Shida pale Tabora ajira zimetawaliw na mazingira ya Rushwa. 250-300 ndio dau lao. japo kuna mabadiliko yamefanywa lakini still pesa mbele kama tai. kama kuna mtu anataka kubisha kuhusu hili, Simple, fika tu eneo la tukio. inahuzunisha sababu yaliyoandikwa ktk mtandao wao na yanayoendelea pale ni vitu viwili tofauti, pale watu wenye ujuzi wanaachwa.
kuna hili pia liangaliwe.
*mnaulizwa mwenye degree/diploma? mpo wangapi? mnanyoosha vidole, unajua nini kinakuja kutokea? mnaenda kufeli katika mtihani wa Saikolojia( Afya ya akili )
ukipata bahati ndio unapata dokezo pale Elimu andika darasa la saba ama kidato cha nne, ukileta mbwembwe za mavyeti, hufiki hata katika Taste.
hilo mosi.
kuna aina nyingine ya Usumbufu umeshamaliza Taste unaambiwa Mtapigiwa simu ( Mazingira mengine haya) wapo wanaopigiwa na wapo ambao hawajapigiwa mpaka sasa wapo huko wanazengea zengea tu.
kama wahusika wapo humu, jirekebisheni upande huo, watu wanasononeka na mnawatia watu ktk maisha magumu zaidi, pia kama wapo watu wa TAKUKURU waliangalie hili kwa ukaribu zaidi, wengi wamesha ripoti haya na wengine wapo nje pale yaani watu wapo tayari pale kutoa ushirikiano sababu washachoka.