DOKEZO Daladala za Arusha zinapandisha nauli, zinakatisha ruti ikifika Saa Moja usiku, LATRA mko wapi?

DOKEZO Daladala za Arusha zinapandisha nauli, zinakatisha ruti ikifika Saa Moja usiku, LATRA mko wapi?

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Mimi ni Mkazi wa Arusha, nimekuwa Mdau wa muda mrefu wa platform yetu hii ya JamiiForums kwa muda mrefu, kero yangu mimi ni kuhusu Daladala kukatisha ruti na kuongeza nauli kinyume cha Sheria.

Huku Arusha na vitongoji vyake tuna changamoto ya usafiri hasa ikifika mida ya Saa moja usiku na kuendelea, vyombo vya usafiri hasa hizi ambazo kwa Dar mnaziida Daladala, wenzetu hawa wanakatisha ruti na wengi wanaongeza nauli zaidi ya ile ya halali.

Ombi langu mamlaka husika washughulikie hiyo kero na pia Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) waweke utaratibu kuwe na tiketI kwenye hizi daladala, kwani najiuliza wao hawaoni hiki kinachoendelea au wanaona na wameamua kuwa kimya watuache tunateseka?
 
Kwa kweli hasa watu wanaoishi arusha-himo road na vitongoji vyake na maanisha USA river ikifika jioni inabidi waandae elfu moja. muda mwingine Hadi elfu moja na Mia tano wakati nauli ya halali ni Mia Saba. Latra waingilie Kati Hilo watu pakusemea hawana.
 
Kati ya taasisi mbovu mbovu katka kusimamia maelekezo yake, ni hawa pia. Kazi kutangaza nauli mpya tu
 
Back
Top Bottom