KERO Daladala za Mbezi-Kawe zisiwaache abiria mbali na Kituo cha Daladala cha Kawe

KERO Daladala za Mbezi-Kawe zisiwaache abiria mbali na Kituo cha Daladala cha Kawe

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Kuna daladala huwa zinazingua sana. Yaani unaenda mahali lakini hawakufikishi kama inavyopaswa. Kwa mfano, unaweza kuwa unaenda mahali, lakini wakiona mmebaki watu watano ndani ya gari wanageukia mbali na kituo, au wakati mwingine wanakufaulisha kwenye gari lingine lililojaa na nafasi ya kukaa unakosa.

Imagine unajikuta umesimama wakati uliwahi mapema kituoni ili upate siti ya kukaa. Umetoka home umeng'arisha kiatu fresh ili ufike ofisini ukiwa vizuri then mtu anakutembeza kwenye vumbi unatokwa na jasho. Ukifika unanukia ubeberu fulani hivi unaanza kukwepa kukumbatiana na watu wazuri.

Ubaya ni kwamba unashitukizwa tu kuwa "Abiria, tumefika mwisho!" then kondakta anakuchekea tu kana kwamba upo tayari kushiriki naye ufedhuli huo.

Kuna wakati bajeti ya boda ni buku tu ila daladala akikushusha mbali na kituo gharama inaweza kufika buku-jero au mbili kabisa. Inakera!

Daladala za Mbezi-Kawe ziache ujinga huu. Kuna daladala za ruti hii huwa ni mwiko kwao kuingia stendi. Wanageukia mita kama 200 hivi kabla ya kufika kituoni ili wasipange foleni. Huu ni ukatili. Nauli zetu zinakuwa hazijaisha. Hapohapo wanapokuacha, ukigeuza na gari hadi kituoni wakati wa jioni wanakuchaji jero.

Sema nini, tusake hela tununue magari, Wakuu.

#SogaZaPedestrian
 
Kuna daladala huwa zinazingua sana. Yaani unaenda mahali lakini hawakufikishi kama inavyopaswa.
Hadi hili unataka serikali ya CCM ikusaidie kusolve?
Kwanini msigome kushuka abiria wote? Mmoja atoke akamuite traffic na nauli mrudishiwe kutokomeza huo upuuzi
 
Watanzania tuna shida. Hata konda na dereva hatuwezi kuwalazimisha watufikishe mwisho wa safari kama TLB waliyopewa
 
Wanaume wa Dar Mmezidi kudeka [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hadi hili unataka serikali ya CCM ikusaidie kusolve?
Kwanini msigome kushuka abiria wote? Mmoja atoke akamuite traffic na nauli mrudishiwe kutokomeza huo upuuzi
Nadhani hili SADC ndiyo wanaliweza. 😀

On a serious note, mimi nilipendekeza tufanye hivyo, wenzangu wakasema hawataki malumbano wakasepa.
 
Mimi juzi nilishushwa boma huku mtaani badala ya machinga complex tulikua wengi, nilikua nimegoma kushuka nikajikuta nimebaki peke yangu
Wengine wameshuka huku wanalalamika nikawa sina budi
Natembea huku nimenuna mbele wanaume wawili na wao walishuka wanatembea huku wanamtukana dereva niliwaona wapuuzi tu! Watanzania tunajua kulalamika ila matendo 0
Pole sana aisee. Ndiyo watu tulio nao. Wakati mimi napendekeza tugome sikuwa najiwaza mimi, nilikua namuonea huruma mama mmoja mgonjwa aliyekuwa anaenda kupata huduma kwa Mwamposa. Nadhani mwanae alimkokota hadi wakafika. Mimi nilitimua vumbi hadi mgahawani kwangu.
 
Back
Top Bottom