Kwa vyovyote hii ni project ambayo ilifanyiwa uchambuzi wa kina na kuonekana ku-breakeven ndani ya muda fulani unaokubalika ndio maana benki walimkubalia kumkopesha. Kwa hiyo riba ya benki au elimu ya ujasiriamali sio sababu za kumfanya kushindwa kulipwa.
Huyu bwana atakuwa amefanya misappropriation (kutumia pesa za mkopo wa shule kwenye shughuli nyingine ambazo hazihusiani na shule au mradi ulioidhinishwa na benki) kiasi cha kumfanya ashindwe kuendesha shule kwa faida ambayo ingemwezesha kuendelea kulipia mkopo wa benki na gharama za uendeshaji wa shule.
Duh, ngombe wa maskini hazai! Huyu Mkandawile alihangaika sana kuipata hiyo shule, alikuwa anfundisha tuition ya Chemistry usiku na mchana! Yaelekea alikosa tu elimu ya ujasiriamali