mkulimamiwa
Member
- Mar 4, 2025
- 39
- 36
Sifahamu shida ni nini
Vimikatiko vya umeme visivyoeleweka vimekuwa vingi kiasi cha kujiuliza maswali iwapo tayari Tanesco wameshaanza kutoa dozi ya mgao wa umeme
Wakati matamko ya viongozi mbalimbali yakitolewa ya kutokuwepo mgao wala usumbufu wowote wa umeme hata kwa misimu mitatu ya ukame nchini,
Hali inayojitokeza sasa ni ya sintofahamu na tunaanza kujiuliza Je, tuamini lipi kati ya hayo mawili, tuwaamini Tanesco kwamba, nchi inahaki ya kuwa na mikayoko ya umeme mara kwa mara kwa sababu pengine ya ukweli walionao wao, au tuendelee kuamini matamko ya viongozi wetu?
Tanesco ndio wanao kaa na jiko, ndio wapishi, wanajua fika kile kilichoko kwenye vyanzo vyetu vya umeme, au tu Tanesco wanataka kuwachonganisha viongozi wetu na wananchi waliowapa dhamana ya kuongoza nchi?
Watanzania ni watu waliozoea kuongopewa na siyo kuambiwa ukweli, ukisikiliza sababu nyingi za Tanesco za kwa nini umeme unakatika, wao watasema, wapi kwenye matengenezo sjui ya nguzo na nyaya...
Kama sababu ni hiyo, Je, ni lini watakamilisha matengenezo na kuacha umeme ukae hata mwaka bila kukatika?
Ni lini tutafikia huko? Mawazo yangu, huu ulishakuwa kama mchezo tu ilihali ukweli wanaujua, na ndiyo maana kuna wakati akili za watanzania, mambo haya yanapokuwa ya kujirudia rudia sana, huwa tunaamini ni hali za mgao tu wa umeme wala hakuna lingine
Ni vyema tuwe tu wakweli, mnachosha sana Tanesco
Vimikatiko vya umeme visivyoeleweka vimekuwa vingi kiasi cha kujiuliza maswali iwapo tayari Tanesco wameshaanza kutoa dozi ya mgao wa umeme
Wakati matamko ya viongozi mbalimbali yakitolewa ya kutokuwepo mgao wala usumbufu wowote wa umeme hata kwa misimu mitatu ya ukame nchini,
Hali inayojitokeza sasa ni ya sintofahamu na tunaanza kujiuliza Je, tuamini lipi kati ya hayo mawili, tuwaamini Tanesco kwamba, nchi inahaki ya kuwa na mikayoko ya umeme mara kwa mara kwa sababu pengine ya ukweli walionao wao, au tuendelee kuamini matamko ya viongozi wetu?
Tanesco ndio wanao kaa na jiko, ndio wapishi, wanajua fika kile kilichoko kwenye vyanzo vyetu vya umeme, au tu Tanesco wanataka kuwachonganisha viongozi wetu na wananchi waliowapa dhamana ya kuongoza nchi?
Watanzania ni watu waliozoea kuongopewa na siyo kuambiwa ukweli, ukisikiliza sababu nyingi za Tanesco za kwa nini umeme unakatika, wao watasema, wapi kwenye matengenezo sjui ya nguzo na nyaya...
Kama sababu ni hiyo, Je, ni lini watakamilisha matengenezo na kuacha umeme ukae hata mwaka bila kukatika?
Ni lini tutafikia huko? Mawazo yangu, huu ulishakuwa kama mchezo tu ilihali ukweli wanaujua, na ndiyo maana kuna wakati akili za watanzania, mambo haya yanapokuwa ya kujirudia rudia sana, huwa tunaamini ni hali za mgao tu wa umeme wala hakuna lingine
Ni vyema tuwe tu wakweli, mnachosha sana Tanesco