Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,872
- 34,363
Cyber crime
KWA KISWAHILI NA KWA UREFU ZAIDI;
Umoja wa Ulaya Waiasa Tanzania Kuhakikisha Sheria ya Uhalifu wa Mtandaoni ya mwaka 2015 Haikiuki Haki za Raia Wake.
Mabalozi wa Umoja wa Ulaya, Ubelgiji, Denmark, Ufini, Ufaransa, Ujerumani, Ireland, Italia,
Uholanzi, Hispania, Sweden, Uingereza na Mabalozi wa Canada, Norway, Uswisi na Marekani
wanaikumbusha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa ilijizatiti kutumia Sheria
ya Uhalifu wa Kimtandao ya 2015 kwa namna ambayo inaheshimu uhuru wa kimsingi na
kushughulikia uwezekano wa tafsiri hasi ya sheria hiyo. Hata hivyo, kesi za kwanza za
matumizi ya sheria hiyo zimeongeza wasiwasi katika ukiukwaji wa misingi ya uhuru.
Mabalozi wana wasiwasi kuhusu kukamatwa hivi karibuni kwa wafanyakazi wa Kituo cha Sheria
na Haki za Binadamu (Legal and Human Rights Centre) pamoja na vifaa muhimu vya kiufundi,
Sehemu ya 16 ya Sheria ya Uhalifu wa mitandao ikitumika kama rejea. Matukio hayo yalitokea
wakati shirika hilo lilikuwa likiandaa maoni yaliyotolewa na waangalizi wa uchaguzi nchini
kote, kazi ambayo kituo hicho cha haki za binadamu kilipewa kibali na Tume ya Taifa ya
Uchaguzi. Mabalozi wanafahamu kuwa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ni mwanachama
wa Umoja wa Watetezi wa Haki za Binadamu.
Kama ilivyoelekezwa katika Mkataba wa Demokrasia wa Afrika, Uchaguzi na Utawala, Mabalozi
wanaamini "kuna haja ya kuimarisha waangalizi wa uchaguzi katika nafasi yao, hasa kwa
kuzingatia umuhimu wao katika kuhakiki utaratibu, uwazi na uaminifu wa chaguzi."
Mabalozi wanaisihi Serikali ya Tanzania kuhakikisha utekelezaji wa Sheria ya Uhalifu wa
Kimtandao haisababishi uvunjifu wa haki za binadamu na uhuru wa kimsingi, hasa uhuru wa
kujieleza na kujumuika na haki ya kushiriki katika chaguzi za uhakika na kwamba inaheshimu
misingi ya utawala bora na jukumu la waangalizi wa uchaguzi na mashirika ya kiraia katika
michakato ya kidemokrasia.
KWA KISWAHILI NA KWA UREFU ZAIDI;
Umoja wa Ulaya Waiasa Tanzania Kuhakikisha Sheria ya Uhalifu wa Mtandaoni ya mwaka 2015 Haikiuki Haki za Raia Wake.
Mabalozi wa Umoja wa Ulaya, Ubelgiji, Denmark, Ufini, Ufaransa, Ujerumani, Ireland, Italia,
Uholanzi, Hispania, Sweden, Uingereza na Mabalozi wa Canada, Norway, Uswisi na Marekani
wanaikumbusha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa ilijizatiti kutumia Sheria
ya Uhalifu wa Kimtandao ya 2015 kwa namna ambayo inaheshimu uhuru wa kimsingi na
kushughulikia uwezekano wa tafsiri hasi ya sheria hiyo. Hata hivyo, kesi za kwanza za
matumizi ya sheria hiyo zimeongeza wasiwasi katika ukiukwaji wa misingi ya uhuru.
Mabalozi wana wasiwasi kuhusu kukamatwa hivi karibuni kwa wafanyakazi wa Kituo cha Sheria
na Haki za Binadamu (Legal and Human Rights Centre) pamoja na vifaa muhimu vya kiufundi,
Sehemu ya 16 ya Sheria ya Uhalifu wa mitandao ikitumika kama rejea. Matukio hayo yalitokea
wakati shirika hilo lilikuwa likiandaa maoni yaliyotolewa na waangalizi wa uchaguzi nchini
kote, kazi ambayo kituo hicho cha haki za binadamu kilipewa kibali na Tume ya Taifa ya
Uchaguzi. Mabalozi wanafahamu kuwa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ni mwanachama
wa Umoja wa Watetezi wa Haki za Binadamu.
Kama ilivyoelekezwa katika Mkataba wa Demokrasia wa Afrika, Uchaguzi na Utawala, Mabalozi
wanaamini "kuna haja ya kuimarisha waangalizi wa uchaguzi katika nafasi yao, hasa kwa
kuzingatia umuhimu wao katika kuhakiki utaratibu, uwazi na uaminifu wa chaguzi."
Mabalozi wanaisihi Serikali ya Tanzania kuhakikisha utekelezaji wa Sheria ya Uhalifu wa
Kimtandao haisababishi uvunjifu wa haki za binadamu na uhuru wa kimsingi, hasa uhuru wa
kujieleza na kujumuika na haki ya kushiriki katika chaguzi za uhakika na kwamba inaheshimu
misingi ya utawala bora na jukumu la waangalizi wa uchaguzi na mashirika ya kiraia katika
michakato ya kidemokrasia.