all) hususani ktk shule za msingi na masekondari lakini compter courses si ngumu.
3. Ndugu wadau, Je unadhani kuna haja ya kutenganisha sifa za kuingilia katika BSc. Computer Science na BSc. Computer Engineering?? FUNGUKA KAMA UNA MAWAZO MAZURI KWA AJILI YA KUNISAIDIA NA PIA KUVISAIDIA VYUO VYETU NA JAMII NZIMA YA KITANZANIA
####KATIKA KUJENGA POINTS ZAKO UNAWEZA KULINGANISHA FANI NYINGINEZO UNAZOZIFAHAMU ILI KUONA KAMA KUNA HAJA YA KUFANYA MABADILIKO PIA KTK HIZO FANI&SIFA ZA KUINGILIA####
NAOMBA KUWASILISHA