Corona Virus Nchini Tanzania

Corona Virus Nchini Tanzania

Ng'wanamalundi

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2008
Posts
1,203
Reaction score
1,422
Habarini za jioni wanajamvi.

Mimi siishi Dar Muda mfupi uliopita niliona ujumbe kwenye WhatsApp ya ndugu mmoja ikionyesha magari yakipita Kariakoo yakifukizia dawa ya kuua corona, sawasawa na yale yaliyokuwa yakionekana kwenye miji ya Uchina.

Hii ni hatua kubwa na nzuri sana iliyochukuliwa na Serikali kukabili janga hili. Baada ya kuona 'clip' hiyo nilikimbilia hapa JF nikifikiria nitapata habari zaidi hapa kwa kuwa nyuzi huanzishwa hapa hata juu ya tetesi tu ya kitu tarajiwa na watu hufurika kuchangia nyuzi hizo. Nimestuka kwamba hakuna chochote humu JF juu ya habari hii!

Je, hii ni kwa sababu suala lenyewe si muhimu? Au ni kwa sababu ni hatua nzuri iliyochukuliwa na Serikali na wachangiaji wengi wa humu JF wamejikita kwenye mada za kulaumu Serikali tu? Kwa kuwa hili ni jambo zuri lisilolaumika, labda ndiyo maana wachangiaji hao wameona wakae kimya tu?

Kwenye 'clip' hiyo niliwasikia wakazi wa hapo Kariakoo na viongozi wa Machinga wakisifia hatua hiyo na mmoja wa wachangiaji akagusia kwamba hatua hiyo iliagizwa na Mkuu wa Mkoa.

Labda ndiyo hilo limeleta nongwa kwa kuwa hakuna mtu anayekuwa tayari kumpongeza Makonda au Serikali ya JPM kwa ujumla. Watu wamejikita katika kumlaumu Makonda tu na Serikali ya JPM.

Naomba mjuaji anielimishe kuhusu hili.
 
Kama ni habari za makonda au baba yake tupilia mbali kabisaaa... Hatutaki maujinga ujinga sisi.
 
Hayo ni kufanya mambo bila hata kujua kama yatakuwa na faida au la. Pia ni kuiga tu wenzetu. Kwa ufupi kuna watu wanataka kunawa kisiasa na wapo tayari kumwaga mabilioni ya walipa kodi ili mradi sifa wapate.

Upukiziaji wa dawa (space spraying) hauna maana kabisa wakati wagonjwa wakiwa wachache sana (14), unafaa pale mnapokuwa na wagojwa wengi eg 1000.

Walichopaswa kufanya mapema ni kufunga viwanja vya ndege, wangefanya mapema tusingekuwa na wagonjwa hata mmoja hadi sasa. Hakuna sifa kwa makonda ila lawama kwake.
 
Una akili ndogo! Yaani kwenye nchi hii yenye mikoa zaidi ya 25 gari moja peke yake ipulize dawa kariakoo kisha unakuja kuleta uzi kwa mihemko?!

Tatizo hujamuelewa mtoa mada, yeye anamuongelea Makonda na uwajibikaji ndani ya mkoa wake. Hii ni creativity ya Makonda kwa nafasi aliyokuwa nayo, wewe unaongelea general scenario, sasa nini maana ya mgawanyo wa madaraka?
 
Mimi mwenyewe niliiona nikaja huku nikakutana na uzi wako, kila siku kuna jambo jipya hutokea na kuna mtu huja kupata taarifa zaidi Jamiiforums na akikuta halipo hufungua uzi, labda ni mara ya kwanza hali hiyo kujitokeza kwako.
 
Back
Top Bottom