Daktari jela kwa kumpa sumu mkewe kusudi ili mimba itoke

Daktari jela kwa kumpa sumu mkewe kusudi ili mimba itoke

DeepPond

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2017
Posts
41,728
Reaction score
103,997
Ilitokea Ohio, marekani, 2000

KWA KIFUPI Ni kwamba,
Binti mmoja baada ya kula sana ujana, miaka 33 anaamua kuseto kwa kutafuta mume wa ndoto zake afanye maisha.

Vigezo vyake Ni awe mrefu, handsome na professional na anabahatika kupata mchumba daktari na penz lao Moto Moto penzi linaingia changamoto baada ya binti kupata ujauzito wake wa kwanza kabla ya kufunga ndoa yao rasmi.

Ujauzito ule unahatarisha maisha ya binti baada ya mwanaume kurudiana na ex wake wanaodhamiria Mimba ile itoke kwa mume kumpatia binti, sumu ya taratibu itakayotoa ujauzito ule bila mtu yoyote yule kushtukia kama Kuna faulo play imefanyika.

images-1357.jpeg
 
NI HIVI...
Ofisi za RED CROSS chini ya Wizara ya mambo ya ndani, jeshi la uokoaji pamoja na Hospital ya rufaa Chini ya wizaraya afya vinatizamana ila (zinatenganishwa na barabara) , na wafanyakaz wa taasisi zote mbili wanashea mgahawa mmoja kwa ajili ya chai na vyakula mbalimbali.

Misheli akiwa Ni binti miaka 33 na mtumishi wa kitengo Cha Huduma ya kwanza, akajikuta anateta Jambo na shoga yake Cathe ambae Ni nesi wa hospital ya rufaa opposite na anakofanyia Kazi.

Misheli Anamwambia Cathe kwamba kwa umri wake huu miaka 33 sasa anahitaji kuseto kupata mwanaume handsome, professional na anaeeleweka wa kuzaa nae na ikiwezekana kujenga nae familia.

Cathe anampa tip shoga yake kwamba pale kazin kwao Kuna dokta kwa Sasa Yuko singo na anazo sifa zote alizotaja (Na akamwonesha picha yake) . Alikua anadate na nesi mwenzao pale ila nesi mwenyewe mapepe sn haeleweki, alishamfumania na wakaachana, kwaiyo Kama unaweza kuichukua Kama opportunity, Basi date nae serious Muoane.

Cathe akasisitiza kama kamuelewa Basi afanye mpango awakutanishe, misheli atajiongeza mwenyewe wawe pamoja kwenye Mahusiano. Misheli kafurahi na kakubali kukutanishwa na dokta.

Na hapo ndipo balaa linakoanzia..

****************
 
Walipokutanishwa TU mgahawani,
ilkua Ni Kama love at first sight, dokta nae alijikuta kamuelewa Sana misheli, na wanaume tusivokawia, dokta kaomba namba chap ya misheli, misheli akampatia, wakatongozana kwenye simu na kisha kuanza Mahusiano rasmi.

Mahusiano yao yalikua Moto Moto na hawakujificha maana mida la chai au lunch pale mgahawani walikua pamoja,kazini walitembeleana na wafanyakaz wote wa taasisi zote mbili wakajua kweli dokta na red Cross wana Mahusiano serious.

Hawakuwia Sana Misheli akanasa ujauzito wa Dokta, ilikua Ni habari njema Sana kwa wote wawili na wakaanza kujadili mipango ya kuishi pamoja, kufunga ndoa na namna ya kumpokea mtoto ajaye.

Misheli akamwambia dokta,Kwanini wasianze kuishi pamoja maana tayar tumbon kabeba kiumbe chake. Dokta Akasema MDA wa kuish pamoja Bado ukzingatia Hatuna makazi mazuri ya kueleweka kuish km family maana naishi Kota za hospital na Wewe unaishi uswahilini sana,tujenge kwanza.

Misheli akamwambia dokta kwann tusijichange tukope pesa benk tukanunue nyumba kubwa iliyokamilika ili tuish pamoja kuliko kuishi hivi mbali mbali tukisubir kujenga. Dokta Akasema tuvute subira kwanza.

Ila dokta Ni Kama Kuna kitu hakiko sawa akilin mwake....

****************
 
Misheli baada ya kuona Kama dokta anajishauri sana, misheli akaenda benk kakopa pesa na kanunua nyumba ya familia iliyokamilika. Akamwambia mpenz wake dokta wahamie kwenye nyumba aliyonunua.

Dokta kamsifu ila kasema atahamia pale rasmi baada ya kufunga ndoa, waanze na mipango ya ndoa kwanza maana mimba inaendelea kukua. Sio vizur unavaa shela na tumbo limevimba linaonekana. Misheli kakubali.

Mipango ya ndoa imeenda vizur, baadae dokta kabadilika eti Hataki. Showoff's anapendekeza watafunga ndoa ya kiserikali kwa sherehe fupi Sana, jamaa na marafiki wa karibu watataarifiwa kuhudhuria . Misheli kasema haina shida.

Baadae Tena dokta akabadilika,akamwambia misheli kwamba wanatakiwa kusitisha kwanza mipango yao ya ndoa. Kuna vitu anahisi haviko sawa.Misheli anastaajabu, Ni vitu gani haviko sawa!

Dokta akasema hajawahi kufikiria kufunga ndoa bila uwepo wa wazazi wake na kwao wote ufunga ndoa za kidini sio za kiserikali. Kwaiyo havutiwi kabisa kufunga ndoa ya kiserikali bila uwepo wa ndugu zake.

Misheli akauliza Sasa itakuaje, dokta akasema wahairishe kwanza mpaka ajifungue, Kisha watafunga ndoa ya kidini maana kwa dini Yao Ni mwiko mjamzito kufungishwa ndoa. Misheli anaona haina budi kukubaliana na mpenz wake.

Ila moyoni misheli anahisi mpenz wake kabadilika sn,Kuna kitu hakiko sawa...

****************
 
Siku zinaenda mimba inafika miez 3 anaanza kuskia tetesi dokta karudiana na ex wake yule nesi mapepe. Misheli anajipa Muda kuchunguza tetesi hizo. Kamfata Cathe, kasema yenye mwnyw kaskia ila Hana uhakika. Wachunguze kwanza.

Gafla siku misheli anakuta call history kwenye simu ya Dokta alimpigia ex wake wakaongea Zaid ya dkk 50. Dokta anajitetea hakuna kibaya chochote walichoongea, anaempenda Ni yeye TU. Mawasiliano Yao Ni mambo ya Kazi TU. Misheli anaamua kukaa kimya.

Sasa kama ilivokua utaratibu, siku za Kazi kila mtu anaishi kwake isipokua jumamosi na jumapili tu dokta alipaswa kuja kushinda na kulala nyumbani kwa misheli kwnyw ile nyumba mpya aliyonunua.

Dokta anafika Kama kawaida, ila ghafla saa 1 jioni anaaga anaenda shift hatoweza kulala pale kwa leo, kapigiwa simu ya dharula. Baada TU ya dokta kuondoka Misheli machale yanamcheza Sana anampigia shoga yake nesi Cathe kuthibitisha taarifa hizo.

Cathe anamwambia hajajua na Yuko kazin MDA huu, Ila alichokiona Ni gari ya dokta ilikuja ikaishia parking, afu nesi mapepe kaondoka na kwenda kupanda ile gari. Ana wasiwasi Hawa wawili watakua pamoja MDA huu.

Basi misheli anaamua kumpigia simu dokta na kumuuliza Kama kafika salama kazini, dokta anaitikia kwamba kweli kafika salama na anaendelea na Kazi. Misheli anaamua Kumrudia shoga Yake Cathe, anataarifiwa huenda wameenda nyumbani kwa nesi mapepe, ndo upenda kukutania.

Basi misheli anaomba kuelekezwa na baada ya kupajua kweli misheli anaamua kuelekea nyumbani kwa nesi mapepe, kufanya fumanizi...
 
Kufika anaona gari ya dokta imepaki nje, anajua moja kwa Moja dokta yumo humu ndani. Anasukuma mlango kumbe uko wazi, anazama. Ndani moja kwa moja chumban na kuwakuta dokta na nesi mapepe wako uchi wa mnyama wanafanya mapenzi.

Wanatahamaki na misheli anamuuliza dokta "uyu uliyenae Ni Nani", dokta anamkana na kumuuliza "kwani wee unaeuliza ni Kama Nani, mbona sikujui, unaharibu starehe za Watu" Nesi mapepe anakazia kua aondoke pale haraka sana kabla hajaita polisi. Nesi analia na kuondoka kwa aibu Sana eneo Lile.

Baada ya kufika nyumbani, anampigia dada Yake na shoga Yake Cathe kuwaeleza kilichomkuta kwenye fumanizi lile la mchumba wake dokta, Misheli anafikia uamuzi wa kuachana rasmi na dokta na kufuta kila kumbukumbu zote zinazomhusu dokta maishani mwake.

Hawajakaa siku mbili dokta anamtafuta misheli na kuomba msamaha na kuomba warudiane, alikua Ni shetani yule, Hata haelewi Nini kilitokea siku ile, anajuta sana, nesi yule anahisi Kuna namna alimroga na anaahidi na kuapa hatorudia Tena.

Misheli anamfikishia taarifa zile dada Yake na shoga Yake Cathe. Wote wanamshauri ausikilize Moyo wake tu, Kama bado anampenda dokta,haina shida arudiane nae TU, atabadilika. Wanaume kuchepuka kawaida. Misheli anakubali kurudiana na dokta.

Na hili ndo linakua kosa lake kubwa sana maishani.....

****************
 
Siku ya kurudiana kwao, dokta anamwambia misheli kamwandalia Dinner night special kwa ajili ya msamaha wao na kuanza penzi lao upya, misheli anajiandaa kwa mtoko wa Nguvu na wanakutana hotel ya ufukweni specila kwa ajili ya dinner za wapendanao

Misheli kafika kamkuta dokta. Na kila. Kitu kishaandaliwa mezani, dokta kakaa anamsubiri na Chupa ya shampein. Dokta anampokea misheli kwa goti la unyenyekevu, anajieleza mengi, misheli anakubali kumsamehe,wanakiss na wanaanza kunywa na kulishana. Penzi limekua jipya.

Katkat ya dinner, misheli anabanwa tumbo na kuomba kwenda toilet. Tumbo linamuuma Sana mpk anaomba panado kwa mhudumu anameza anajiskia nafuu. Dokta anasema itakua Hali ya kawaida huenda ana allergies na shampein. Wanaamua kusitisha ile dinner na misheli anarudishwa nyumban kwake tumbo likimuuma sana.

Usiku ule dokta Akasema hatoenda kulala kwake kota, atalala pale Pale kuangalia afya ya mpnz wake. Usiku ule wamelala vizuri na kulipokucha dokta kaamka mapema Sana kanunua nyama kaenda jikoni kumwandalia supu nzito mpnz wake misheli.

Misheli anaamshwa anywe supu, ila baada ya mafunda kadhaa ya supu na vipande vya nyama anajikuta tumbo linamnyonga Tena na kichefuchefu Sana, anaenda chooni kutapika, akitapika sana ghafla anaona Kama damu kama anablidi chini ya mapaja. Yake.

Moyo unamwenda mbio anawaza nn kimetokea...

****************
 
Anamuita dokta aje kuona, dokta anafka na kumwambia kwa mimba changa Ni kawaida Sana kublidi Kdg, Wala asiwe na wasiwasi, kesho wataenda hospital wakamchek tatizo kwny ultrasound litakua Nini. Misheli anakubali Kisha anaenda kupumzika.

Kulipokucha mapema sana dokta akaaga anatangulia kazini kwake, ila atakapojiskia nafuu atampigia amfate na gar wakamchek tatizo Ni Nini kwenye ultrasound. Misheli mida ya saa 4 asbh akampigia dokta amfate hakupokea simu, Basi akaona sio kesi huenda yuko bize Sana.

Akampigia dada ake na kumweleza anavojiskia na alikofikia. Sista kamshauri ampigie dokta wa familia Yao akamuangalie, dokta wa familia akafika pale na kumchukua na kwenda kumpima hospitalini kwake. Baada ya vipimo ikaonekana Mtoto Yuko sawa kabisa tumboni na hamna tatzo lolote lile. Dokta wa familia akamuuliza kwani ule Ni ujauzito wake wa ngapi, misheli akasema Ni ujauzito wa kwanza.

Dokta akamwambia damu kdg kutoka na tumbo kunyonga Ni kawaida sana kwa wanaopata ujauzito wa kwanza wakiwa na miaka 30 Na zaidi. Wee una miaka 33, kitaalam mifupa ishakomaa sana , kwaiyo Apo maumivu na damu kidg ni Nyonga inajaribu kujitanua ili kutengeneza nafasi ya Mtoto Wako. Kwaiyo vumilia TU Ni Hali ya mpito. Basi misheli akamwelewa dokta wa familia Yao.

Dokta akashaur kwa Hali Yake hii inabidi apate mtu wa kua nae karibu, endapo litatokea lolote Lile. Sio vzur mjamzito na una hali Hii afu unaishi peke yako. Basi misheli akamwomba dada Yake aje aishi kwake awe anamwangalia. Dada Yake Kweli jioni ile ile akafika kwake.

Ujio wa dada nyumbani kwake ndio unakuja kufunua yaliyojificha....

***********************
 
Baada ya dada kufika,
Afya Yake imeendelea vzur sana Hadi wikendi ilipofika, dokta alipokuja kulala kwa misheli Kama kawaida Yao. Dada Yake akaomba ruhusa awaache arudi home maana shemej keshafika,Kuna ishu zake akamalizie, atarudi jumatatu. Wote wakafurahi na kumuaga na kumtakia kila heri sista. Misheli akabaki na dokta nyumbani.

Dokta kaenda kashughulikia kila kitu pale home pamoja na kuandaa dinner jikoni kwa ajili Yao wote wawili. Baada ya kula vijiko kadhaa, misheli anaskia Tena kichefuchefu,tumbo linanyonga Sana, anaenda kutapika chooni.

Hamu ya kula inakata,anabembelezwa sana na mpenz wake amalizie chakula ila tumbo linauma Sana anaamua kwenda chumbani kulala.

Asbh mpenz wake dokta anaamka na anamuandalia chai, ila nayo haimalizi anafika katikati kichefuchefu kikali kinambana anaitapika yote na tumbo linamnyonga Sana. Dokta Hana bundi kumuacha mishel akapumzike

Misheli Akiwa kitandani inabd ampigie dada Yake amweleze jins anavojiskia na ile Hali imemrudia tena, dada Yake mchana anafika nyumban kwake kumjulia Hali mdogo wake.

Sista alipofika TU, dokta anaaga anaenda Kuangalia mpira, dokta anamwomba sista amwangalizie mchumba wake anajiskia vby na kuwaachia Ela ya matumizi.

Dokta alipoondoka TU, sista anapewa mkanda mzima, sista anapata Sana mashaka na ile Hali na kuamua kumwambia ukweli mdg wake Anachokihisi moyoni mwake.

Hapa ndo balaa linapoanzia......

***********************
 
Sista anatilia mashaka Kwamba kwanini kila anapokuepo na shemej (dokta) ndipo yeye anaumwa Hali ile. Kuna kitu anahisi hakiko sawa na kumuuliza Kama ana uhakika 100% na usalama wa kila chakula anachoandaliwa na mpenz wake ili ale?

Misheli akamwambia Hana uhakika maana Mara zote analetewa chakula kilichokamilika, Hata walipokua beach pamoja kwny dinner mara ya kwanza anaumwa alikuta kila kitu kimeshaandaliwa akala, Mara ya pili anaumwa dokta ndie aliefata vinywaji vile kaunta na kumimina kwny glass, Hapa nyumbani pia dokta ndie huandaa mweyewe chakula jikoni.

Basi dada mtu akamshauri misheli aweke mtego wa Siri kujua hili Jambo.

Mtego wenyewe akamwambia misheli akatege camera ya Siri jikoni kwake kinakoandaliwa chakula, Kisha usiku ule dinner itakua ni chapati za maji na soda. Chapati zitapikwa na wao na kua tayari, kisha dokta akirejea, misheli na dada Yake watamwomba dokta kimahaba akawaandalie dinner yao mezani ili waje wale.

Chakula kikishaletwa mezani, kabla ya kuliwa, misheli atajifanya anarud jikoni kufata tomato Kisha akaangalie kwny camera Yao waliyotega jikoni kilichojiri.

Kama kweli Kuna kitu dokta uwa anaweka, Ataonekana. Pia wakibaini kaweka, kile chakula au kinywaji hakitaliwa na kitawekwa pemben Kama ushahidi, Kisha ule ushahidi utapelekwa polisi akashtakiwe.

Kweli mtego wao ukaenda Kama ulivokua, dokta alivoambiwa akaandae dinner alete mezani, Camera ikamnasa dokta akiingia jikoni kuandaa chapati na soda, Kisha kuchukua unga unga mfuko was suruali na kuumiminia kwenye glass mojawapo zile 3 kwenye Trey ya soda.

****************
 
Msosi ulivofika tu mezani,
Misheli akapewa glass yake, sista nae anapewa glass yake na iliyobaki ndo akashika dokta. Misheli palepale machale yakamcheza akaaga anaenda Jikoni uku kashika Ile glass aliyopewa ili kufata tomato.

Kufika jikon brek ya kwanza kwenye camera, Kweli akaona kila kitu kwny camera na kugundua vitu vilimiminwa kwenye glass mojawapo. Akaamua kuchukua Chupa tupu ya soda na kumiminia Ile soda Yake yote toka kwny ile glass aliyoshika.

Chini ya glass akastaajabu unga unga mwingi mweupe umetuama. Akaumimina wote kwny ile Chupa na kuficha. Kisha akachukua soda nyngn mpya kwny friji na kumimina kwny glass mpya na kurud sebleni wakaendelea na dinner yao.

Cha ajabu baada ya kubadilisha kile kinywaji hakujiskia tofauti kabisa na usiku ule na wakalala salama, asbh na mapema dokta kaamka kumuangalia supu misheli anywe. Misheli akamjibu atainywa baadae, hajiskii kunywa saivi. yeye aende TU kazini.

Dokta alivoenda tu kazini kwake, misheli na dada Yake wakaibeba ile supu aliyoandaa dokta pamoja na ile soda ya Jana Yake, na flash yao wakavipeleka polisi kumfungulia mashtaka dokta kwa jaribio la kuwapa sumu.

************
 
Maaskali waliposkia ile story nzima Ya misheli na dada Yake, kitu Cha kwanza wakachukua zile soda na supu vikapimwe wakajiridhishe kweli kama vina sumu ndani au wanahisi TU. Walivopima kwenye maabara ya polisi , majibu yakaja kua hamna sumu yoyote ndani vinywaji vile inayoweza kuua mtu.

Misheli na dada Yake wakabaki na mshangao, Maaskali nao wakawaza mambo mengi Sana na kwa jins walivomfahamu yule dokta, Tena kwa kiumbe ambacho Ni damu yake, ikawa Kama haiwaingii akilini. Wakahisi Hawa wanawake huenda wametengeneza Hii video, wanataka kumchafua TU dokta na kumharibia Kazi Yake.

Wakamuuliza misheli, unahisi Ni Kwanini dokta afanye hivi kwako na wee ndie mchumba wake na kiumbe kilicho tumboni Ni damu yake. Misheli Akasema amerudiana na ex wake, wanamahusiano anahisi sababu itakua hiyo.

Misheli Akamuuliza Kama anaoushahidi, Akasema Hana ila anahisi, Maaskali wakamwambia kesi Yake haina MASHIKO na haiingii akilini, Basi wakaaga na kuondoka ila mioyoni mwao hawajaridhika kabisa.

Walivofika nyumban, dada mtu kaaga anarud kwake na misheli kabaki kwake. Usiku ule dokta akampigia kua watoke out, kweli misheli katoka out na wakaagiza vunywaji na kula, Ila baada TU ya kula, tumbo likanyonga Tena. Misheli kakatisha kula akarudishwa nyumbani, dokta nae. Akaaga anaenda nyumbani kwake.

Baada ya dokta kuondoka, misheli akampigia Tena dada Yake na kumwambia ile Hali imemrudia tena alipotolewa out na dokta Wakala chakula. Dada kashaur tuwaambie Tena polisi. Polisi walipopigiwa wakawaambia kesho asbh waende kituoni, kuna kitu kichunguzwe, Hii sio Hali ya kawaida. Wakasema sawa.

*******************
 
Kesho Yake Walipofika kituoni nao maaskali maswali yakawa mengi, ikabidi wampigie daktari wao khs sumu gani isiyoua ila inayoweza ikasababisha mjamzito damu kutoka chini, tumbo kunyonga na kutapika sana. Dokta akawaambia huenda labda Kama kanywa dawa za kutolea mimba zilizozoeleka Kama misospol,mifepristone n.k

Maaskali wakasema haiwezekani iwe dawa za kutolea mimba maana zile Ni chungu na hawa wamesema sio chungu, ingekua hivyo wangeweza kuzihisi mdomoni.

Dokta akawaelekeza kwa mfamasia mzoefu, ndie mtaalam Sana wa madawa anaweza kuwapa mwangaza zaidi. Mfamasia alivopigiwa simu akawaambia kwa maelezo waliyotoa huenda kweli wamekunywa dawa za kutolea mimba.

Na dawa za kutolea mimba sio lazima ziwe Ni dawa rasmi TU mnazozijua ninyi mitaani, sipo nyingi Sana zisizo rasmi na zinaweza pia kutoa mimba. Na kwa maelezo yenu, huenda dawa yenyewe ikawa kapewa misoprostol brand ya cytotec. Wakauliza kivipi.

Akawaambia kua misoprostol ya cytotec Ni dawa ya unga unga mweupe, inayoyeyuka kwenye maji haraka sana, haina harufu yyt Wala ladha yyt, na inaweza kuchanganywa kwenye chakula au kinywaji chochote na mtu akinywa asihisi tofauti.

Akaongezea kua Kiasili miso-cytotec Ni dawa ya kutibu vidonda vya tumbo ila utumiwa kiharamu pia kutolea mimba, ila mashart Yake ni kwamba haitakiwi kutumiwa na mjamzito, mana inatabia ya kusababisha mimba kutoka.

****************
 
Mfamasia pia akaongezea kua,
Na madaktari huitumia kutolea mimba kwa special cases Sana na kwa dozi ndogo Sana, tena ikiwa njia ni zingine zote zimeshindikana kwa maana kwa dozi kubwa uweza kusababisha mimba kutoka na zipo case nyingi Watu wamepata ugumba kwa Dozi kubwa za misocytotec. Kwaiyo kwa mjamzito ile Ni sumu Sana.

Maaskali wakamwomba mfamasia, kua wanazosampuli kituoni kwao Kama uwezekano upo wasaidiwe kuzipima Kama Zina sumu iyo aliyoisema. Mfamasia kawakubalia na sampuni zile zikapelekwa maabara ya ya madawa ili kupimwa.

Majibu yalivorudi, mfamasia yule kawapigia maaskali na kuwaambia sampuli zote walizopeleka (supu na soda) Zina kiwango kikubwa Sana Cha miso-cytotec, hivyo Kama alikua anapewa mwanamke Basi lengo lilikua kutoa ile mimba,kuua kile kiumbe tumboni au ikizidi uweza kumsabishia ugumba wa milele.

Pia Mfamasia akashaur hatua za kisheria zichukuliwe haraka sana na mjamzito aanze matibabu haraka ya antidote ili kuoindoa sumu ile mwilini mwa mjamzito yule. Maaskali wakasema wamemwelewa.

Maaskali walivokaa Tena kutafakari bado ikawa haiwaingii akilini dokta akaue Mtoto wake mwnyw na kumsababishia ugumba mkewe mtarajiwa. Machale yakahisi Hapa Kuna mtu anatengenezewa kesi.

Basi Wakashauri hiyo flash ya misheli na camera Yao viwekwe pembeni, wakaweke camera Yao wenyewe, kila kitu khs mtego wao wapange Kama walivopanga mwanzo, wao watajificha stoo wakiangalia camera Yao online kwa Siri, Kama kweli Kuna kitu Cha tofauti dokta ataweka, wataingilia Kati wamkamate ready handled na watamuarrest kwa mujibu wa Sheria.

Misheli akakubaliana na maaskali,
Siku ya mtego Kama kawaida, maaskali wakatangulia nyumbani Hadi jikoni, wakatega camera ya Siri ikiwa katika umbo la mdoli juu ya friji ikitizama eneo zima la meza ya maandalizi ya chakula jikoni, Kisha wakaenda kujificha kwenye stoo kusubiria....
 
Dokta kafika Kama kawaida kwa mpenz wake misheli, kaambiwa na mpenz wake akamwandalie kinywaji jikoni. Dokta anafika jikoni, anamimina juice kwenye glass kisha anavuta sumu yake mfukoni na kumiminia kwenye glass. Maaskali kule stoo wanamwona na kumvamia pale pale.

Dokta anatamahaki, maaskali Hawa hapa, wanamwambia uko chini ya ulinzi, unatuhumiwa kwa kumpa sumu mpenz wako, dokta anauliza sumu ipi, maaskali wanamwambia angalia juu ya friji, tuliweka camera yetu ya Siri tumekunasa.

Dokta anajitetea ile haikua sumu alikua anamuwekea virutubisho mkewe ambae Ni mjamzito. Maaskali wanampiga pingu na kuondoka nae.

Walipofika polisi, misheli. Anaitwa ili kuandika maelezo na kufungua kesi, Kisha maaskali wanaenda mahakamani kuomba search warrant ili wakamkague nyumbani kwake na kila kitu chake.

Walipoenda nyumbani kwake, wakakagua computer Yake, wakagundua email alizokua akiwasiliana na ex wake kumweleza jinsi gani hakua na mipango na misheli,kwanz mimba ile iliingia bahati mbaya na alipanga kuitoa.

Na kwenye maelezo yao, ex wake (nesi mapepe) anakazia kua hawez kudate na dokta kwa uhuru mpk ajiridhishe ile mimba ya misheli imetoka kabisa, yeye ndio mwanamke pekee anaepaswa kumzalia watoto. Dokta anasisitiza bado anaendeleza juhudi.

Walimkagua pia kwenye droo ya dressing table yake wakakuta bahasha ya kifungashio chenye lebo ya cytotec,na walipomkagua kwenye buti la gari , zikakutwa Chupa tano za unga wa cytotec na Moja iko nusu.

Dokta Alipoulizwa khs nesi mapepe, wamekuta kwenye simu yake ana mahusiano mengine ya Siri, akakiri kweli ana Mahusiano ya Siri ila hayahusiani na kumpa misheli Sumu ya kutolea mimba,yule Ni Mchepuko TU, anaomba maaskali wamtunzie iyo siri.

Walipomkazia khs email zilizokua kwenye computer yake nyumban wakiongelea kumtoa mimba misheli, dokta akakaa kimya.

Alipoulizwa khs cytotec kukutwa kwny buti la gari lake, akajitetea ana wagonjwa wa nje wanaumwa vidonda vya tumbo,uwa anawapelekea dawa Mara kwa Mara. Alipoulizwa majina Yao wakajiridhishe, akajitetea kua kiapo chake kinamzuia kutoa Siri za wagonjwa wake.

Maaskali wakaona mbali na ushahidi waliokua nao, mahakamani watahitaji shahidi wa kuthibitisha. Basi wakaenda kumuarrest nesi mapepe na kumwonesha email zote alizokua anachat na dokta. Na wakamwambia asipotoa ushirikiano Basi nae atajumuishwa na dokta kwenye mashtaka ya jaribio la kuua kwa sumu kwa kukusudia.

Nesi mapepe akakiri atasema ukweli wote Aya mambo yasifike mbali ataharibikiwa kazi. Maaskali wakamsihi afunguke uku wakaanza kumrekodi kisirisiri. Nesi akaanza kumkaanga dokta.....

**********************
 
Nesi Akafunguka kua mwanzoni dokta walipanga kumuua misheli kwa kumpa insulini aumwe Kisukari taratibu ili Hadi afe, ila aliponasa tu ujauzito, yeye akabadilisha wazo kua wasimuue na Bali Ila mimba yake itoke TU afu aachane nae azae na yeye TU.

Nesi Akasema pia kua zile cytotec hazikutoka hospitalini wanakofanya Kazi maana ingezua maswali, walienda kuzinunua duka la dawa mitaani. Na kweli nesi mapepe akawapeleka maaskali mpk walikonunua. Na kivuli Cha risiti kikaonesha alielipia pesa Ni dokta. Maaskali wakachukua ule ushahidi.

Maaskali waliporud kwadokta na kuwaambia akiri mambo yasifike mbali, dokta akawa anagoma, dokta wakamsikilizisha kdg mahojiano Yao na nesi. Dokta akaishiwa Nguvu na kuomba maji ya kunywa. Baada kunywa maji akaomb kwenda msalani.

Akiwa chumba Cha maaskali, maaskali wakamwambia akatumie choo chao Cha mle ndani ofsini mwao kilichoungana na bafu akiwa kafungwa pingu. Maaskali wakashangaa jamaa mbona Kama anachekewa Sana, wakavunja mlango wanakuta kavua shati kaninginia kajinyonga kwenye nondo ya vent ya choo.

Maaskali vichwa vikauma...
 
Anamuita dokta aje kuona, dokta anafka na kumwambia kwa mimba changa Ni kawaida Sana kublidi Kdg, Wala asiwe na wasiwasi, kesho wataenda hospital wakamchek tatizo kwny ultrasound litakua Nini. Misheli anakubali Kisha anaenda kupumzika.

Kulipokucha mapema sana dokta akaaga anatangulia kazini kwake, ila atakapojiskia nafuu atampigia amfate na gar wakamchek tatizo Ni Nini kwenye ultrasound. Misheli mida ya saa 4 asbh akampigia dokta amfate hakupokea simu, Basi akaona sio kesi huenda yuko bize Sana.

Akampigia dada ake na kumweleza anavojiskia na alikofikia. Sista kamshauri ampigie dokta wa familia Yao akamuangalie, dokta wa familia akafika pale na kumchukua na kwenda kumpima hospitalini kwake. Baada ya vipimo ikaonekana Mtoto Yuko sawa kabisa tumboni na hamna tatzo lolote lile. Dokta wa familia akamuuliza kwani ule Ni ujauzito wake wa ngapi, misheli akasema Ni ujauzito wa kwanza.

Dokta akamwambia damu kdg kutoka na tumbo kunyonga Ni kawaida sana kwa wanaopata ujauzito wa kwanza wakiwa na miaka 30 Na zaidi. Wee una miaka 33, kitaalam mifupa ishakomaa sana , kwaiyo Apo maumivu na damu kidg ni Nyonga inajaribu kujitanua ili kutengeneza nafasi ya Mtoto Wako. Kwaiyo vumilia TU Ni Hali ya mpito. Basi misheli akamwelewa dokta wa familia Yao.

Dokta akashaur kwa Hali Yake hii inabidi apate mtu wa kua nae karibu, endapo litatokea lolote Lile. Sio vzur mjamzito na una hali Hii afu unaishi peke yako. Basi misheli akamwomba dada Yake aje aishi kwake awe anamwangalia. Dada Yake Kweli jioni ile ile akafika kwake.

Ujio wa dada nyumbani kwake ndio unakuja kufunua yaliyojificha....

***********************
Usikawie mkuu
 
Maaskali Wamemtoa pale kumbe alkua bado mzima, kesho Yake wakamuwaisha haraka sana mahakamani. Kule lilisikilizwa wiki 2 kisha akahukumiwa

-miaka 10 jela kwa jaribio la kuua kwa sumu kwa kukusudia bila parole

-Miaka 5 kwa jaribio la kutoa mimba. Kwa kukusudia bila hiari ya mhusika
(marekani utoaji mimba unaruhusiwa, ila kwa hiari ya mhusika)

- Akafungiwa leseni yake ya udaktari miaka 20

NESI MAPEPE yeye akahukumiwa
-miaka 2 jela kwa kushiriki jaribio la kuua na kutoa mimba, ila amesamehewa mwaka 1 atautumikia kifungo Cha nje kwa makubaliano ya ushirikiano ktk kesi pamoja na kua shahidi dhidi ya dokta kwa plea bargain.

-akafungiwa leseni yake ya uuguzi kwa miaka 5

Court ikafungwa, wafungwa wakenda kutumikia jela.

Misheli ameendelea kulea mimba yake chini ya uangalizi maalum na kwa bahati mbaya, ilivofika miez 7 ile mimba ikatoka. Na kwenye hati ikaandikwa "mimba imetoka sababu ya wingi wa sumu ya cytotec kwenye kizazi"

Ikabidi Tena waendesha mashtaka Wa serikali wawarudishe Tena mahakamani toka jela, dokta na nesi mapepe waje kusomewa mashtaka Yao mapya na wahukumiwe upya kwa Kushiriki na kuitoa mimba ya misheli.

Wakasomewa tena mashtaka Yao na hawakua na lakujitetea zaidi ya kukiri, hakimu akagonga nyundo na wakaongezewa miaka 5 kila mmoja kwenye vifungo vyao vya awali.

THE END*
Credit:
-court Casefiles: Michelle Baker vs doctor mainad
- Documentary ya Forensic file "bitter pill to swallow"
 
Back
Top Bottom