chrome
JF-Expert Member
- Oct 10, 2011
- 401
- 426
Sekta ya afya nchini Kenya inakabiliwa na msukusuko kutokana na mfululizo wa migomo ya wahudumu wa afya katikati ya janga la virusi vya corona.
Muungano wa wahudumu wa maabara nchini Kenya umetoa muda wa hadi Januari 4 mwaka unaokuja kwa serikali kushughulikia madai yao au wajiunge na wauguzi na maafisa wa kliniki walio kwenye mgomo kwa muda wa siku 25 hivi sasa.
Kupitia muungano wao, KNUMLO, wahudumu hao wameisuta serikali wakisema imepuuza kitengo hicho muhimu huku juhudi zao, kushirikisha mazungumzo na asasi za serikali zikigonga mwamba kama anavyoelezea katibu mkuu Chrispine Momanyi.
"Endapo siku saba kuanzia sasa, taifa lote, iwe hata ni sekta ya binafsi, shirika la umma kama CDC, tunashirikiana kusitisha huduma zozote kwa hii serikali na wananchi kwa sababu hatuchukuliwi kuwa watu muhimu."
Kiasi wahudumu wa maabara 267 wameambukizwa virusi vya Corona
Muungano wa wahudumu wa maabara nchini Kenya umetoa muda wa hadi Januari 4 mwaka unaokuja kwa serikali kushughulikia madai yao au wajiunge na wauguzi na maafisa wa kliniki walio kwenye mgomo kwa muda wa siku 25 hivi sasa.
Kupitia muungano wao, KNUMLO, wahudumu hao wameisuta serikali wakisema imepuuza kitengo hicho muhimu huku juhudi zao, kushirikisha mazungumzo na asasi za serikali zikigonga mwamba kama anavyoelezea katibu mkuu Chrispine Momanyi.
"Endapo siku saba kuanzia sasa, taifa lote, iwe hata ni sekta ya binafsi, shirika la umma kama CDC, tunashirikiana kusitisha huduma zozote kwa hii serikali na wananchi kwa sababu hatuchukuliwi kuwa watu muhimu."
Kiasi wahudumu wa maabara 267 wameambukizwa virusi vya Corona