Corneille Nangaa; Mkuu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Congo(CENI) aliyegeuka mkuu wa waasi

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Huyu mkuu wa kundi la waasi linaloitwa Congo River Alliance wakiwemo M23 wanaotaka kumng'oa Rais Tshisekedi ndiy aliyekuwa mkuu wa tume ya uchaguzi iliyomuingiza Tshisekedi madarakani mwaka 2018 katika uchaguzi wenye utata unaodaiwa Martin Fayulu ndio alishinda ila Kabila na Tshisekedi wakacheza dili na tume ya uchaguzi kupora ushindi.

Nangaa na Tshisekedi walikuja kukorofishana baadaye baada ya Nangaa kuanza kumpiga Tshisekedi na kutaka kugombea urais mwaka 2023 hadi akapewa kesi ya uhaini ndipo akakimbilia Nairobi Kenya pamoja na kiongozi wa M23 kuunganisha makundi ya waasi kwa mwamvuli wa CRA.


Hapa akiwa kalamba suti enzi hizo anakula maisha serikalini



Hapa baada ya kuvua suti na kuvaa gwanda!
 
Kwenye MAISHA ya siasa akuna adui w milele na akuna Rafiki w milele.
KAZI ni kipimo cha UTU
 
Wacongo wamejaa ujinga ubaya ni kuwa lawama zote anatwishwa PK.
 
Daah!! Huu Mwamba umeazimia kwenda all the way to Kinshasa kilomita 1700kms away.
 
Huyu naye anapigania demokrasia?
 
Huyu naye anapigania demokrasia?
Congo inahitaji kwanza angalau order kabla hata ya kuwazia democracy, Tshisekedi ameshindwa kuhakikisha nchi ina order.
 
Congo inahitaji kwanza angalau order kabla hata ya kuwazia democracy, Tshisekedi ameshindwa kuhakikisha nchi ina order.
Kwa hiyo Nangaa ndiye mbadala wa Tshekedi kwa sasa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…