Elections 2010 Dalili ya ushindi wa kushindo kwa chadema imekwishaonekana


Mkuu ili hoja yako ieleweke siyo lazima utumie lugha kali kama ilivyo kwenye sentensi yako ya mwisho.

Hapo kwenye uwekezaji ndipo ambapo ninaomba ufafanue, mmewekeza nini? The only way ya kuwekeza kwa watu wa chini/vijijini ni kwa kuboresha bei za mazao yao, hapo ni total failure. Kila kona bei ya mazao ni mbaya kuliko. Kuanzia kahawa, tumbaku, pamba, mpaka mahindi. Bado miundombinu ya vijijini ni zero, maji zero, afya zero, elimu ndo usiseme kabisaaaa. Hebu niambie huo uwekezaji unaousema ni upi?

Usiwatukane wakazi wa vijijini, sema ukweli kwamba mnatumia ujinga wao au kutojua kwao haki zao na ndio maana mnapata kura. Zikitokea NGOs kama HakiElimu zikaanza kuelimisha jamii serikali inakuja juu. Hata Zimbabwe ilikuwa hivyo hivyo, ushindi wa Mugabe ulikuwa unatoka vijijini, iko siku waliamka na kujua haki zao. Hata Tanzania ya leo mwamko upo, taratibu mtaondoka tu, maana wananchi wanaamka na kuelewa haki zao na kujua adui yao wa kweli ni nani.

Mwaka 2005 mlipeta kilaini, mwaka huu hali ni ngumu ndio maana mmeanza kutoa hata ahadi ambazo hazitekelezeki na kusema uongo juu. Mojawapo ya mambo ambayo mmesema uongo ni pamoja na JK kusema amepandisha mishahara halafu waziri wake anasema HAPANA, wote wako ndani ya serikali moja. Mnaahidi kugawia watu ardhi na kumbe mlishauza kwa wawekezaji, Kigamboni wamewabana mseme agenda yenu, JK kaingia mitini anasema ni jukumu la diwani, yaani maamuzi lifanye baraza la mawaziri, halafu umsukumie diwani? Hata aibu hana! Mmewadanganya wakulima wa mahindi wa Mby kwamba wakauze mahindi yao SGR na kumbe hakuna hela. Mamlaka ya Korosho baada ya kuona cheche za Prof Lipumba juzi wamejifanya kutangaza kufungua msimu wa kununua korosho, ajabu ni kwamba hawana hata senti wanategemewa wakanunue mali kauli!

Huo ndio uwekezaji wenu kwa kutumia ujinga wa watu wa chini kabisa ambao umewaelezea vyema kabisa kwamba hawajui hata computer, sema kabisa kwamba hawajui hata kusoma, maana ujinga wao ndio mtaji wenu! So sad ... na unasema kwa ujasiri kabisa kwamba mmewekeza kwenye ujinga wao!
 
Ndugu zangu, Hii siyo kificho tena. Kuna vituko vingi Dr. Slaa anafanyiwa ili mradi aonekane hana sifa. Lakini hata hao wanaotaka jamii ione kuwa hana sifa, wao wenyewe wanofanya mipango hiyo, wanajua kuwa Dr. Slaa ni moto wa kuotea mbali kwa habari ya sera na uongozi shupavu.

Jakaya mpaka sasa ahadi alizotoa 2005 hazikukamilika, ahadi anazotoa leo hazitekelezeki wala hazina manufaa kwa wananchi wa kawaida. mfano, JK amewaahidi wananchi wa Kigoma kuwatengenezea uwanja wa ndege wa Kimataifa, wananchi wa kawaida wa Kigoma watafaidikaje? watapanda ndege?

Ushindi upo, piga na linda kura yako isichakachuliwe na Chi Chi Em
 
 


Dilili ya kumi na moja
Wanamtumia hata mama Kikwete ktk kampeni, badala ya UWT kama ilivyokuwa siku za nyuma. UWT kama wamegoma vile maana hawana kitu cha kuwaambia akina mama maskini wa Tanzania CCM HAWAAMINIANI. AGALIA HATA KIPINDI CHA KUSAKA KURA ZA WADHAMINI WA KIKWETE. alimtumia Ridhiwani.
 
Vijijini wameamka, mijini kuna matatizo ya watu kutaka kuuza kura. Leo kaika kijiji nilikozaliwa mgombea wa CCM alishindwa kuhutubia mkutano wa kampeni kwa kuzomewa na watu wengi, kijiji cha Haydom - Mbulu, mwaka huu vijiji vya kule watu wengi wamekataa kudanganywa. Kila kona ni mjadala. Chadema ina nafsi kubwa ya kushinda mbulu.

Napenda muelewe kuwa vijiji vingi watu wameamka ila wasomi wachache hawataki kuelewa ufisadi wa CCM;

Zaidi tuelimishe watu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…