Corona ina faida

Corona ina faida

Joined
Mar 30, 2020
Posts
4
Reaction score
0
KORONA INA FAIDA
20200329_195432_0001.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Korona imetupa msamiati mpya "korona"
imekuza lugha
 
Korona haiteui, tajiri na maskini
Dunia haichagui, iuwe iache nani
Waafrika hijui, wachina wamarekani
Korona ina hasara, na zake faida pia

Ingawa inagutusha, kwa kuuwa wengi watu
Katika haya maisha, inazo faida kwetu
Mwanzo imetufundisha, kunawa mikono yetu
Korona ina hasara, na zake faida pia

Mitaroni na vilabu , walevi wametitia
Wamepunguza sharabu, hatuwaoni kwa ndia
Wote wamejiratibu,kwa nyumba kajifungia
Korona ina hasara, na zake faida pia.

Ubovu umesimama , vita sijavisikia
Kumekuwa na heshima,silaha zimetulia
Tumeanza kuisoma,Korani na Bibilia
Korona ina hasara, na faida zake pia.


Ile mipango ya kando, kitambo ulosikia
Biashara za magendo, usiku ukiingia
Vyote vimewekwa kando, na watu kujirudia
Korona ina hasara, na faida zake pia
images%20(2).jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom