COVID19: Ushauri kwa Watalii au Wasafiri wanaotoka Tanzania kwenda maeneo mbalimbali nje ya nchi

COVID19: Ushauri kwa Watalii au Wasafiri wanaotoka Tanzania kwenda maeneo mbalimbali nje ya nchi

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
Anga la Tanzania likiwa limefunguliwa na kuruhusu wasafiri kutoka pande mbalimbali za dunia, inategemewa kuwa hivi karibuni nchi mbalimbali zitafungua mipaka na shughuli za utalii zitaanza kuimarika upya.

Ingawa si jambo linaloshauriwa lakini hakuna namna ya kulizuia kwani Maisha lazima yataendelea na kila mtu ana uhuru endapo havunji sheria wala taratibu.

Mapendekezo yanayotolewa kwa Watalii wa Kimataifa ni kama ifuatavyo

Ø Ni jambo jema zaidi endapo unaumwa au una matatizo ya kiafya kama Kisukari, Shinikizo la Damu, Pumu au una umri mkubwa kuepuka au kusubiri kwanza kabla ya kufanya safari za kimataifa

Ø Taratibu za jumla za usafi ikiwemo kunawa mikono kwa maji tiririka na sabuni mara kwa mara, uvaaji barakoa, Kukohoa kistaarabu (kwenye sehemu ya ndani ya kiwiko cha mkono au kwenye tishu ambayo itatupwa mara tu baada ya kumaliza), na kuepuka kushika pua au mdomo zizingatiwe

Ø Umakini unahitajika katika suala zima la chakula kuanzia usafi wa mikono ya mlaji na eneo utakaponunua chakula, uandaaji wake pamoja na ufungashaji. Epuka chakula ambacho hujaona uandaaji wake au ambacho kinauzwa eneo la wazi ambalo watu wanapita au kinachouzwa na mtu asiyevaa barakoa

Ø Epuka kwenda maeneo ya misongamano ya watu ambapo itakuwa ngumu kuweka umbali wa mita 1 kati yako na mtu mwingine

Ø Uendapo kwenye “museums” au vivutio vingine epuka kushika sehemu za pembeni ya ngazi, kushika vitu vilivyo katika maonesho, kushikana mikono na watu kwani ni sehemu zinazotembelewa na watu wengi kwa siku

Ø Epuka kujihusisha kingono na watu wa eneo utakaloenda kwani ni rahisi sana kupata maambukizi wakati wa tendo

Ø Kuwa makini unapotumia vilevi. Inashauriwa zaidi kutumia vilevi uwapo ndani ili kuweza kujidhibiti unapolewa

Ø Utakaporudi nchini ni sharti ujitenge kwa siku 14 ili kuepuka kusambaza maambukizi (endapo umepata) kwa wengine
 
Upvote 0
Kuhusiana na hili la vyakula. Binafsi niliwahi kuandika uzi kuangazia mustakabali wake:

Hizi biashara za vyakula hazisambazi covid-19 kweli?

Kwenye travel advisory hii bila shaka tokea nje, pana onyo la dhahiri kuhusiana na vyakula na maambukizi ya Corona.

Kwa nini wenye mamlaka wakiwa wanajua hatari za vyakula hivi na ugonjwa huu wameendelea kupiga kimya wakiachia wengine kuambukizwa pasipo na kujali?

Enyi tuliowapa dhamana tuwaamini kwa lipi kama hata kwenye kutupa ukweli kamili wa na ya kujikinga mnaamua kutotwambia?
 
Hapo pa vilevi kunywea ndani labda wanaoenda nje kufanya mambo serious. Ila wale wa kutalii, yaani niende zangu nje kustarehe halafu ninywe ndani?
 
Hapo pa vilevi kunywea ndani labda wanaoenda nje kufanya mambo serious. Ila wale wa kutalii, yaani niende zangu nje kustarehe halafu ninywe ndani?
Kwa hali ilivyo bora tu unywee ndani maana starehe ya siku moja halafu upate maambukizi ambayo huenda yakagharimu uhai yafaa nini?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom