mkuu Asante sana kwa kuanzisha Uzi huu.
Mimi pia ni Mteja wa kampuni hii natumia kingamuzi chao.
Hata mimi nilipokea sms yao hiyo siku ya ijumaa, wametuambia kuna Station 2 wameongeza lakini cha Ajabu hazipo kwenye Menu.
Pili Mechi za Afcon walituambia tutaziona kupitia station ya ZBC2 ni kweli jana walionyesha ila ikakatika gafla mpaka sasa zimeota Mbawa siyo ZBC ZBC2 zote hazipo.
Swali je! Inamaana uongozi na usimamizi wa Vingamuzi hivi hawajui kwamba station hizo hazipo?
Hawa jamaa wamekuwa wazembe sana kwenye kutoa huduma.
Unaweza ukalipia huduma wanachukua muda mrefu kufungua.
Wakati mwingine wanakata huduma na wakati bado una muda wa hewani ni kero tupu.
Nadhani hawakuwekana sawa na jamaa wa ZBC2 kwenye malipo ya kurusha mechi hizo ndiyo maana wamekata huduma. Sijui kama kule Azam Tv ZBC2 ipo hewani!
yaelekea kuna hujuma juu ya jambo hili, maana hata Azam Tv wanatumia station hiyo iyo ya ZBC2 kuonyesha Mechi hizo.We we sisi was Azam tunacheki mechi live
Edit title tafadhali - Ardhi ?Walidai tutaona AFCOM kupitia ZBC2. Jana wameonyesha mechi ya ufunguzi kwa muda wakatoweka hewani mpaka sasa.
Biashara hizi zinahitaji kukidhi mahitaji ya wateja na kutoa taarifa sahihi. Binafsi mmeniboa sana kwa ahadi hii ya uongo.
Ujumbe wao huu hapa
"Ahsante sana mteja wetu wa king'amuzi cha Continental kwa kuwa nasi mwaka wote 2016. Ili kuonyesha shukrani zetu kwako, tumeongeza channel ya ATN na TV1, vilevile usikose kuangalia mashindano ya AFCON kupitia ZBC2"
sasa unatumia kingámuzi cha continental kwa nini hilo ni kosa lakoWalidai tutaona AFCOM kupitia ZBC2. Jana wameonyesha mechi ya ufunguzi kwa muda wakatoweka hewani mpaka sasa.
Biashara hizi zinahitaji kukidhi mahitaji ya wateja na kutoa taarifa sahihi. Binafsi mmeniboa sana kwa ahadi hii ya uongo.
Ujumbe wao huu hapa
"Ahsante sana mteja wetu wa king'amuzi cha Continental kwa kuwa nasi mwaka wote 2016. Ili kuonyesha shukrani zetu kwako, tumeongeza channel ya ATN na TV1, vilevile usikose kuangalia mashindano ya AFCON kupitia ZBC2"