D.B. Cooper: Tukio halisi la kusisimua lililogeuka hadithi ya 'Alfu lela ulela'

kutokana na kanuni za sehemu ya tufani yako ya kutolea shekeli zako ni illegal kwenye maeneo yenye miguu mingi. Hii ni chenga ya moyo.
 
safi kiongozistory nzuri sana nimejifunza mengi
 
Mkuu puuza mbali ushauli kama huo wa mym watu kama hawa ndo wanasababisha watz wengi wawe na uelewa mdogo sana. Fikilia vitabu vya ujasusi vya kibongo jinsi vilivyokuwa vikipigwa marufk au hata kuhaririwa kiasi kwamba dhana kuu ya kitabu inapotea, inafikia wataki watz walio wachache kati ya wengi wanafahamu CIA na FBI wanavyofanya kazi kuzid askali kanzu na maafisa usalama wetu na walio wengi ndo 0 kabsa. Sababu kuu ndo kama hizo za huyu mym. Hazina mantiki wala mashiko. Hizi juzi ze komedi kuvaa nguo zinazofanana na jeshi la polisi basi imekuwa nongwa. Najiulza kama USA wangekuwa kama sis wangeweza kuchez series kama prison break au 24hrs na nyinginezo?? Some time huwa nafkir ni silikari ndo huwafanya watu kuwa na uwezomdogo wa kufkiri. Hivi majuzi mbongo mwenzetu kajitahidi kutumia akili aliyozaliwa nayo kutengeneza helikopta yake hadi kufikia kuzungusha yale mapanga yake TMA wakamchimba mkwara mzito, Vipi kama ingefikia hatua ya kuipaisha si angeozea segerea??? Some time I hate this....
 
Huyu Cooper nahic aliruka kwenda juu hakurudi chini[emoji23] [emoji23]

Wakuu hii kitu haina majibu kama FBI wamekaa 45yrs eti wewe uje upate majibu baada tu ya kusoma kwa the bold.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Umeuaaaa na bado hapo mwingne anachimba mikwara kuwa The Bold asitiririke zaid. Watz buana
 
Sema sisi tatizo lugha hatuinjoi vizuri ndio maana tunakimbilia huku walikotafuna akina The bold ili tumeze vizuri!
Ni kweli The Bold (who fears) ametutafunia kila kitu japo na yeye "ametupeleka peleka" baadhi ya sehemu.

Kwa mfano sio kweli kwamba Cooper aliruka na parachute mbili mbovu. Aliruka na parachute moja ya ukweli na moja ya kujifunzia, ambayo haifunguki. Na hapo ndio umakini wa Cooper umehojiwa, utachukuaje parachute limeandikwa "halifunguki, kwa mafunzo tu..."

Na si kweli kwamba 727 ni ndege "ambayo unaweza ku control "manually" speed ya ndege na mwinuko wa ndege hata ukiwa sehemu ya abiria." Yani manufacturer atengeneze ndege ambayo abiria tusipopenda spidi na altitude ya ndege tunai boost up wenyewe huku nyuma....duuuuh! That's another new one.

Na si kweli kwamba FBI walisambaza serial number za hela baada ya kumkosa Cooper mwaka na zaidi. Serial zilisambazwa immediately baada ya tukio.

Na si kweli kwamba 727 inaruka maximum altitude ya 10,000ft aliyoitaka Cooper. Ingekuwa inagonga sana milima. Cooper alitaka ndege iruke 10,000 ft ili iwe chini chini, sio maximum height. 727 zinakwenda mpaka 40,000ft. Soma hapa tafadhali.

Na si kweli kwamba utaratibu wa mizigo ya abiria kusachiwa ulianza baada ya tukio la Cooper. Kuna matukio mengi ya kupenyeza mabomu yaliendelea kutokea baada ya hapo na bila kuwepo ku sachiwa. Mfano TWA Flight 57 ilipenyezwa bomu na kulipuliwa Las Vegas Nevada. In fact TWA 57 was the watershed moment in commercial aviation security. Angalia hapa na hapa.

Na si kweli kwamba Cooper alijitambulisha kama D B Cooper kama The Bold alivyosema kwenye mstari wake wa mwisho wa stori. Akinunua tiketi, alijitambulisha kama Dan Cooper.
 
Na si kweli kwamba Cooper alijitambulisha kama D B Cooper kama The Bold alivyosema kwenye mstari wake wa mwisho wa stori. Akinunua tiketi, alijitambulisha kama Dan Cooper.

Nashukuru kwa point zako mkuu, ntakujibu kadiri ntakavyoweza lakini naomba na hicho kipengele japo juu..

Kwanza kabisa nahisi hujaisoma stori niliyoiandika kwasababu kama ungesoma ungelifahamu kuwa katika katika paragrafu za mwanzo kabisa nimeandika hivi, nanukuu;

"...alifika katika counter ya kampuni ya ndege ya Northwest Orient Airlines na akatoa fedha cash dola 20 na kununua tiketi ya ndege flight 305 kwenda mjini Seattle............. Jamaa huyu alijitambulisha kama Dan Cooper"

Bado sijaelewa kitu unachojaribu kusahihisha!

Pia nafahamu kwanini jina linaloripotiwa lilibadilika kutoka kuwa Dan Cooper mpaka D.B Cooper! Ni vile baada ya tukio FBI walimshikilia kwa muda jamaa fulani mjini Portland kwa kuwa jina lake aliitwa D.B Cooper na alikuwa na rekodi ya uhalifu hivyo kufanana huku kwa majina kati ya jina lake na jina la Dan Cooper kukamfanya awe suspect kwa muda na vyombo vya habari pasipo kujua wakidhani yule ndiye mtuhumiwa halisi wakaanza kuripoti hilo tukio kwamba limetekelezwa na mtu aliyeitwa D.B Cooper na imeendelea hivyo mpaka leo licha baadae FBI kusisitiza kuwa yule jamaa hausiki na hilo tukio lakini mazoea yamebakia hivyo kuwa jina la mtekaji yule wa ndege anatambuliwa kama D.B Cooper!

Ntarudi kukujibu hoja zilizobaki kadiri ntavyoona inafaa kuzijibu ama la!
 
Asante kwa maelezo yako. Lakin yote story ilikuwa nzuri. Si rahisi saana msimuliaji akasimulia jinsi tukio lilivyokuwa kwa ufasaha aslimia mia na simuliz likapendeza bila ya kuweka maneno yake "ama kwa kujua au kutokujua" ili iwe rahisi kueleweka kwa hadhila.
 

Mkuu hii hoja uliikazania sana tangu jana na nikajitahidi kukujibu kadiri nilivyoweza nikaandika maelezo marefu sana kana kwamba naandika stori nyingine mpya, nilidhani umenielewa nashangaa kwanini unarise tena hoja hii ambalo nimejitahidi kadiri niwezavyo kutoa mawazo yangu kwanini cooper hakutumia parashuti 'nzima'! Tafadhali soma post #249
 
Na si kweli kwamba FBI walisambaza serial number za hela baada ya kumkosa Cooper mwaka na zaidi. Serial zilisambazwa immediately baada ya tukio.

Mkuu sijajua neno immediately kwako li amaana gani lakini kwa tafsiri yangi mimi ukizingatia muda ambao FBI walizisambaza hizo serial numbers haikuwa "immediately" baada ya tukio.. Na mfumo walioutumia awali kusambaza serial number ulikuwa wa kizamani kwamba mtu ingelimbidi alinganishe noti alizonazo na namba za hela ya cooper manually!

Yani kwa mfano; kama nina mgahawa wangu na akaja na hela za Cooper akanunua chakula na mimi sijajisumbua kuzilinganisha fedha nilizopewa na orodha ya FBI ya serial number za hela za Cooper basi zitapita katika mikono yangu na mzunguko wangu binafsi wa hela pasipo kujua na kwenda kwa mwingine..

Haikuwa immediately na haikuwa effective.
 
Na si kweli kwamba utaratibu wa mizigo ya abiria kusachiwa ulianza baada ya tukio la Cooper. Kuna matukio mengi ya kupenyeza mabomu yaliendelea kutokea baada ya hapo na bila kuwepo ku sachiwa.

Mkuu sijui usahihi wa hicho ulichokisema ni wa kiwango gani lakini niseme tu mimi nimeandika kwa kadiri ya ninachokifahamu!
Na ninachokifahamu ni kwamba baada ya tukio la Cooper mwaka 1971, mwaka uliofuata 1972 kulikuwa na taribani matukio 13 ya watu kuteka ndege kuiga alichokifanya Cooper (wote walikamatwa au kuuawa), na ninachofahamu ni kwamba baada ya hapa ndipo sasa vyombo vya usalama vikaanzisha/kusisitiza utaratibu wa kukagua mizigo ya abiria kabla ya kupanda ndege na ulitokea upinzani mkali mpaka watu kuifungulia serikali kesi za kikatiba mahakamani kupinga hili suala.

Kama nilivyosema naandika kile ambacho nakifahamu, na hicho ndicho ninachokifahamu! Kama siko sahihi basi ni makosa ya kibinadamu kwani mimi pia ni binadamu na siwezi kufahamu kila kitu.
 
Achana nae.. Anakupoteze mda wako
 
Ni kweli The Bold (who fears)

Mkuu, naona hili nalo umelikomalia toka jana kwamba 'sifunguki' kila kitu kwa sababu ya uoga usiokuwa na maana yoyote ile!! Let me tell you a little story..

Kwa unyenyekevu kabisa pasipo kujivuna niseme kuwa nimekuwa moja ya wanaJF ambao wamekuwa wathubutu kuanzisha nyuzi con traversal ambazo mda mwingine zinahatarisha hata usalama wangu! Na hapa siongelei hadithi za akina cooper au akina narbartolo ambao nimepost siku za hivi karibuni.. Huko nyuma mwaka 2014 nilipost vitu vya kutatanisha humu vingine vilikuwa fiction, vingine fiction iliyochanganyika na ukweli na vingine ukweli mtupu (hizo nyuzi bado zipo unaweza kuziangalia) na ziliniletea sekeseke za kutosha tu. Tangu nimerudi tena JF sipendi kuongelea hizo mambo.. wengi hawafahamu kuwa zile mambo zilizusha mushkeli sana, na kwasehemu zilinigharimu! Niishie hapo tu..

Sasa ninachojaribu kusema ni nini??? Katika uzi wangu uliopita ambao ulimuhusu 'The Friday Night Bank Robber' kwenye upande wa comments kuna sehemu nikasema "dah kuna jamaa amenipa inside story ya wajamaa walioiba makontena ya Copper kutoka Zambia the story is very interesting kwasababu ishu ilikuwa very organised natamani niisimulie lakini nahofia kuna watu 'tutaanza kusumbuana'" kuna mdau akanijibu simulia tu usiogope nikamwambia labda nikisimulie niziache details nyingi na nahisi nikifanya hivyo nitapunguza utamu wa stori.

Maana yangi ni kwamba, kuna muda lazima tujifunze kuchora mstari. Ingawa tunasimuliana haya mambo ili kuenjoy tu na kukuza fikra zetu na maarifa lakini lazima tuwe na kiasi kwa kiwango tunacho 'funguka' kuhusu haya mambo.
Pia fahamu kuwa siongelei tu sijui stori ya cooper, sijui nortarbatolo, No naongelea haya masuala kwa ujumla wake.

Anyways, sikutaka kuongelea haya mambo yote hivi ila naona toka jana umenikomalia The Bold muoga alafu uoga wake hauna maana, so imenibidi tu 'povu' linitoke kwa kiasi hiki ili tufahamiane sawa sawa

Naamini umenielew mkuu.!
Tuendelee kufurahia simulizi, haya mambo mengine tuachane nayo..
 
Kwanza kabisa nahisi hujaisoma stori niliyoiandika kwasababu
Nimeonyesha mtiririko wa makosa na vibwagizo vya kibunifu vilivyosheheni katika hadithi yako, utasemaje hadithi sijaisoma? Hahahaaaaaa....

Wewe ndio umesema "mwenyewe alijitambulisha kama DB Copper..." Well, Cooper hakuwahi kujitambulisha kama D B Cooper, umeteleza, usinilaumu mimi. Hukuyasema?

Umedai Cooper alichagua Boeing 727 kwa sababu ndege hii unaweza kuibadilisha speed pamoja na kuinyanyua angani na kuirudisha chini "manually" kutokea huku tunakokaa abiria! You said that, didn't you? Hahahaaa...

Na ukasema Cooper alichagua Boeing 727 kwa vile haziruki zaidi ya 10,000ft. Jamani, 727 imekuwa propeller aircraft ya Idara ya Wanyama Pori?

And you leveraged those points to show that Cooper was a hellacious genius. Sasa najiuliza, hata ma DCM yetu njia panda ya Tandika-Yanga-Mango abiria hatujapewa access ya kupunguza spidi ya gobole kutokea kwenye viti vyetu! Iweje kitu delicate cha kuruka angani wawape machizi kama Cooper access ya ku control ndege manually???

Huwezi kukwepa lawama ya ku embellish your story only to paint Cooper as a super human criminal mastermind. Tuna matatu tunapoendelea mbele: Uthibitishe kauli zako, ufute kauli zako, au ufungiwe indefinately kwa kupotosha umma.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…