Prof Koboko
JF-Expert Member
- Aug 15, 2020
- 350
- 2,550
Tuanze na wewe,he wewe unayo corona?Tuwe wakweli tusije kuficha maradhi alafu kifo kikatuumbua.
Serikali ya Tanzania na hasa kiongozi wetu mkuu amerudia mara nyingi kuwa hatuna ugonjwa wa Covid-19 na wote tumeshuhudia ya kuwa kambi na wodi zilizokuwa zimetengwa zilifungwa tangu mwaka jana.Hili ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu.
Jambo moja ambalo binafsi sikubaliani nalo ni hili la kuweka matumaini makubwa katika dua na maombi na kuanza kulegeza taratibu zingine za kujikinga. Duniani wanaoathirika na Covid wengine ni wacha Mungu kuliko hata sisi na hatuna ubora wa kiimani kuliko wao.
Naamini ya kuwa mafanikio makubwa tuliyopata mwaka jana pamoja na hizo dua na maombi ni kuanza kuchukua hatua mapema kuhamasisha watu kwa kupitia njia mbalimbali.
Ugonjwa upo South Africa, Malawi, Kenya na Uganda achilia mbali Burundi na Rwanda na kwa mantiki hiyo ni suala la muda tu.
Serikali iendelee kutangaza kuwa hakuna Covid-19 lakini irudishe uhamasishaji wa kujikinga. Barakoa katika public places (hasa daladala) iwe lazima, vifaa vya kunawia mikono sehemu za biashara virudishwe, shule zote taratibu za awali ziwekewe mkazo.
Kwa kuwa ugoNjwa umeonyesha kuwa na athari kubwa kwa watu walio na magonjwa mengine (co morbidity kama kisukari, Pressure na HIV), kliniki za magonja haya ziwekewe utaratibu mzuri.
TANZANIA KORONA HAKUNA ILA KWA JIRANI IPO!
Serikali ya Tanzania na hasa kiongozi wetu mkuu amerudia mara nyingi kuwa hatuna ugonjwa wa Covid-19 na wote tumeshuhudia ya kuwa kambi na wodi zilizokuwa zimetengwa zilifungwa tangu mwaka jana.Hili ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu.
Jambo moja ambalo binafsi sikubaliani nalo ni hili la kuweka matumaini makubwa katika dua na maombi na kuanza kulegeza taratibu zingine za kujikinga. Duniani wanaoathirika na Covid wengine ni wacha Mungu kuliko hata sisi na hatuna ubora wa kiimani kuliko wao.
Naamini ya kuwa mafanikio makubwa tuliyopata mwaka jana pamoja na hizo dua na maombi ni kuanza kuchukua hatua mapema kuhamasisha watu kwa kupitia njia mbalimbali.
Ugonjwa upo South Africa, Malawi, Kenya na Uganda achilia mbali Burundi na Rwanda na kwa mantiki hiyo ni suala la muda tu.
Serikali iendelee kutangaza kuwa hakuna Covid-19 lakini irudishe uhamasishaji wa kujikinga. Barakoa katika public places (hasa daladala) iwe lazima, vifaa vya kunawia mikono sehemu za biashara virudishwe, shule zote taratibu za awali ziwekewe mkazo.
Kwa kuwa ugoNjwa umeonyesha kuwa na athari kubwa kwa watu walio na magonjwa mengine (co morbidity kama kisukari, Pressure na HIV), kliniki za magonja haya ziwekewe utaratibu mzuri.
TANZANIA KORONA HAKUNA ILA KWA JIRANI IPO!
Brother nitakupinga hapo sweden. Herd immunity haijawasaidia chochote. Walikuwa na maambukizi 535000 na vifo 10,323.Mkuu, juzi hapa Malawi imetoa amri ya kufunga shule, mwezi mmoja au mwili iliyo pita Malawi ilipoteza mawaziri wawili kwa mpigo, walipishana kwa siku tu!
Wiki iliyopita niliona BBC documetary ikizungumzia kwamba Kenya imegundurika ina a new strain ya corona ambayo haipo popote Duniani hisipo kuwa Kenya tu na kibaya zaidi wanasema ugonjwa huo umegundurika huko TAVETA yaani mpakani mwa Kenya na Tanzania, nikawa najiuliza maswali mengi hivi hawa Wakenya wanazungumzia ugunduzi wa new strain ya corona mpakani mwa Tanzania na Kenya wana lengo gani? Kwa nini taasisi ya utafiti ya chanjo kutoka Uingereza (Oxford University) ikishirikiana na taasisi ya utafiti ya Kenya (KEMRON) wanakuja na horror stories kutoka mpakani mwa nchi zetu mbili.
Binafsi nashauri ingekuwa vizuri kama Serikali yetu inge hoji kwa kina taasisi hizo mbili zinazo jihusisha na tafiti pamoja na majaribio ya chanjo ya Oxford ili ijulikane statements zao zilikuwa zina maanisha nini au zina ajenda ya siri.
Tukija hapa kwetu so far so good i.e hali ya hivi sasa aona ni shwari kabisa, cha muhimu ni kila mmoja wetu achukue tahadhali - wataalamu wetu wa Wizara ya afya labda wanachukuwa approach ya kisayansi inayo julikana kama "herd immunity theory" kama wenzetu wa Sweden - mbinu hiyo imefanya maambukizi ya corona yapunguwe sana sana huko Sweden unlike Continental Europe na USA wanao lazimisha lockdown - my opinion.
Swali la kipuuzi
Herd immunity? Unajua Swedeni wameshakufa wangapi? Na walificha juu ya maambukizi? Hoja yangu sio kuwa na lockdown bali tuambiwe ukweli kama kuna maambukizi tuchukue hatua.
Kuhusu huo utafiti juu ya chanjo,siwezi fahamu una nia gani? Na wala sijasema tufanye tafiti juu ya chanjo.