Congo DRC yavunja uhusiano na Rwanda kufuatia mzunguko wa Goma unofanywa na waasi wa M23

Congo DRC yavunja uhusiano na Rwanda kufuatia mzunguko wa Goma unofanywa na waasi wa M23

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
Leo hii serikali ya Congo DRC imetangaza kuvunja mahusiano na Rwanda huku wanajeshi wapatao 13 wa kutoka vikosi vya kulinda amani na wanajeshi wengine wa kigeni kuuawa.

Wizara ya mambo ya nje ya Congo DRC imetangaza leo kuwa inawaondoa watumishi wote walioko katika ofisi ya ubalozi wa Congo DRC mjini Kinshasa. Serikali ya Rwanda bado kujibu hata hii inoashiria mambo kutokuwa mazuri baina ya nchi hizi majirani.

Ofisi hiyo itafungwa ndani ya masaa 48 yajayo na wafanyakazi wote wameamriwa kurudi Kinshasa.

Leo hii pia baraza La Usalama la Umoja wa Mataifa litaketi kuzungumzia hali inoendelea nchini Congo DRC kufuatia ombi la serikali ya Congo DRC.

Hadi sasa vikosi vya waasi wa M23 vikiwa ni sehemu ya vikosi vya waasi vipatavyo 100 vimeshachukua kilomita zipatazo 27 za mji wa Sake. Jana serikali ya Congo ilisema vikosi vya nchi za SADC vya SAMIDRC viliweza kuwarudisha nyuma waasi hao lakini tayari wanajeshi wawili wa Afrika Kusini, mmoja wa Uruguay na wengine wa kigeni wameishauawa.

Akizungumza na AP kwa masharti ya kutotajwa jina afisa mmoja wa UN amesema kuwa pia kuna wanajeshi wengine watatu walouawa kutoka Malawi na Afrika Kusini pekee hadi sasa imepiteza wanajeshi 7.

Majeshi ya kulinda amani ya MONUSCO yapo nchini Congo DRC tangia mwaka 2005 na iadadi yao ilikuwa ni askari 14,000. Tangu mwaka 2021 majeshi ya Congo DRC na yale ya nchi SADC yamekuwa yakikabiliana na vikosi vya M23 kuvizuia kuchukua mji wa Goma.

Mji huo wa kistratejia una madini lukuki waasi hao wa M23 ambao ni wa kabila la Watutsi wamekuwa wakidai kuwa Goma ni jimbo lao. Rwanda pia imekuwa ikituhumiwa kuvisaidia vikosi hivyo kwa silaha, mitambo ya makombora na vingine.

Madini yaliyoko katika maeneo ya mji huo ni pamoja na Dhahabu, Almasi, cassiterite, coltan, tourmaline, pyrochlore, na Wolfram.

Rwanda imekana kuvisaidia vikosi hivyo lakini imekiri kuwepo kwa vikosi vya majeshi ya Rwanda upande wa mashariki ambako ndiko kunopakana na mji wa Goma na pia kuwepo kwa mitambo ya makombora huku ikidai kuwa mitambo hiyo ipo kuimarisha ulinzi na pia kuangalia vikosi vya Congo DRC ili kuvizuia kuingia Rwanda.

Pia habari za kijasusi ambazo bado hazijathibitishwa zadai kuwa vikosi vya majeshi ya Rwanda vimeingia mpakani na Congo DRC kusaidia vikosi vya waasi kuchukua mazima mji wa Goma ambao ni makao makuu ya jimbo la Kivu ya kaskazini.

Kwa kifupi ni kuwa tayari vita kamili ikaingia hatua ingine nchini Rwanda khasa kufuatia kitendo kilofanywa na majeshi ya Rwanda hadi kufikia asubuhi ya leo.

Baadhi ya vyanzo vya habari hii:

Actualite

AP
 
Mataifa ya maziwa makuu yanatakiwa kuandaa mkakati wa kumuondoa madarakani huyu dikteta Kagame bila ya hivyo amani haitakuwepo mashariki ya Congo.
Kagame anatoa somo la maslahi mapana,yaani jamaa ana mentality kama ya US ,hata kwa kuiba as long nchi yale ifaidike. Hi mentality tukiwa nayo tu kwa resources tulizo kuwa nazo ndani TZ hii nchi itapaa kimaendeleo tatizo ubinafsi, ufisadi na rushwa.
 
Kagame anaionea sana Congo. Mbona haigusi Tanzania

Atume wanajeshi wake waje waibe madini Geita.

Tumnyooshe
 
Leo hii serikali ya Congo DRC imetanganza kuvunja mahusiano na Rwanda huku wanajeshi wapatao 13 wa kutoka vikosi vya kulinda amani na wanajeshi wengine wa kigeni kuuawa.

Wizara ya mambo ya nje ya Congo DRC imetangaza leo kuwa inawaondoa watumishi wote walioko katika ofisi ya ubalozi wa Congo DRC mjini Kinshasa. Serikali ya Rwanda bado kujibu hata hii inoashiria mambo kutokuwa mazuri baina ya nchi hizi majirani.

Ofisi hiyo itafungwa ndani ya masaa 48 yajayo na wafanyakazi wote wameamriwa kurudi Kinshasa.

Leo hii pia baraza La Usalama la Umoja wa Mataifa litaketi kuzungumzia hali inoendelea nchini Congo DRC kufuatia ombi la serikali ya Congo DRC.

Hadi sasa vikosi vya waasi wa M23 vikiwa i sehemu ya vikosi vya waasi vipatavyo 100 vimeshacukua kilomita zipatazo 27 za mji wa Sake. Jana serikali ya Congo ilisema vikosi vya nchi za SADC vya SAMIDRC viliweza kuwarudisha nyuma waasi hao lakini tayari wanajeshi wawili wa Afrika Kusini, mmoja wa Uruguay na wengine wa kigeni wameishauawa.

Akizungumza na AP kwa masharti ya kutotajwa jina afisa mmoja wa UN amesema kuwa pia kuna wanajeshi wengine watatu walouawa kutoka Malawi na Afrika Kusini pekee hadi sasa imepiteza wanajeshi 7.

Majeshi ya kulinda amani ya MONUSCO yapo nchini Congo DRC tangia mwaka 2005 na iadadi yao ilikuwa ni askari 14,000. Tangu mwaka 2021 majeshi ya Congo DRC na yale ya nchi SADC yamekuwa yakikabiliana na vikosi vya M23 kuvizuia kuchukua mji wa Goma.

Mji huo wa kistratejia una madini lukuki waasi hao wa M23 ambao ni wa kabila la Watutsi wamekuwa wakidai kuwa Goma ni jimbo lao. Rwanda pia imekuwa ikituhumiwa kuvisaidia vikosi hivyo kwa silaha, mitambo ya makombora na vingine.

Madini yaliyoko katika maeneo ya mji huo ni pamoja na Dhahabu, Almasi, cassiterite, coltan, tourmaline, pyrochlore, na Wolfram.

Rwanda imekana kuvisaidia vikosi hivyo lakini imekiri kuwepo kwa vikosi vya majeshi ya Rwanda upande wa mashariki ambako ndiko kunopakana na mji wa Goma na pia kuwepo kwa mitambo ya makombora huku ikidai kuwa mitambo hiyo ipo kuimarisha ulinzi na pia kuangalia vikosi vya Congo DRC ili kuvizuia kuingia Rwanda.

Pia habari za kijasusi ambazo bado hazijathibitishwa zadai kuwa vikosi vya majeshi ya Rwanda vimeingia mpakani na Congo DRC kusaidia vikosi vya waasi kuchukua mazima mji wa Goma ambao ni makao makuu ya jimbo la Kivu ya kaskazini.

Kwa kifupi ni kuwa tayari vita kamili ikaingia hatua ingine nchini Rwanda khasa kufuatia kitendo kilofanywa na majeshi ya Rwanda haid kufikia asubuhi ya leo.

Baadhi ya vyanzo vya habari hii:

Actualite

AP
Mataifa ya maziwa makuu yanatakiwa kuandaa mkakati wa kumuondoa madarakani huyu dikteta Kagame bila ya hivyo amani haitakuwepo mashariki ya Congo.
A short sighted mind argument.

Je, umeshatafiti kwa kina ili kujua kiini hasa Cha mapigano hayo yanayoendelea huko Goma?

Kwa taarifa yako:
Raia wengi sana wa Ukraine watakuwa wapo tayari kukubali kuivunja nchi yao ili wajiunge na kuwa sehemu ya nchi ya Marekani na kuwa Jimbo la 51 la nchi hiyo ya Marekani kuliko kukubali kuwa raia wa nchi ya Urusi ambayo ni majirani zao wanaopakana nao mpaka mmoja. Watu wa Ukraine kamwe hawapo tayari kabisa kuwa Raia wa nchi ya Urusi.
Do you know Why?
 
Kagame anaionea sana Congo. Mbona haigusi Tanzania

Atume wanajeshi wake waje waibe madini Geita.

Tumnyooshe
Wizi ulouzoea unafanywa na vibaka. Wezi professional hupelekewa mzigo kwao. Geita afuate nini? Huenda hayo ya Geita anapelekewa nchini kwake. Kwa hiyo hana haja ya kuja huko
 
Wizi ulouzoea unafanywa na vibaka. Wezi professional hupelekewa mzigo kwao. Geita afuate nini? Huenda hayo ya Geita anapelekewa nchini kwake. Kwa hiyo hana haja ya kuja huko

Mbona congo anapeleka majeshi yake? Hasubiri kupelekewa.

Tunataka Alete jeshi la watutsi Tanzania lije kubeba madini kama anavyofanya congo
 
Kagame anaionea sana Congo. Mbona haigusi Tanzania

Atume wanajeshi wake waje waibe madini Geita.

Tumnyooshe
Wanyarundi watakua watumwa wetu japo utumwa ulipigwa marufuku ,ila watakua wanalima miwa Kagera ,mtu wa na Kwa ujiran wa ugali dagaa,sehem ya kulala kwenye halls ,na kuoga ,saa 11 sharp waamshwe waanze mazoez na kunywa uji saa 12 asbh shamban mpka saa 10 ndo wale msosi
 
Back
Top Bottom