kwetunikwetu lazima tukubali ukweli wa kuwa watanzania (hasa wenye viji pesa) hatuko healthy.
mtu anakula zake nyama choma za kufa mtu anashushia na beer zake kadhaa na siku nzima alikuwa amekaa ofisini. Asubuhi kuna wanaokunywa supu ya nyama pia ( kwa vile ana hela), mboga mboga hakumbuki kala lini, he is overweight kukaribia obese pengine na hajijui.
tunahitaji kubadili namna ya tunavyokula ....................
Wamasai, Wahadzabe etc wanakula nyama ya kuchoma miaka nenda rudi na bado hawalalamiki kuhusu gonjwa la gout. Tatizo linatokana na watu kutofanya mazoezi.
vegeterianism..............??!!!
Wamasai wanakunywa sana dawa mza asili, thats why huwezi sikia mmasai anaumwa gout
sio mtu aache kula nyama kabisa ........lakini tupunguze na pia tufanye mazoezi.
Tujenge mazoea ya kula samaki hasa fresh fish.Maharage yajulikana kama Mboga ya Taifa maana mashule yoooote, magereza, na hata mahospitali ya G ndo mboga yao. si tulikuwa twala maharage mara saba kwa wiki shuleni, ikibadilishwa basi ni mapande ya kabichi ya kwa taaabu sana "SUPU" sio nyama ni supu maana ikiwa siku ya nyama (ambayo ni mara moja kwa mwezi ama kwa temu) ni kasheshe, labda tatizo kubwa lilikuwa ni kuona usiku maana kuna jamaa ilikuwa ikifika jioni tu basi inabidi umshike mkono kumrejesha bwenini, ila sijawai kuona ama kusikia magonjwa ya miguu.
Huyu Dr ataka kutuulia mboga zetu, maana uswazi mbali ya sukuma wiki ni nyama na maharage tu ndo zinatamba.
Inategemea umeyala kwa muda gani na kumbuka pia na suala la mazoezi, mashuleni haina shida sana watu hufanya mazoezi, fikiria sasa anayekula vyakula hivyo ni mtu mzima na si mtu wa mazoezi, tuzingatie ushauri wa wataalamu wetu.That being the case vijana waliopitia boarding wote wangekuwa na hayo matatizo bse maharage nod ilikuwa daily