Mwanaharakati huru, Cyprian Musiba, amewataka wasanii wa Tanzania kutumia ushawishi wao kutangaza mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Akizungumza na Jambo TV jijini Dodoma tarehe 3 Machi 2025, Musiba amesema kuwa kuelekea Uchaguzi Mkuu, ni muhimu kuweka nguvu kubwa katika kusambaza taarifa kuhusu mafanikio ya Rais Dkt. Samia, huku akibainisha kuwa wasanii ni miongoni mwa watu wanaopaswa kushiriki kikamilifu katika jukumu hilo.
Hata hivyo, kauli yake imekuja miezi michache tu baada ya yeye mwenyewe kueleza kuwa haoni umuhimu wa wasanii kushiriki katika matukio ya kiserikali, na kuwashauri Watanzania kuwapuuza.
Akizungumza na Jambo TV jijini Dodoma tarehe 3 Machi 2025, Musiba amesema kuwa kuelekea Uchaguzi Mkuu, ni muhimu kuweka nguvu kubwa katika kusambaza taarifa kuhusu mafanikio ya Rais Dkt. Samia, huku akibainisha kuwa wasanii ni miongoni mwa watu wanaopaswa kushiriki kikamilifu katika jukumu hilo.
Hata hivyo, kauli yake imekuja miezi michache tu baada ya yeye mwenyewe kueleza kuwa haoni umuhimu wa wasanii kushiriki katika matukio ya kiserikali, na kuwashauri Watanzania kuwapuuza.