Daktari ni kama sijamuelewa hivi

Benokolongokonongose

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2012
Posts
213
Reaction score
52
Habari zenu wakuu katika afya! Rafiki yangu amekuwa na shida ya kutopata mtoto yapata miaka miwili tangu andoeke(afunge ndoa). Alivyoenda kwa daktari akampima na akasema hana tatizo lolote isipokuwa nguo anazovaa zimemsababishia akose mtoto. Nguo hizi ni: Skin tights(vibana ngozi),suruali nk. Hoja ya daktari ni kuwa sehemu za siri hazihitaji kupata joto kali au kubanwa. Ni kama nimeachwa kwenye mataa. Kama ukweli ni huu si inafaa kuongezwa kwenye vyanzo vya uzazi wa mpango? Nawasilisha. Wenu Benokolongokonongose.
 
(Ujumbe kwa rafiki)
Nenda kwa maktari wengine, labda useme unaweza fika miji gani au upo karibu nayo watu wakutajie majina ya gynaecologists au clinic za gynaecology.

Ila msiache kumuomba Mungu, na asifikirie wazo la kuzaa ajisahaulishe na mume asilikumbushe. Jambo hilo kuwekwa akilini mwa mke na mume kuliongelea sana linabadili mengi mwilini na kwa asilimia kubwa ya watu hainasi.
Wakienda kuchekiwa wasirudi kushinda wanaongelea kuji stress etc
Esp mke lazima asijawe na mawazo hayo kila sekunde. Wapeane moyo na wafurahie maisha na kusubiri muda wao. ( Hii ni kama hawana matatizo kabisa kiafya juu ya hili)
 
Kutopata mtoto kuna sababu nyingi sana hili la nguo ni kama dr kachomekea tu japo si vizuri kuvaa vibana ngozi hata kama huhitaji mtoto
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…