Dah! Afande Mwita Kaniokoa kwa Waifu

Dah! Afande Mwita Kaniokoa kwa Waifu

tutafikatu

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2011
Posts
3,327
Reaction score
4,624
Jana nimepiga vyombo balaa. Pembeni nilikuwa na kinikia la UDSM. Linasoma Masters pale COET na limepanga mtaa wa pili jirani na nyumba yangu. Siku moja nililichanganya nikalinunulia panti kwa Mama Tarimo Boutique, lakini mama Tarimo akaja kuleta soo kwa kumuuliza Bi. Mkubwa kama chupi zilimtosha. Na mimi nilivyo mwendawazimu Bibi Mkubwa alipokuja kwa hasira kuniuliza kulikoni nilipopeleka chupi, wala sikumchelewesha kujifanya nimezisahau kwenye gari. Mama Junior alitafuta chupi hadi kwenye chesisi!!!! Alipozikosa akajua waosha gari watakuwa walizitua.

Sasa leo saa 12 asbh nimeamka. Mikono ya Amina iko kifuani mwangu. Ebwanae, pamoja na ukora wangu sijawahi lala nje ya kitanda changu. Najua Bi. Mkubwa atakuwa amepiga simu hadi kwa wakwe zake.

Uzuri nikamkumbuka Afande Mwita. Huyu OCD nimetoka naye mbali sana. Nilijua hatoniangusha. Nikampa mkanda mzima. Mwita akanitia ndani. Akampigia simu Bi Mkubwa aje Polisi kunichukua. Ati kanikuta kituoni nimetiwa ndani, baada ya msako uliofanywa Bar jana usiku. Yaani Agness na maneno yote yalimwisha. Akawa ananionea huruma tu. Ati hawa Polisi kwanini wawabebe bar nzima hata wikiendi wakati watu mpo kwenye starehe zenu. Hawajui wewe ni TISS?

Basi mimi nikiwa mpole kabisa nikamshika mkono Bi. Mkubwa. Shhhh. Hayo mambo ya TISS ni yangu na wewe. Hizo ni ajali za kawaida za kwenye masanga.
 
hahahhahha! huyo afande akili kubwa, kuna afande mwaka majuzi akili ndogo cheo kikubwa demu tumekosana kamfata kamjaza upepo nae bila kufikiria kanitwangia simu si nkamtukana kinyama.

wacha anitie ndani siku 3, kisa mwanamke pumbavu sana
 
Back
Top Bottom