Dakika ambayo goli limefungwa, Azam TV jirekebisheni kwenye hili

goodwillmaths

Member
Joined
Mar 3, 2017
Posts
22
Reaction score
19
Mfano,TV ya Azam inaonesha penalty ya Mbao imepigwa 26:18. Hiyo inahesabika ni dakika ya 27 (27')
Namba unayoiona unaongeza 1
Nyinyi mmeandika 26'.

Pia nimeona kwenye magoli mengi tu muda wa goli mnaandika mnaouona. Mf 34:36 nyie mnaandika 34 badala ya 35.

Angalieni hata wenzenu wa Ulaya kwenye UEFA kanuni ni unaongeza 1 .(ingawaje goal la Messi la kwanza dhidi ya PSV Supersport walikosea ,30:59 wao wakasema 32,la Dembele 73:58 wao wakasema 75. Ila hata Live score,flashscore,soccer24,futbol24 walikosea. Ila wao walihisi ni DKK ilikuwa imeingia nyingine 31:01 na 74:01. Muda sahisi ulikuwa 31 na 74.) BBC,Skysports websites walirecord kwa usahihi.


MOJA YA MADHARA MADOGO

inawezatokea siku Simba na Yanga goal likaingia 35:46. Nyie mkasema 35 wakati usahihi ni 36. Watu wakabishana(wakawekeana dau) juu ya ni muda gani goal limeingia atakayewafuatisha ataliwa kwa nyie kutokuwa makini. Huku na huku MTU kapigwa kisu ,Mara mashada yakahusika(kwa ndugu zangu wakristo).

OUT OF TOPIC
Wa kubet watanielewa vizuri . goal likifungwa 26:58 hiyo ni 27' . uliyebet 28+ umechana mkeka ila kutokana na livescore kutokuwa makini watasema 28'. utaenda kusumbua betting shops.

Azam TV zingatieni ushauri huo. Ila fanyeni ushauri mjiridhishe
 
Nimeona wanaandika 96' badala ya kuandika 90+6 yaani utadhani hiyo mechi inachezwa dakika 120' ....au unakuta half time bado but extra time wanaandika 46' au 47' badala ya 45+2 au 45+3'....hawa Azam Washamba mno
 
Nimeona wanaandika 96' badala ya kuandika 90+6 yaani utadhani hiyo mechi inachezwa dakika 120' ....au unakuta half time bado but extra time wanaandika 46' au 47' badala ya 45+2 au 45+3'....hawa Azam Washamba mno
Wanatakiwa wajirekebishe. Mdogo mdogo watakuwa bora
 
Wazee wa mikeka utawajua tu.
 
Azam TV ball position hata timu zicheze vipi 44 kwa 56. Siku hizi sina time na takwimu za mechi.
 
Unakuta mtu mtangazaji wa mpira huku yeye mwenyewe hana interest na mpira sidhani kama hayo mambo atayajulia wapi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…