D.B. Cooper: Tukio halisi la kusisimua lililogeuka hadithi ya 'Alfu lela ulela'

Tuwekee yako ambayo ni sahihi mkuu
 
Bila shaka mkuu nitakutag.. Umetisha sana kiongozi! Ila tukumbukane basi hizo lunch mkuu hahahahah
Hahahahaha usijali mkuu lunch zenyewe za migahawani, wali nyama 1,500/= finyango 2 moja inalika nyingine unatupa, mchuzi rangi ya supu ila unaambiwa imeungwa na nyanya. Anyway ukianzisha story nyingine takuwa nakurushia hata jero ya pepsi.
 
Au twambie sasa kwamba story yoooote ni uzushi.

Maana hakuna kitu kama hicho.
That's right, nakubali na ndicho ninachokisema, hakuna kitu kama hicho!

Ndege haiwezi, nini ndege, Bajaji haiwezi kuwa na operation controls wanakokaa abiria, zingetekwa sana na ma terrorist! Ngalawa na mitumbwi ndio abiria wote tuna controlling authority juu ya mwendo wa chombo chetu kwa sababu sote tunapiga makasia! Sio ndege, sio treni, sio gari, sio Bajaj.

Kuhusu whether hii stori ni mara yangu ya kwanza kuisikia, au kwamba sijui natatufa kiki kwa stori ya mwingine, well, hapa sio Facebook, sio Instagram, hatuna kitu hicho hapa cha kusema hii stori ya fulani usiiguse unatafuta kiki, that's purile, utoto. Ukileta mada watu wanajadili freely, unaongeza kama unacho, kuna kukosoana na ukichemka ukabisha unamalizwa vile vile, you take your medicine.

Natafuta kiki nani ananijua? Mnaokotoa okota every new lingo in town, hata maneno ya vijana na vitoto vya show biz mnataka kuleta JF. Kutafuta kiki ni maneno yanayo spill over into tabloids kutoka kwenye mabishano ya Instagram za kina Team Wema, na Team Lulu na kile kijana kilichoshinda Big Brother. Sio hapa JF! Don't drag JF into the muck.

In the final analysis, hakuna commercial jet aircraft inayoishia 10,000ft. Hiyo ni propeller craft ya Idara ya Wanyama Pori.

Hakuna ndege ambayo abiria wana access na control devices. Huyo ni farasi na piki piki ndio abiria ukijitikisa tikisa kwa nguvu unaweza kuhujumu chombo, sio ndege.

Dan Cooper hakuchagua 727 kwa sababu hizo, hazipo. Hakuwa makini ki hivyo.
 

Nilidhani utaelewa mantiki yangu kwamba hukuwa na haja ya kuendelea kukosoa tena na tena.kurudia rudia.
Hapa ndipo mtazamo wa kick ulipokuzoa.

Binafsi niliona toka mwanzo kwamba kuna vitu haviko sawa,lakini hii si stori????, tena ya mwaka sabini??? Kuanza kutafuta usahihi wake kwa nguvu namna hii ili iwe nini hasa!!!!

Hata kama haikuwa hivyo unavyosema bado stori ni kwamba cooper hajaonekana mpaka leo na pesa hazikupatikana chini ya umakini mkubwa.mh?????
 
Daah yani hata mimi hapo ndipo ninapomshangaa huyu mjomba! Yani anapost kitu kile kile tena na tena.. Nimejitahidi nimjibu au labda kumwambia poa yaishe kama kuna mahali nimekosea mimi ni binadamu, lakini bado mjomba haelewi, anarudi anapost tena mambo yale yale! Khaaa ninemshauri basi mkuu andika uzi utupe hiyo version yako lakini wapiiiii mjomba haelewi.. Ndio hapo nikagundua huyu mtu anatafuka 'kiki' alafu anasahau watoto wa mjini wanamsemo wao Siku hizi wanakwambia #HatutoiKiki #UsifosiTufanane
 
Hahahahaha usijali mkuu lunch zenyewe za migahawani, wali nyama 1,500/= finyango 2 moja inalika nyingine unatupa, mchuzi rangi ya supu ila unaambiwa imeungwa na nyanya. Anyway ukianzisha story nyingine takuwa nakurushia hata jero ya pepsi.
migahawa yetu unaagiza wali rosti nyama unaletewa wali supu! Ukimwambia sitaki supu nimeagiza wali rosti nyama anakwambia ndio hii nimekuletea.. Hahahahaha
 
Binafsi niliona toka mwanzo kwamba kuna vitu haviko sawa,lakini hii si stori????, tena ya mwaka sabini??? Kuanza kutafuta usahihi wake kwa nguvu namna hii ili iwe nini hasa!!!!


No, you are wrong. This is not a fictional. Tukio lilitokea, huna creative license ya kubadilisha hadithi.

Ever so briefly, mimi nilichangia kwamba sioni kuwa Cooper ni genius kihivyo. Wengine, akiwemo The so-called Bold, wakatumia wrong claims za features za Boeing 727 ili kuonyesha umakini wa Cooper alipochagua ndege ya kuteka. Nilipohoji hayo madai all hell broke loose!

Kwamba hii stori tu, haikosolewi. Well, this is a true story, huwezi kuongeza vichorombwezo vyako ili kum paint Cooper as a cosmic criminal mind who draws up his plans with differential equations. Hakuna ubaya kusahihisha makosa kwenye tukio la ukweli, sio fiction hii.
 
Nimependa umahiri wa D. Cooper ,kwanza inadhirisha kwamba hakukurupuka,halafu ana uzoefu wa kutosha (ambao hatujui aliupata wapi), lakini nahisi kutoka na mtu wa namna hii,tunaweza kujifunza mengi ya kiusalama (intelligence).

Mimi nahisi huyu kiumbe /mtu hakutoka sayari hii (extraterrestrial)
 
Mkuu huyo jamaa usihangaike nae...muache tu apite mbele..watu wengine ni matatizo ya malezi yan hawaelewi kitu...so kumuelewesha ni kama kujaza maji kwenye tenga
 
The db cooper case was a hoax by the fbi yall dnt kno dar
 
Kwakua hata marubani hawakuwa wanajua km ndege yao inafunguka mlango wa nyuma ila FBI tu, basi watekaji ni wao na mmoja wao alieteka ndege wao ndio walimtowesha pamoja na ushahidi wake, alitolewa kwenye ndege kwa ndege mbili zilizokuwa zimeruka chini na juu ya ndege ya mateka, ndege ya chini ndio ilimchukua iwe kwa kutumia kamba na mwendo sawa au kwa kushikwa mkono ktk mwendo ulio sawa.
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Umeuaaaa na bado hapo mwingne anachimba mikwara kuwa The Bold asitiririke zaid. Watz buana
Hahahahahaa ni kutaka kujitanabaisha kwamba na yeye anafahamu mambo ya usalama. Sasa karne hii movie kibao zimejaa zinaonyesha masuala ya kijasusi vp the bold asitiririke kwa tukio lilokwisha miaka 45 iliyopita wakati hata wao wenyewe wana mpango wa kulitengenezea sinema yake.
 
Kwameh unajua unachefua na unataka watu wapewe BAN humu jamvini
  • kwanini na wewe usilete story yako ya filamu ambayo si fiction na tuichambue
ni vitabu vingapi vimetungwa kuhusu hili tukio wakati wewe unasema unalijua kuwa ni la kweli.

kwa hiyo hata The bold akiongezea ww hayakuhusu acha watu ambao hawawezu kusearch kutumia search engine km Wekipedi au Google wafaidi.
unaposema hii story haikosolewi ndipo napokudharau na kuchefua nakuomba tu unyamaze kwani juzi tu lilikuwepo Kongamano la kuchambua huu ukweli ingawa FBI walishalifunga
If you crave more DB Cooper – even after the History Channel broadcasted their four-hour documentary and the FBI closed the case last month – you can partake in another Cooper fete at the Puyallup Library next week.

I am the author of DB Cooper and the FBI – A Case Study of America’s Only Unsolved Skyjacking, and on Tuesday, August 9, 2016, I will be speaking on DB Cooper as part of their local author series. The conversation will begin at 6:30 pm, and is free.

The Mountain News - WA
labda nikuombe acha malumbano ya kitoto mwache The Bold aendelee kuburudisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…