stephot
JF-Expert Member
- Mar 1, 2012
- 17,216
- 26,225
Jamani wadau naombeni msaada wenu,mama yangu umri umesogea kidogo about 75Yrs old,amaepata tatizo kwenye jicho lake la kushoto yapata miezi minne (4) sasa,lilianza kupoteze uwezo wa kuona mpaka sasa anaona kwa shida yaani anaona kitu kama ukungu,sasa tuliamaua kumpeleka CCBRT wamesema kuwa anahitajika kufanyiwa operasheni tatizo mara zote appointment yake inapofika pressure inapanda kwahiyo wamekuwa wakiahirisha,niliwahi kusikia kuwa kuna wataalamu wanaotibu matatizo ya Macho bila ya kufanyia Operasheni,mwenye kujua hawa wataalamu tafadhali anijuze niweze kumsaidia mama yangu.