OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
Hebu tupate kumfahamu Saidi Ntibazonkiza kwa ufupi, jamaa amezaliwa 1 May 1987 kwa majirani zetu hapo Bujumbura Burundi kwa hiyo kwa sasa ana miaka 33.
Kuhusu umri tuache hivyo hivyo tu maana inasemekana Kagame Cup ya 1997 alicheza. Ukipiga hesabu hapo alicheza akiwa na miaka 10.
Mwamba alianza kucheza soka katika klabu ya Vital’O ya Burundi kuanzia mwaka 2003 hadi 2005. Baadaye alihamia Uholanzi na klabu ya NEC ndio ilikuwa ya eneo la jirani na makazi yake kwa hiyo alianza kufanya mazoezi na timu ya vijana.
Baadaye akasajiliwa kwa mkataba wa kudumu na NEC, mwanzoni mwa msimu wa 2006-07 alianza kwa kucheza timu ya vijana lakini baada ya muda mfupi alipandishwa kwenyebtimu ya wakubwa na mnamo November 18, 2006 alicheza mechi yake ya kwanza kwenye Ligi ya Uholanzi dhidi ya Sparta Rotterdam.
Alidumu NEC kwa miaka minne (2006-2010) akiwa amecheza mechi 70 na kufunga mabao nane
Mwaka 2010 aliondoka NEC na kujiunga na KC Cracovia ya Poland ambapo alidumu kwa miaka minne pia kuanzia 2010 hadi 2014 huku akicheza mechi 85 na kufunga magoli 17.
Baada ya hapo akatimkia zake Uturuki na kujiunga na Akhisar Belediyespor ambapo alidumu kwa mwaka mmoja tu (2014-2015), huku akicheza mechi 13 na kufunga goli moja pekee!
Safari haikuishia hapo, mwaka 2015 akajiunga na Caen ya Ufaransa. Alianzia Caen B ambapo alicheza mechi nne na alifunga goli moja. Baadaye akapelekwa Caen ya wakubwa ambapo alicheza mechi 14 na kufunga goli moja kwa mwaka mmoja ambao alicheza hapo.
Baada ya kuondoka Ufaransa, mwaka 2017 akaenda zake Kazakhstan na kujiunga na FC Kaysar Kyzylorda ambayo aliichezea mechi 10 na kufunga mabao mawili.
Baada ya miaka 12 ya kuzunguka Ulaya, akarudi zake nyumbani Burundi kwenye klabu yake aliyoanzia maisha ya soka Vital’O.
Jana ametia dole gumba kuitumikia timu ya WANANCHI Yanga SC.
Kuhusu umri tuache hivyo hivyo tu maana inasemekana Kagame Cup ya 1997 alicheza. Ukipiga hesabu hapo alicheza akiwa na miaka 10.
Mwamba alianza kucheza soka katika klabu ya Vital’O ya Burundi kuanzia mwaka 2003 hadi 2005. Baadaye alihamia Uholanzi na klabu ya NEC ndio ilikuwa ya eneo la jirani na makazi yake kwa hiyo alianza kufanya mazoezi na timu ya vijana.
Baadaye akasajiliwa kwa mkataba wa kudumu na NEC, mwanzoni mwa msimu wa 2006-07 alianza kwa kucheza timu ya vijana lakini baada ya muda mfupi alipandishwa kwenyebtimu ya wakubwa na mnamo November 18, 2006 alicheza mechi yake ya kwanza kwenye Ligi ya Uholanzi dhidi ya Sparta Rotterdam.
Alidumu NEC kwa miaka minne (2006-2010) akiwa amecheza mechi 70 na kufunga mabao nane
Mwaka 2010 aliondoka NEC na kujiunga na KC Cracovia ya Poland ambapo alidumu kwa miaka minne pia kuanzia 2010 hadi 2014 huku akicheza mechi 85 na kufunga magoli 17.
Baada ya hapo akatimkia zake Uturuki na kujiunga na Akhisar Belediyespor ambapo alidumu kwa mwaka mmoja tu (2014-2015), huku akicheza mechi 13 na kufunga goli moja pekee!
Safari haikuishia hapo, mwaka 2015 akajiunga na Caen ya Ufaransa. Alianzia Caen B ambapo alicheza mechi nne na alifunga goli moja. Baadaye akapelekwa Caen ya wakubwa ambapo alicheza mechi 14 na kufunga goli moja kwa mwaka mmoja ambao alicheza hapo.
Baada ya kuondoka Ufaransa, mwaka 2017 akaenda zake Kazakhstan na kujiunga na FC Kaysar Kyzylorda ambayo aliichezea mechi 10 na kufunga mabao mawili.
Baada ya miaka 12 ya kuzunguka Ulaya, akarudi zake nyumbani Burundi kwenye klabu yake aliyoanzia maisha ya soka Vital’O.
Jana ametia dole gumba kuitumikia timu ya WANANCHI Yanga SC.