Tetesi: Corona inapukutisha watu Dar. Kuna wanaolalamika ndugu zao kuzikwa kinguvu na Mamlaka Dar huko Bahari Beach, Buza na Mbweni

Ninamashaka kama hii idadi ya wagonjwa inayotajwa sasa haina uhusiano wowote na tamko la WB la kukopesha nchi zilizoathirika zaidi na corona.
Kauli ile ya Ummy mwalimu ya kwamba "tumeamua kusema ukweli" na kisha kutaja idadi kubwa ya wenye virusi vya corona,nilhisi tu kuna kitu hapa si kwamba et wameamua kusema ukweli tofauti na wengi walivyodhani.
 
Tembeleeni usiku wa manane sehemu zilizotajwa kama Buza makaburini mkajionee
Bahari beach eneo la kondo Buza na Mbweni acheni kusifia mapambio ya mwami wa kihutu anaetupeleka kuzimu
Tuwekeeni hata picha au video clip basi tuone hayo makaburi
 
Mtaani kwangu na ninapofanyia kazi hakuna case yoyote ya maambukizi wala vifo. Maelezo kama hayo bila kuweka takwimu tunahesabu kama uzushi, uzandiki na uongo!!
 
I believe huo ndio uhalisia. Tuchukue tahadhari. Ila si vema kutiana hofu sababu naamini tuko kwenye peak na tutavuka salama.
Hatuko kwenye peak tusijidanganye maambukizi ndio kwanza yanasambaa kuelekea Inland
 
Sasa jemadari wa majeshi kajifisha chato unategemea sisi tufanyeje? Chamhimu kila mtu ajilinde kwa namna yake. Kaa ndani toka nje kwa kuvizia
 
I believe huo ndio uhalisia. Tuchukue tahadhari. Ila si vema kutiana hofu sababu naamini tuko kwenye peak na tutavuka salama.
Sawa! Ila unaposema tupo kwenye peak, ni hatua gani kubwa zilizochukuliwa kuepusha maambukizi zaidi katika jamii?
 
Tunawaomba ndugu wa Marehemu waje watie uzito kwenye uzi huu ili kuwepo na uhalali
 
Muafrika bwana kuzikwa kwa umati na kuzikwa bila umati ni swala analoweza kuletea ugomvi! Sasa kama kuna coronavirus what's the problem mamlaka ikifanya inachofanya? peleke ujinga aisee! Au unataka kila mazishi yaende na maambukizi?
 

Wewe umeshuhudia misiba mingapi kwa macho yako, hao wanaofiwa wote ni maskini hawawezi hata kutoa taarifa humu JF wewe ndo uwatolee? Wewe umefiwa na ndugu au watu wa karibu wangapi, je kalba ya corona watu hapo dar walikuwa hawafi? Je wakati huu wa corona unataka mjikusanye kwenye misiba wakati unajua kuna zuio la mikusanyiko, toa taarifavzavuhakika na sio watu wanasema huo ndo unaitwa uongo, nakushauri jitenge kaa ndani kulinda afya yako,
 
Nasasa Wagonjwa wengi wanatoroka na kwenda kujifukiza ili kuunga mkono ushauri wa mkemia wa Mayalla
Kwa hizi kejeli na uzushi wenu natamani JF ifungiwe kwa muda kwani imewapa kijiwe cha kukashfu na kuzusha kila mtakalo. Ilimradi mnaitukana,kuikashfu serekali basi humu nisehemu salama sana kwenu kuliko ufipa st.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hizi kejeli na uzushi wenu natamani JF ifungiwe kwa muda kwani imewapa kijiwe cha kukashfu na kuzusha kila mtakalo. Ilimradi mnaitukana,kuikashfu serekali basi humu nisehemu salama sana kwenu kuliko ufipa st.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mheshimiwa jana kasema hii mitandao IGP should deal with them!
 
Acha kututisha
wewe. mi huku najivukizia πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…