Pre GE2025 CP Awadhi Haji: Sio kweli kwamba Jeshi la Polisi linakandamiza baadhi ya Vyama vya Siasa

Pre GE2025 CP Awadhi Haji: Sio kweli kwamba Jeshi la Polisi linakandamiza baadhi ya Vyama vya Siasa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
Kamishina wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi Nchini CP Awadhi Haji amesema kuwa mtazamo wa kudhani kwamba Jeshi la Polisi linakandamiza baadhi ya vyama vya siasa sio wakweli.

"Wakati mwingine unakuta baadhi ya vyama vya siasa vimekuwa na dhana hiyo yakudhani labda Jeshi la Polisi limekuwa likiwakandamiza jambo ambalo sio" amesema CP Awadhi Haji

CP Awadhi Haji amesema kwamba dhana hiyo inaweza kuwa ikawa inatokana na utofauti wa mitazamo na uelewa uliopo kwa Watu.

Lakini amesema kuwa Jeshi la Polisi lipo kwa ajili ya kusimamia uzingatiaji Sheria bila kuwa na upendeleo isipokuwa kwa kuzingatia Sheria na taratibu.

Ameyasema hayo wakati akishiriki mafunzo ya kukumbushiana Sheria na miongozo mbalimbali kwa makamanda wa Jeshi la Polisi kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu, ambapo mafunzo hayo yanaratibiwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC)

Ikumbukwe kauli hiyo anaitoa ikiwa ni siku chache baada ya baadhi ya vyama vya siasa na wanaharakati mbalimbali kulitaka Jeshi la Polisi kutekeleza majukumu yao kwa uweledi kwa kuzingatia Sheria, taratibu na maadili vinavyowaongoza katika utekelezaji wa majukumu yao.
 
Back
Top Bottom