JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 685
- 1,124
Hadi sasa hakuna utafiti uliopata hitimisho kuhusu mama mjamzito kumwambukiza mtoto aliye tumboni endapo ameathirika na #COVID19
Kwa mujibu wa WHO, kuna tafiti mbalimbali zinazoashiria kuwa hakuna uwezekano wa maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto aliye tumboni. Pia wameeleza kuwa #CoronaVirus havikukutwa kwenye maji ya uzazi “amniotic fluid” wala maziwa
Wakati inaelezwa kuwa wajawazito wasio na matatizo mengine hawako katika hatari ya kuambukizwa #COVID19 kuliko watu wengine, wanashauriwa kuchukua tahadhari kubwa
Vilevile, si lazima mjamzito ambaye anaonesha dalili za #COVID19 kujifungua kwa njia ya upasuaji bali njia ya uzazi itategemea na mapendeleo yake na ushauri wa mtaalamu
Mama aliyeathirika anaruhusiwa kumnyonyesha mwanae huku akizingatia taratibu za kuzuia maambukizi ikiwemo kuvaa barakoa muda wote awapo na mtoto na kunawa mikono kabla ya kumshika
Source: Coronavirus: Can pregnant mothers infect their children with COVID-19?
Kwa mujibu wa WHO, kuna tafiti mbalimbali zinazoashiria kuwa hakuna uwezekano wa maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto aliye tumboni. Pia wameeleza kuwa #CoronaVirus havikukutwa kwenye maji ya uzazi “amniotic fluid” wala maziwa
Wakati inaelezwa kuwa wajawazito wasio na matatizo mengine hawako katika hatari ya kuambukizwa #COVID19 kuliko watu wengine, wanashauriwa kuchukua tahadhari kubwa
Vilevile, si lazima mjamzito ambaye anaonesha dalili za #COVID19 kujifungua kwa njia ya upasuaji bali njia ya uzazi itategemea na mapendeleo yake na ushauri wa mtaalamu
Mama aliyeathirika anaruhusiwa kumnyonyesha mwanae huku akizingatia taratibu za kuzuia maambukizi ikiwemo kuvaa barakoa muda wote awapo na mtoto na kunawa mikono kabla ya kumshika
Source: Coronavirus: Can pregnant mothers infect their children with COVID-19?
Upvote
0