Mabibi na mabwana moja kwa moja kwenye mada.
Ajabu na kweli pana watu wanakereka mno waonapo tunaandika kuasa na kukumbusha ili kwamba maisha ya watu yakiwamo na yao, yaweze kulindwa. Watu hawa waliobarikiwa mioyo ya ajabu na pia kuwa na midomo michafu iliyojaa matusi katu si wa kuwasabiria matakwa yao. Kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kuwafumbia macho mumiani ili wayafanye yao kwa nafasi.
Burundi ni nchi ambayo kuhusiana na Corona misimamo yake haijawa tofauti sana na yetu. Shughuli zao zote zimekuwa zikiendelea kana kwamba Corona ni ka upepo tu ambako katapita. Hawakuacha kunawa nawa mikono kwa maji tiririka na sabuni au kwa sanitizers, wala kuendekeza safari ambazo hazikuwa za lazima.
Burundi, uchaguzi wao mkuu uliendelea kana kwamba hakukuwa na janga la ugonjwa. Michezo iliendelea kama kawaida, Ibada, masoko, nk na bila shaka hata mashule hayakutatizika.
Wenzetu walipo tayari wameshaonja joto ya jiwe. Mengine tunayoambiana kuhusiana na strokes nk, hizo zinabakia kuwa ni mbwembwe tu, ambazo aghalabu hapa kwetu hizo tunajua kuzicheza zaidi.
Ndani ya siku tatu Rais wa Burundi ni marehemu (RIP), mama yake naye anasemekana kuwa tayari ni marehemu (RIP), mkewe anatibiwa Corona na pia dada yake anatibiwa Corona. Walinzi wote 3 waliompeleka bi Denise Nkurunziza hospitali nao wanatibiwa Corona.
Kwa ujumla serikali nzima ya Burundi itakuwa kwa sasa hivi iko njia panda. Kwani hata president elect General Evarisite Ndayishimiye na hata Spika ambaye angechukua hatamu kwa sasa wanasemekana kuugulia Covid.
Chonde chonde ndugu zetu tusifikie huko. Wala tusijidanganye kuwa haya ni ya Burundi tu. Huu ugonjwa hauna mwenyewe.
Nafasi yetu ya kuishi kama mtu mmoja mmoja inasalia kuwa pale kila mmoja wetu atakapotambua umuhimu wa maisha ya mwenziwe.
Katika imani za TANU na CCM: "binadamu wote ni ndugu zangu." Mwisho wa kunukuu.
Haya yasibakie kwenye makaratasi peke yake.
Ajabu na kweli pana watu wanakereka mno waonapo tunaandika kuasa na kukumbusha ili kwamba maisha ya watu yakiwamo na yao, yaweze kulindwa. Watu hawa waliobarikiwa mioyo ya ajabu na pia kuwa na midomo michafu iliyojaa matusi katu si wa kuwasabiria matakwa yao. Kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kuwafumbia macho mumiani ili wayafanye yao kwa nafasi.
Burundi ni nchi ambayo kuhusiana na Corona misimamo yake haijawa tofauti sana na yetu. Shughuli zao zote zimekuwa zikiendelea kana kwamba Corona ni ka upepo tu ambako katapita. Hawakuacha kunawa nawa mikono kwa maji tiririka na sabuni au kwa sanitizers, wala kuendekeza safari ambazo hazikuwa za lazima.
Burundi, uchaguzi wao mkuu uliendelea kana kwamba hakukuwa na janga la ugonjwa. Michezo iliendelea kama kawaida, Ibada, masoko, nk na bila shaka hata mashule hayakutatizika.
Wenzetu walipo tayari wameshaonja joto ya jiwe. Mengine tunayoambiana kuhusiana na strokes nk, hizo zinabakia kuwa ni mbwembwe tu, ambazo aghalabu hapa kwetu hizo tunajua kuzicheza zaidi.
Ndani ya siku tatu Rais wa Burundi ni marehemu (RIP), mama yake naye anasemekana kuwa tayari ni marehemu (RIP), mkewe anatibiwa Corona na pia dada yake anatibiwa Corona. Walinzi wote 3 waliompeleka bi Denise Nkurunziza hospitali nao wanatibiwa Corona.
Kwa ujumla serikali nzima ya Burundi itakuwa kwa sasa hivi iko njia panda. Kwani hata president elect General Evarisite Ndayishimiye na hata Spika ambaye angechukua hatamu kwa sasa wanasemekana kuugulia Covid.
Chonde chonde ndugu zetu tusifikie huko. Wala tusijidanganye kuwa haya ni ya Burundi tu. Huu ugonjwa hauna mwenyewe.
Nafasi yetu ya kuishi kama mtu mmoja mmoja inasalia kuwa pale kila mmoja wetu atakapotambua umuhimu wa maisha ya mwenziwe.
Katika imani za TANU na CCM: "binadamu wote ni ndugu zangu." Mwisho wa kunukuu.
Haya yasibakie kwenye makaratasi peke yake.